1 Samweli 13 Swahili & English

Listen/Download Audio
1 Samweli 13 (Swahili) 1st Samuel 13 (English)

Sauli alikuwa na umri wa miaka kadha wa kadha hapo alipoanza kutawala;naye akatawala miaka kadha wa kadha juu ya Israeli. 1 Samweli 13:1

Saul was [forty] years old when he began to reign; and when he had reigned two years over Israel,

Naye Sauli alijichagulia watu elfu tatu wa Israeli; ambao katika hao, elfu mbili walikuwa pamoja na Sauli katika Mikmashi, na katika mlima wa Betheli na elfu moja pamoja na Yonathani katika Gibea ya Benyamini; nao wale watu waliosalia akawaruhusu waende kila mtu hemani kwake. 1 Samweli 13:2

Saul chose him three thousand men of Israel, of which two thousand were with Saul in Michmash and in the Mount of Bethel, and one thousand were with Jonathan in Gibeah of Benjamin: and the rest of the people he sent every man to his tent.

Yonathani akaipiga hiyo ngome ya Wafilisti, iliyokuwako huko Gibea, nao Wafilisti wakapata habari. Naye Sauli akapiga tarumbeta katika nchi yote, huku akisema, Na wasikie Waebrania. 1 Samweli 13:3

Jonathan struck the garrison of the Philistines that was in Geba: and the Philistines heard of it. Saul blew the trumpet throughout all the land, saying, Let the Hebrews hear.

Waisraeli wote wakasikia habari ya kwamba Sauli ameipiga hiyo ngome ya Wafilisti, na ya kwamba Waisraeli wamepata kuwa makuruhi kwa Wafilisti. Basi hao watu wakakusanyika pamoja kumfuata Sauli huko Gilgali. 1 Samweli 13:4

All Israel heard say that Saul had struck the garrison of the Philistines, and also that Israel was had in abomination with the Philistines. The people were gathered together after Saul to Gilgal.

Nao Wafilisti wakakusanyana ili wapigane na Waisraeli, magari thelathini elfu, na wapanda farasi sita elfu, na watu kama mchanga ulio ufuoni mwa bahari kwa wingi wao; wakapanda juu, wakapiga kambi yao katika Mikmashi, upande wa mashariki wa Beth-aveni. 1 Samweli 13:5

The Philistines assembled themselves together to fight with Israel, thirty thousand chariots, and six thousand horsemen, and people as the sand which is on the sea-shore in multitude: and they came up, and encamped in Michmash, eastward of Beth Aven.

Hata Waisraeli walipoona ya kuwa wa katika dhiki, (maana watu walifadhaishwa), ndipo hao watu wakajificha katika mapango, na katika vichaka, na katika miamba, na katika mashimo, na katika mabirika. 1 Samweli 13:6

When the men of Israel saw that they were in a strait (for the people were distressed), then the people did hide themselves in caves, and in thickets, and in rocks, and in coverts, and in pits.

Hata baadhi ya Waebrania walivuka Yordani, wakaingia nchi ya Gadi na Gileadi; lakini Sauli alikuwa akaliko huko Gilgali, nao watu wote wakamfuata wakitetemeka. 1 Samweli 13:7

Now some of the Hebrews had gone over the Jordan to the land of Gad and Gilead; but as for Saul, he was yet in Gilgal, and all the people followed him trembling.

Akangoja siku saba, kwa kadiri ya muhula uliowekwa na Samweli lakini Samweli hakuja Gilgali; na hao watu wakatawanyika mbali naye. 1 Samweli 13:8

He stayed seven days, according to the set time that Samuel [had appointed]: but Samuel didn't come to Gilgal; and the people were scattered from him.

Sauli akasema, Nileteeni hapa sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani. Akaitoa sadaka ya kuteketezwa. 1 Samweli 13:9

Saul said, Bring here the burnt offering to me, and the peace-offerings. He offered the burnt offering.

