1 Samweli 28 Swahili & English

Listen/Download Audio
1 Samweli 28 (Swahili) 1st Samuel 28 (English)

Ikawa siku zile hao Wafilisti wakakusanya majeshi yao waende vitani, ili kupigana na Israeli. Naye Akishi akamwambia Daudi, Jua hakika ya kuwa wewe utatoka pamoja nami jeshini, wewe na watu wako. 1 Samweli 28:1

It happened in those days, that the Philistines gathered their hosts together for warfare, to fight with Israel. Achish said to David, Know you assuredly, that you shall go out with me in the host, you and your men.

Naye Daudi akamwambia Akishi, Vema, sasa utajua atakayoyatenda mtumishi wako. Naye Akishi akamwambia Daudi, Haya basi! Mimi nitakufanya wewe kuwa mlinda kichwa changu daima. 1 Samweli 28:2

David said to Achish, Therefore you shall know what your servant will do. Achish said to David, Therefore will I make you keeper of my head for ever.

Basi Samweli alikuwa amefariki dunia, nao Israeli wote walikuwa wamemwomboleza, na kumzika huko Rama, ndani ya mji wake mwenyewe. Tena Sauli alikuwa amewaondolea mbali hao wenye pepo wa utambuzi na wachawi katika nchi. 1 Samweli 28:3

Now Samuel was dead, and all Israel had lamented him, and buried him in Ramah, even in his own city. Saul had put away those who had familiar spirits, and the wizards, out of the land.

Nao Wafilisti wakakusanyika, wakaenda kufanya kambi huko Shunemu; naye Sauli akawakusanya Waisraeli wote, nao wakapiga hema katika Gilboa. 1 Samweli 28:4

The Philistines gathered themselves together, and came and encamped in Shunem: and Saul gathered all Israel together, and they encamped in Gilboa.

Basi alipowaona hao majeshi ya Wafilisti, huyo Sauli akaogopa, na moyo wake ukatetemeka sana. 1 Samweli 28:5

When Saul saw the host of the Philistines, he was afraid, and his heart trembled greatly.

Lakini Sauli alipouliza kwa Bwana, Bwana hakumjibu, wala kwa ndoto, wala kwa Urimu, wala kwa manabii. 1 Samweli 28:6

When Saul inquired of Yahweh, Yahweh didn't answer him, neither by dreams, nor by Urim, nor by prophets.

Ndipo Sauli akawaambia watumishi wake, Nitafutieni mwanamke mwenye pepo wa utambuzi, nipate kumwendea na kuuliza kwake. Watumishi wake wakamwambia, Tazama, yuko mwanamke mwenye pepo wa utambuzi huko Endori. 1 Samweli 28:7

Then said Saul to his servants, Seek me a woman who has a familiar spirit, that I may go to her, and inquire of her. His servants said to him, Behold, there is a woman who has a familiar spirit at En-dor.

Basi Sauli akajigeuza, na kuvaa mavazi mengine, kisha akaenda, yeye na watu wawili pamoja naye, wakamfikilia yule mwanamke usiku; akasema, Tafadhali unibashirie kwa utambuzi, ukanipandishie yeye nitakayemtaja kwako. 1 Samweli 28:8

Saul disguised himself, and put on other clothing, and went, he and two men with him, and they came to the woman by night: and he said, Please divine to me by the familiar spirit, and bring me up whoever I shall name to you.

Yule mwanamke akamwambia, Angalia, unajua alivyofanya Sauli, jinsi alivyowakatilia mbali hao wenye pepo wa utambuzi na wachawi katika nchi; mbona basi wanitegea tanzi uhai wangu, ili kuniua? 1 Samweli 28:9

The woman said to him, Behold, you know what Saul has done, how he has cut off those who have familiar spirits, and the wizards, out of the land: why then lay you a snare for my life, to cause me to die?

Naye Sauli akamwapia kwa Bwana, akasema, Aishivyo Bwana, haitakupata adhabu yo yote kwa jambo hili. 1 Samweli 28:10

Saul swore to her by Yahweh, saying, As Yahweh lives, there shall no punishment happen to you for this thing.

Ndipo yule mwanamke aliposema, Je! Ni nani nitakayekupandishia? Naye akasema, Nipandishie Samweli. 1 Samweli 28:11

Then said the woman, Whom shall I bring up to you? He said, Bring me up Samuel.

Hata yule mwanamke alipomwona Samweli alilia kwa sauti kuu; na yule mwanamke akamwambia Sauli, akasema, Mbona umenidanganya? Kwa kuwa wewe ndiwe Sauli. 1 Samweli 28:12

When the woman saw Samuel, she cried with a loud voice; and the woman spoke to Saul, saying, Why have you deceived me? for you are Saul.

Mfalme akamwambia Usiogope; waona nini? Yule mwanamke akamwambia Sauli, Naona mungu anatoka katika nchi. 1 Samweli 28:13

The king said to her, Don't be afraid: for what do you see? The woman said to Saul, I see a god coming up out of the earth.

