1 Samweli 12 Swahili & English

Listen/Download Audio
1 Samweli 12 (Swahili) 1st Samuel 12 (English)

Kisha Samweli akawaambia Israeli wote, Angalieni, nimeisikiliza sauti yenu katika hayo yote mliyoniambia, nami nimemtawaza mfalme juu yenu. 1 Samweli 12:1

Samuel said to all Israel, Behold, I have listened to your voice in all that you said to me, and have made a king over you.

Basi sasa, angalieni, mfalme anakwenda mbele yenu; na mimi ni mzee, mwenye mvi; tena, tazameni, wana wangu wapo pamoja nanyi; nami nimekwenda mbele yenu toka ujana wangu hata leo. 1 Samweli 12:2

Now, behold, the king walks before you; and I am old and gray-headed; and, behold, my sons are with you: and I have walked before you from my youth to this day.

Nami nipo hapa; basi, mnishuhudie mbele za Bwana, na mbele ya masihi wake,nalitwaa ng`ombe wa nani? au nalitwaa punda wa nani? au ni nani niliye mdhulumu? Ni nani niliyemwonea? Au kwa mkono wa nani nimepokea rushwa inipofushe macho? Nami nitawarudishia ninyi. 1 Samweli 12:3

Here I am: witness against me before Yahweh, and before his anointed: whose ox have I taken? or whose donkey have I taken? or whom have I defrauded? whom have I oppressed? or of whose hand have I taken a ransom to blind my eyes therewith? and I will restore it you.

Nao wakasema, hukutudhulumu, wala hukutuonea, wala hukupokea kitu kwa mkono wa mtu awaye yote. 1 Samweli 12:4

They said, You have not defrauded us, nor oppressed us, neither have you taken anything of any man's hand.

Akawaambia, Bwana ni shahidi juu yenu, na masihi 1 Samweli 12:5

He said to them, Yahweh is witness against you, and his anointed is witness this day, that you have not found anything in my hand. They said, He is witness.

Samweli akawaambia watu, Ni yeye Bwana aliyewaweka Musa na Haruni, ndiye yeye aliyewatoa baba zenu kutoka nchi ya Misri. 1 Samweli 12:6

Samuel said to the people, It is Yahweh who appointed Moses and Aaron, and that brought your fathers up out of the land of Egypt.

Basi sasa simameni, ili niwahutubie mbele za Bwana, kwa kutaja matendo yote ya haki ya Bwana, aliyowatendea ninyi na baba zenu. 1 Samweli 12:7

Now therefore stand still, that I may plead with you before Yahweh concerning all the righteous acts of Yahweh, which he did to you and to your fathers.

Yakobo alipokuwa ameingia Misri, na baba zenu walipomlilia Bwana, ndipo Bwana akawapeleka Musa na Haruni, nao wakawatoa baba zenu kutoka Misri, wakawakalisha mahali hapa. 1 Samweli 12:8

When Jacob was come into Egypt, and your fathers cried to Yahweh, then Yahweh sent Moses and Aaron, who brought forth your fathers out of Egypt, and made them to dwell in this place.

Lakini wakamsahau Bwana, Mungu wao, naye akawauza na kuwatia katika mikono ya Sisera, jemadari wa jeshi la Hazori, na katika mikono ya Wafilisti, na katika mikono ya mfalme wa Moabu, nao wakapigana nao. 1 Samweli 12:9

But they forgot Yahweh their God; and he sold them into the hand of Sisera, captain of the host of Hazor, and into the hand of the Philistines, and into the hand of the king of Moab; and they fought against them.

Nao wakamlilia Bwana, wakasema, Tumefanya dhambi, kwa kuwa tumemwacha Bwana, na kuwatumikia Mabaali na Maashtorethi; lakini sasa utuokoe na mikono ya adui zetu, nasi tutakutumikia wewe. 1 Samweli 12:10

They cried to Yahweh, and said, We have sinned, because we have forsaken Yahweh, and have served the Baals and the Ashtaroth: but now deliver us out of the hand of our enemies, and we will serve you.

Bwana akawatuma Yerubaali, na Baraka, na Yeftha, na Samweli, akawaokoa ninyi na mikono ya adui zenu pande zote, nanyi mkakaa salama. 1 Samweli 12:11

Yahweh sent Jerubbaal, and Bedan, and Jephthah, and Samuel, and delivered you out of the hand of your enemies on every side; and you lived in safety.

