1 Samweli 24 Swahili & English

Listen/Download Audio
1 Samweli 24 (Swahili) 1st Samuel 24 (English)

Ikawa, Sauli aliporudi baada ya kuwafuatia Wafilisti, aliambiwa ya kwamba, Daudi yuko katika nyika ya Engedi. 1 Samweli 24:1

It happened, when Saul was returned from following the Philistines, that it was told him, saying, Behold, David is in the wilderness of En Gedi.

Ndipo Sauli akatwaa watu elfu waliochaguliwa katika Israeli wote, akaenda kumtafuta Daudi na watu wake juu ya majabali ya mbuzi-mwitu. 1 Samweli 24:2

Then Saul took three thousand chosen men out of all Israel, and went to seek David and his men on the rocks of the wild goats.

Akafika penye mazizi ya kondoo kando ya njia, na huko kulikuwa na pango; Sauli akaingia ndani ili kuifunika miguu. Na Daudi na watu wake walikuwa wakikaa mle pangoni ndani sana. 1 Samweli 24:3

He came to the sheep pens by the way, where was a cave; and Saul went in to cover his feet. Now David and his men were abiding in the innermost parts of the cave.

Nao watu wa Daudi wakamwambia, Tazama, hii ndiyo siku ile aliyokuambia Bwana, Angalia, nitamtia adui yako mikononi mwako, nawe utamtenda yo yote utakayoona kuwa mema. Basi Daudi akainuka, akaukata upindo wa vazi lake Sauli kwa siri. 1 Samweli 24:4

The men of David said to him, Behold, the day of which Yahweh said to you, Behold, I will deliver your enemy into your hand, and you shall do to him as it shall seem good to you. Then David arose, and cut off the skirt of Saul's robe secretly.

Lakini halafu, moyo wake Daudi ukamchoma, kwa sababu amekata upindo wa vazi lake Sauli. 1 Samweli 24:5

It happened afterward, that David's heart struck him, because he had cut off Saul's skirt.

Akawaambia watu wake, Hasha! Nisimtendee bwana wangu, masihi wa BWANA,neon hili,kuunyosha mkono wangu juu yake,kwa maana yeye ni masihi wa BWANA. 1 Samweli 24:6

He said to his men, Yahweh forbid that I should do this thing to my lord, Yahweh's anointed, to put forth my hand against him, seeing he is Yahweh's anointed.

Basi Daudi akawazuia watu wake kwa maneno hayo, asiwaache kumwondokea Sauli. Kisha Sauli akatoka pangoni, akaenda zake. 1 Samweli 24:7

So David checked his men with these words, and didn't allow them to rise against Saul. Saul rose up out of the cave, and went on his way.

Daudi naye akainuka baadaye, akatoka pangoni, akamwita Sauli, akisema, Bwana wangu, mfalme. Na Sauli alipotazama nyuma, Daudi akainama uso wake hata nchi, akamsujudia. 1 Samweli 24:8

David also arose afterward, and went out of the cave, and cried after Saul, saying, My lord the king. When Saul looked behind him, David bowed with his face to the earth, and did obeisance.

Daudi akamwambia Sauli, Kwa nini unasikiliza maneno ya watu wasemao, Tazama, Daudi anataka kukudhuru? 1 Samweli 24:9

David said to Saul, Why listen you to men's words, saying, Behold, David seeks your hurt?

Tazama, leo hivi macho yako yameona jinsi Bwana alivyokutia mikononi mwangu pangoni, na watu wengine wakaniambia nikuue; lakini nikakuacha; nikasema, Sitaki kuunyosha mkono wangu juu ya bwana wangu; kwa maana yeye ni masihi wa BWANA. 1 Samweli 24:10

Behold, this day your eyes have seen how that Yahweh had delivered you today into my hand in the cave: and some bade me kill you; but [my eye] spared you; and I said, I will not put forth my hand against my lord; for he is Yahweh's anointed.

Tena, baba yangu, tazama, tafadhali, tazama upindo wa vazi lako mkononi mwangu; maana ikiwa nimeukata upindo wa vazi lako, nisikuue, ujue, na kuona ya kuwa hakuna uovu wala kosa mkononi mwangu, wala sikukukosa neno; ingawa wewe unaniwinda roho yangu ili kuikamata. 1 Samweli 24:11

Moreover, my father, behold, yes, see the skirt of your robe in my hand; for in that I cut off the skirt of your robe, and didn't kill you, know you and see that there is neither evil nor disobedience in my hand, and I have not sinned against you, though you hunt after my life to take it.

Bwana atuamue, mimi na wewe, na Bwana anilipizie kisasi changu kwako; lakini mkono wangu hautakuwa juu yako. 1 Samweli 24:12

Yahweh judge between me and you, and Yahweh avenge me of you; but my hand shall not be on you.

Kama vile walivyosema watu wa kale katika mithali yao, Katika waovu hutoka uovu; ila mkono wangu hautakuwa juu yako. 1 Samweli 24:13

As says the proverb of the ancients, Out of the wicked comes forth wickedness; but my hand shall not be on you.

Na mfalme wa Israeli ametoka ili kumfuatia nani? Unamwinda nani? Ni kuwinda mbwa mfu, au kiroboto. 1 Samweli 24:14

After whom is the king of Israel come out? after whom do you pursue? after a dead dog, after a flea.

Basi Bwana atuamue, akatuhukumu mimi na wewe, akaone, akanitetee neno langu, akaniokoe na mkono wako. 1 Samweli 24:15

Yahweh therefore be judge, and give sentence between me and you, and see, and plead my cause, and deliver me out of your hand.

Ikawa, Daudi alipokwisha kumwambia Sauli maneno hayo Sauli alisema, Hii ndiyo sauti yako, Daudi, mwanangu? Naye Sauli akapaza sauti yake, akalia. 1 Samweli 24:16

It came to pass, when David had made an end of speaking these words to Saul, that Saul said, Is this your voice, my son David? Saul lifted up his voice, and wept.

Akamwambia Daudi, Wewe u mwenye haki kuliko mimi; maana wewe umenitendea mema, nami nimekutenda mabaya. 1 Samweli 24:17

He said to David, You are more righteous than I; for you have rendered to me good, whereas I have rendered to you evil.

Nawe umeonyesha leo jinsi ulivyonitendea mema, kwani Bwana aliponitia mikononi mwako, hukuniua. 1 Samweli 24:18

You have declared this day how that you have dealt well with me, because when Yahweh had delivered me up into your hand, you didn't kill me.

Maana mtu akimwona adui yake, je! Atamwacha aende zake salama? Basi Bwana na akulipe mema kwa haya uliyonitendea leo. 1 Samweli 24:19

For if a man finds his enemy, will he let him go away unharmed? Therefore may Yahweh reward you good for that which you have done to me this day.

Na sasa, angalia, najua ya kuwa hakika utakuwa mfalme, na ufalme wa Israeli utafanyika imara mkononi mwako. 1 Samweli 24:20

Now, behold, I know that you shall surely be king, and that the kingdom of Israel shall be established in your hand.

Basi sasa, uniapie kwa Bwana, ya kwamba hutawakatilia mbali wazao wangu baada yangu, wala hutaliharibu jina langu katika mbari ya baba yangu. 1 Samweli 24:21

Swear now therefore to me by Yahweh, that you will not cut off my seed after me, and that you will not destroy my name out of my father's house.

Naye Daudi akamwapia Sauli. Kisha Sauli akaenda zake kwao; lakini Daudi na watu wake wakapanda kwenda ngomeni. 1 Samweli 24:22

David swore to Saul. Saul went home; but David and his men got them up to the stronghold.