Naye akamwuliza, Ni mfano wa nini? Akajibu, Ni mzee anazuka; naye amefunikwa vazi. Basi Sauli akatambua ya kwamba ndiye Samweli mwenyewe, akainama uso wake mpaka nchi, akasujudia. 1 Samweli 28:14

He said to her, What form is he of? She said, An old man comes up; and he is covered with a robe. Saul perceived that it was Samuel, and he bowed with his face to the ground, and did obeisance.

Ndipo Samweli akamwambia Sauli, Mbona umenitaabisha mimi, hata kunipandisha juu? Sauli akajibu, Mimi nimetaabika sana; kwa kuwa hao Wafilisti wananifanyia vita, naye Mungu ameniacha; hanijibu tena, wala kwa manabii, wala kwa ndoto; kwa hiyo nimekuita wewe, ili wewe unijulishe nifanyeje. 1 Samweli 28:15

Samuel said to Saul, Why have you disquieted me, to bring me up? Saul answered, I am sore distressed; for the Philistines make war against me, and God is departed from me, and answers me no more, neither by prophets, nor by dreams: therefore I have called you, that you may make known to me what I shall do.

Samweli akasema, Kwa nini kuniuliza mimi, akiwa Bwana amekuacha, naye amekuwa adui yako? 1 Samweli 28:16

Samuel said, Why then do you ask of me, seeing Yahweh is departed from you, and is become your adversary?

Yeye Bwana amekutendea kama alivyosema kwa kinywa changu; Bwana amekurarulia ufalme mkononi mwako, na kumpa jirani yako, yaani, Daudi. 1 Samweli 28:17

Yahweh has done to you, as he spoke by me: and Yahweh has torn the kingdom out of your hand, and given it to your neighbor, even to David.

Kwa sababu wewe hukuitii sauti ya Bwana, wala hukumtimilizia hasira yake kali juu ya Amaleki; kwa sababu hii Bwana amekutendea hili leo. 1 Samweli 28:18

Because you didn't obey the voice of Yahweh, and didn't execute his fierce wrath on Amalek, therefore has Yahweh done this thing to you this day.

Tena pamoja na wewe Bwana atawatia Israeli mikononi mwa Wafilisti; hata na kesho wewe na wanao mtakuwapo pamoja nami; tena Bwana atawatia jeshi la Israeli pia mikononi mwa Wafilisti. 1 Samweli 28:19

Moreover Yahweh will deliver Israel also with you into the hand of the Philistines; and tomorrow shall you and your sons be with me: Yahweh will deliver the host of Israel also into the hand of the Philistines.

Mara Sauli akaanguka chini kifulifuli, akaingiwa na hofu kuu kwa sababu ya maneno hayo ya Samweli, wala hakuwa na nguvu yo yote; kwa maana hakula chakula mchana kutwa, wala usiku kucha. 1 Samweli 28:20

Then Saul fell immediately his full length on the earth, and was sore afraid, because of the words of Samuel: and there was no strength in him; for he had eaten no bread all the day, nor all the night.

Ndipo yule mwanamke akamwendea Sauli, akamwona ya kuwa yeye ametaabika sana, akamwambia, Angalia, mjakazi wako ameisikiliza sauti yako, nami nimeutia uhai wangu mkononi mwangu, nami nimeyasikiliza maneno yako uliyoniambia. 1 Samweli 28:21

The woman came to Saul, and saw that he was sore troubled, and said to him, Behold, your handmaid has listened to your voice, and I have put my life in my hand, and have listened to your words which you spoke to me.

Basi sasa, tafadhali, wewe uisikilize sauti ya mjakazi wako, nikakuandalie ngaa mkate kidogo; ukale, ili upate nguvu, utakapokwenda zako. 1 Samweli 28:22

Now therefore, please listen also to the voice of your handmaid, and let me set a morsel of bread before you; and eat, that you may have strength, when you go on your way.

Lakini yeye alikataa, akasema, Mimi sitaki kula. Ila watumishi wake, pamoja na yule mwanamke, wakamlazimisha; naye akaisikiliza sauti yao. Basi akainuka hapo chini, akaketi juu ya kitanda. 1 Samweli 28:23

But he refused, and said, I will not eat. But his servants, together with the woman, constrained him; and he listened to their voice. So he arose from the earth, and sat on the bed.

Naye yule mwanamke alikuwa na ndama aliyenona nyumbani; akafanya haraka kumchinja; akatwaa na unga, akaukanda, akafanya mkate wa mofa kwa unga huo; 1 Samweli 28:24

The woman had a fattened calf in the house; and she hurried, and killed it; and she took flour, and kneaded it, and did bake unleavened bread of it:

kisha akamwandalia Sauli na watumishi wake; wakala. Ndipo wakaondoka, wakaenda zao usiku ule.

1 Samweli 28:25

and she brought it before Saul, and before his servants; and they ate. Then they rose up, and went away that night.