1 Samweli 23 Swahili & English

Listen/Download Audio
1 Samweli 23 (Swahili) 1st Samuel 23 (English)

Kisha wakamwambia Daudi, kusema, Angalia, Wafilisti wanapigana vita juu ya Keila na kuiba nafaka sakafuni mwa kupuria. 1 Samweli 23:1

They told David, saying, Behold, the Philistines are fighting against Keilah, and are robbing the threshing floors.

Basi Daudi akamwuliza Bwana, kusema, Je! Niende nikawapige hao Wafilisti? Naye Bwana akamwambia Daudi, Nenda ukawapige Wafilisti, na kuuokoa Keila. 1 Samweli 23:2

Therefore David inquired of Yahweh, saying, Shall I go and strike these Philistines? Yahweh said to David, Go, and strike the Philistines, and save Keilah.

Ila watu wake Daudi wakamwambia, Tazama, sisi tunaogopa hapa katika Yuda; je! Si zaidi tukienda Keila juu ya majeshi ya Wafilisti? 1 Samweli 23:3

David's men said to him, Behold, we are afraid here in Judah: how much more then if we go to Keilah against the armies of the Philistines?

Basi Daudi akamwuliza Bwana tena, Naye Bwana akamjibu, akasema, Ondoka, ukashukie Keila; kwa kuwa nitawatia hao Wafilisti mikononi mwako. 1 Samweli 23:4

Then David inquired of Yahweh yet again. Yahweh answered him, and said, Arise, go down to Keilah; for I will deliver the Philistines into your hand.

Ndipo wakaenda Keila, Daudi na watu wake, wakapigana na hao Wafilisti, wakateka nyara ng'ombe zao, na kuwaua uuaji mkuu. Hivyo Daudi akawaokoa watu wa Keila. 1 Samweli 23:5

David and his men went to Keilah, and fought with the Philistines, and brought away their cattle, and killed them with a great slaughter. So David saved the inhabitants of Keilah.

Ikawa Abiathari, mwana wa Ahimeleki, alipomkimbilia Daudi huko Keila, alishuka na naivera mkononi mwake. 1 Samweli 23:6

It happened, when Abiathar the son of Ahimelech fled to David to Keilah, that he came down with an ephod in his hand.

Kisha Sauli aliambiwa ya kwamba Daudi amefika Keila. Sauli akasema, Mungu amemtia mkononi mwangu; kwa maana amefungwa ndani, kwa vile alivyoingia katika mji wenye malango na makomeo. 1 Samweli 23:7

It was told Saul that David was come to Keilah. Saul said, God has delivered him into my hand; for he is shut in, by entering into a town that has gates and bars.

Basi Sauli akawaita watu wote waende vitani, ili waishukie Keila, na kumhusuru Daudi na watu wake. 1 Samweli 23:8

Saul summoned all the people to war, to go down to Keilah, to besiege David and his men.

Naye Daudi alifahamu ya kuwa Sauli amemkusudia mabaya; akamwambia Abiathari, kuhani, Lete hapa hiyo naivera. 1 Samweli 23:9

David knew that Saul was devising mischief against him; and he said to Abiathar the priest, Bring here the ephod.

Ndipo Daudi akasema, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mimi mtumwa wako nimesikia hakika ya kuwa Sauli anataka kuja huku Keila, ili kuuharibu mji kwa ajili yangu. 1 Samweli 23:10

Then said David, O Yahweh, the God of Israel, your servant has surely heard that Saul seeks to come to Keilah, to destroy the city for my sake.

Je! Watu wa Keila watanitoa, nitiwe mkononi mwake? Je! Sauli atashuka, kama mtumwa wako alivyosikia? Ee Bwana, Mungu wa Israeli, nakusihi, umwambie mtumwa wako. Naye Bwana akamjibu, Atashuka. 1 Samweli 23:11

Will the men of Keilah deliver me up into his hand? will Saul come down, as your servant has heard? Yahweh, the God of Israel, I beg you, tell your servant. Yahweh said, He will come down.

Ndipo Daudi akasema, Je! Watu wa Keila watanitia mimi na watu wangu mkononi mwake Sauli? Bwana akasema, Watakutia. 1 Samweli 23:12

Then said David, Will the men of Keilah deliver up to me and my men into the hand of Saul? Yahweh said, They will deliver you up.

Basi Daudi na watu wake, ambao wapata kama mia sita, wakaondoka na kutoka Keila, wakaenda po pote walipoweza kwenda. Kisha Sauli akaambiwa ya kwamba Daudi amekimbia toka Keila; akaacha kutoka nje. 1 Samweli 23:13

Then David and his men, who were about six hundred, arose and departed out of Keilah, and went wherever they could go. It was told Saul that David was escaped from Keilah; and he gave up going there.

Basi Daudi alikuwa akikaa nyikani ngomeni, akakaa katika nchi ya milima milima kwenye nyika ya Zifu. Naye Sauli alikuwa akimtafuta kila siku, lakini Mungu hakumtia mikononi mwake. 1 Samweli 23:14

David abode in the wilderness in the strongholds, and remained in the hill-country in the wilderness of Ziph. Saul sought him every day, but God didn't deliver him into his hand.