Hata mlipomwona Nahashi, mfalme wa wana wa Amoni, amekuja kupigana nanyi, mliniambia, Sivyo, lakini mfalme atatutawala; ingawa Bwana, Mungu wenu, ni mfalme wenu. 1 Samweli 12:12

When you saw that Nahash the king of the children of Ammon came against you, you said to me, No, but a king shall reign over us; when Yahweh your God was your king.

Basi sasa, mtazameni mfalme mliyemchagua na kumtaka; tazameni, Bwana ameweka mfalme juu yenu. 1 Samweli 12:13

Now therefore see the king whom you have chosen, and whom you have asked for: and, behold, Yahweh has set a king over you.

Kama mkimcha Bwana, na kumtumikia, na kuisikia sauti yake, msiiasi amri ya Bwana, tena kama ninyi, na mfalme anayewatawala, mkimfuata Bwana, Mungu wenu, vema! 1 Samweli 12:14

If you will fear Yahweh, and serve him, and listen to his voice, and not rebel against the commandment of Yahweh, and both you and also the king who reigns over you are followers of Yahweh your God, [well]:

Bali msipoisikia sauti ya Bwana, mkiiasi amri ya Bwana, ndipo mkono wa Bwana utakuwa juu yenu, kama ulivyokuwa juu ya baba zenu. 1 Samweli 12:15

but if you will not listen to the voice of Yahweh, but rebel against the commandment of Yahweh, then will the hand of Yahweh be against you, as it was against your fathers.

Na sasa simameni, mkalione jambo hili kubwa, Bwana atakalolitenda mbele ya macho yenu. 1 Samweli 12:16

Now therefore stand still and see this great thing, which Yahweh will do before your eyes.

Leo je! Si mavuno ya ngano? Nitamwomba Bwana, kwamba apeleke ngurumo na mvua; nanyi mtajua na kuona ya kuwa uovu wenu ni mwingi sana, mlioufanya machoni pa Bwana, kwa kujitakia mfalme. 1 Samweli 12:17

Isn't it wheat harvest today? I will call to Yahweh, that he may send thunder and rain; and you shall know and see that your wickedness is great, which you have done in the sight of Yahweh, in asking you a king.

Basi Samweli akamwomba Bwana, naye Bwana akapeleka ngurumo na mvua siku ile; nao watu wote wakamwogopa Bwana sana, na Samweli pia. 1 Samweli 12:18

So Samuel called to Yahweh; and Yahweh sent thunder and rain that day: and all the people greatly feared Yahweh and Samuel.

Watu wote wakamwambia Samweli, Utuombee sisi watumwa wako kwa Bwana, Mungu wako, tusije tukafa; maana tumeongeza dhambi zetu zote kwa uovu huu, wa kujitakia mfalme. 1 Samweli 12:19

All the people said to Samuel, Pray for your servants to Yahweh your God, that we not die; for we have added to all our sins [this] evil, to ask us a king.

Samweli akawaambia, Msiogope; ni kweli mmeutenda uovu huu wote; lakini msigeuke na kuacha kumfuata Bwana, bali mtumikieni Bwana kwa mioyo yenu yote. 1 Samweli 12:20

Samuel said to the people, "Don't be afraid; you have indeed done all this evil; yet don't turn aside from following Yahweh, but serve Yahweh with all your heart:

Wala msigeuke upande, maana, kufuata vitu vya ubatili, 1 Samweli 12:21

and don't turn aside; for [then would you go] after vain things which can't profit nor deliver, for they are vain.

visivyoweza kusaidia wala kuokoa, kwa kuwa havifai kitu. Maana Bwana hatawaacha watu wake kwa ajili ya jina lake kuu; kwa kuwa imempendeza Bwana kuwafanya ninyi kuwa watu wake mwenyewe. 1 Samweli 12:22

For Yahweh will not forsake his people for his great name's sake, because it has pleased Yahweh to make you a people to himself.

Walakini mimi, hasha! Nisimtende Bwana dhambi kwa kuacha kuwaombea ninyi; lakini nitawaelimisha katika njia iliyo njema, na kunyoka 1 Samweli 12:23

Moreover as for me, far be it from me that I should sin against Yahweh in ceasing to pray for you: but I will instruct you in the good and the right way.

Mcheni Bwana tu, mkamtumikie kwa kweli kwa mioyo yenu yote; maana, kumbukeni jinsi alivyowatendea mambo makuu. 1 Samweli 12:24

Only fear Yahweh, and serve him in truth with all your heart; for consider how great things he has done for you.

Lakini kama mkiendelea kutenda mabaya, mtaangamia, ninyi na mfalme wenu pia. 1 Samweli 12:25

But if you shall still do wickedly, you shall be consumed, both you and your king."