Daudi akaona ya kwamba Sauli ametoka nje ili kutafuta roho yake; naye Daudi akawako katika nyika ya Zifu, huko Horeshi. 1 Samweli 23:15

David saw that Saul had come out to seek his life: and David was in the wilderness of Ziph in the wood.

Ndipo Yonathani, mwana wa Sauli, akainuka akamwendea Daudi huko Horeshi, akamtia nguvu mkono wake katika Mungu. 1 Samweli 23:16

Jonathan, Saul's son, arose, and went to David into the wood, and strengthened his hand in God.

Akamwambia, Usiogope, kwa maana mkono wa Sauli, babangu, hautakupata; na wewe utakuwa mfalme juu ya Israeli; na mimi nitakuwa wa pili wako; ndivyo ajuavyo hata Sauli, babangu. 1 Samweli 23:17

He said to him, Don't be afraid; for the hand of Saul my father shall not find you; and you shall be king over Israel, and I shall be next to you; and that also Saul my father knows.

Na hao wawili wakafanya agano mbele za Bwana; Daudi naye akakaa huko Horeshi, na Yonathani akaenda nyumbani kwake. 1 Samweli 23:18

They two made a covenant before Yahweh: and David abode in the wood, and Jonathan went to his house.

Ndipo wale Wazifi wakakwea kwa Sauli huko Gibea, wakasema, Je! Yule Daudi hakujificha kwetu ngomeni mwa Horeshi, kilimani pa Hakila upande wa kusini wa Yeshimoni? 1 Samweli 23:19

Then came up the Ziphites to Saul to Gibeah, saying, Doesn't David hide himself with us in the strongholds in the wood, in the hill of Hachilah, which is on the south of the desert?

Basi sasa, Ee mfalme, ushuke, kama utakavyo nafsini mwako kushuka; na kazi yetu itakuwa kumtia mkononi mwa mfalme. 1 Samweli 23:20

Now therefore, O king, come down, according to all the desire of your soul to come down; and our part shall be to deliver him up into the king's hand.

Naye Sauli akasema, Na mbarikiwe ninyi na Bwana; kwa sababu mmenihurumia. 1 Samweli 23:21

Saul said, Blessed be you of Yahweh; for you have had compassion on me.

Nendeni, nawasihi, mkazidi kupata hakika, mkajue na kuona mahali pake anapojificha, tena ni nani aliyemwona huko; maana nimeambiwa ya kwamba atenda kwa hila nyingi. 1 Samweli 23:22

Please go make yet more sure, and know and see his place where his haunt is, [and] who has seen him there; for it is told me that he deals very subtly.

Chunguzeni basi, mkayajue maficho yake yote anapojificha; kisha njoni kwangu, tena msikose, nami nitakwenda pamoja nanyi; tena itakuwa, akiwapo katika nchi, mimi nitamtafuta-tafuta katika elfu zote za Yuda. 1 Samweli 23:23

See therefore, and take knowledge of all the lurking-places where he hides himself, and come you again to me of a certainty, and I will go with you: and it shall happen, if he be in the land, that I will search him out among all the thousands of Judah.

Nao wakaondoka, wakaenda Zifu kumtangulia Sauli; lakini Daudi na watu wake walikuwapo nyikani pa Maoni, katika Araba upande wa kusini wa jangwa. 1 Samweli 23:24

They arose, and went to Ziph before Saul: but David and his men were in the wilderness of Maon, in the Arabah on the south of the desert.

Basi Sauli na watu wake wakaenda kumtafuta. Watu wakamwambia Daudi; basi kwa hiyo akashuka mpaka mwambani, akakaa nyikani pa Maoni. Naye Sauli alipopata habari, alimwinda Daudi nyikani pa Maoni. 1 Samweli 23:25

Saul and his men went to seek him. They told David: why he came down to the rock, and abode in the wilderness of Maon. When Saul heard [that], he pursued after David in the wilderness of Maon.

Sauli akaenda upande huu wa mlima, na Daudi na watu wake wakaenda upande huu wa mlima; naye Daudi akafanya haraka sana kwenda zake kwa hofu ya Sauli; kwa sababu Sauli na watu wake wakamzunguka Daudi na watu wake ili kuwakamata. 1 Samweli 23:26

Saul went on this side of the mountain, and David and his men on that side of the mountain: and David made haste to get away for fear of Saul; for Saul and his men compassed David and his men round about to take them.

Lakini akaja mjumbe kwa Sauli, kusema, Njoo upesi, kwa kuwa Wafilisti wameishambulia nchi. 1 Samweli 23:27

But there came a messenger to Saul, saying, Haste you, and come; for the Philistines have made a raid on the land.

Basi Sauli akarudi kutoka kumwinda Daudi, akaenda kinyume cha Wafilisti; kwa hiyo wakapaita mahali pale, Selahamalekothi. 1 Samweli 23:28

So Saul returned from pursuing after David, and went against the Philistines: therefore they called that place Sela Hammahlekoth.

Naye Daudi akakwea kutoka huko, akakaa katika ngome ya Engedi. 1 Samweli 23:29

David went up from there, and lived in the strongholds of En Gedi.