Hata mara alipokwisha kuitoa hiyo sadaka ya kuteketezwa, kumbe! Samweli akatokea. Naye Sauli akatoka kwenda kumlaki na kumsalimu. 1 Samweli 13:10

It came to pass that as soon as he had made an end of offering the burnt offering, behold, Samuel came; and Saul went out to meet him, that he might greet him.

Samweli akasema, Umefanya nini? Naye Sauli akasema, Ni kwa sababu naliona ya kuwa watu wanatawanyika mbali nami, na wewe hukuja siku zile zilizonenwa; nao Wafilisti wamekusanyika pamoja huko Mikmashi; 1 Samweli 13:11

Samuel said, What have you done? Saul said, Because I saw that the people were scattered from me, and that you didn't come within the days appointed, and that the Philistines assembled themselves together at Michmash;

basi nikasema, Wafilisti watanishukia sasa mpaka Gilgali, kabla sijaomba fadhili za Bwana; kwa hiyo nalijishurutisha, nikatoa sadaka ya kuteketezwa. 1 Samweli 13:12

therefore said I, Now will the Philistines come down on me to Gilgal, and I haven't entreated the favor of Yahweh: I forced myself therefore, and offered the burnt offering.

Naye Samweli akamwambia Sauli, Umefanya upumbavu; hukuishika amri ya Bwana, Mungu wako, aliyokuamuru; kwa maana Bwana angaliufanya ufalme wako kuwa imara juu ya Israeli milele. 1 Samweli 13:13

Samuel said to Saul, You have done foolishly; you have not kept the commandment of Yahweh your God, which he commanded you: for now would Yahweh have established your kingdom on Israel forever.

Lakini sasa ufalme wako hautadumu; Bwana amejitafutia mtu aupendezaye moyo wake, naye Bwana amemwamuru yeye kuwa mkuu juu ya watu wake, kwa sababu wewe hukulishika neno lile Bwana alilokuamuru. 1 Samweli 13:14

But now your kingdom shall not continue: Yahweh has sought him a man after his own heart, and Yahweh has appointed him to be prince over his people, because you have not kept that which Yahweh commanded you.

Basi Samweli akaondoka, akapanda kutoka Gilgali mpaka Gibea ya Benyamini. Naye Sauli akawahesabu watu waliokuwapo pamoja naye, wapata kama mia sita. 1 Samweli 13:15

Samuel arose, and got him up from Gilgal to Gibeah of Benjamin. Saul numbered the people who were present with him, about six hundred men.

Naye Sauli, na mwanawe Yonathani, na watu waliokuwapo pamoja nao, wakakaa huko Geba ya Benyamini; lakini Wafilisti wakatua katika Mikmashi. 1 Samweli 13:16

Saul, and Jonathan his son, and the people who were present with them, abode in Geba of Benjamin: but the Philistines encamped in Michmash.

Nao watekaji wa nyara wakatoka katika marago ya hao Wafilisti, vikosi vitatu; kikosi kimoja kikageukia njia iendayo Ofra, mpaka nchi ya Shuali; 1 Samweli 13:17

The spoilers came out of the camp of the Philistines in three companies: one company turned to the way that leads to Ophrah, to the land of Shual;

na kikosi kingine kikageukia njia iendayo Beth-horoni; na kikosi kingine kikageukia njia ya mpakani ielekeayo bonde la Seboimu upande wa nyika. 1 Samweli 13:18

and another company turned the way to Beth Horon; and another company turned the way of the border that looks down on the valley of Zeboim toward the wilderness.

Basi, hakuonekana mhunzi ye yote katika nchi yote ya Israeli; kwa kuwa Wafilisti walisema, Waebrania wasije wakajifanyizia panga au mikuki; 1 Samweli 13:19

Now there was no smith found throughout all the land of Israel; for the Philistines said, Lest the Hebrews make them swords or spears:

lakini Waisraeli wote hushuka kwa Wafilisti, ili kunoa kila mtu jembe lake, na mundu wake, na shoka lake, na sululu yake; 1 Samweli 13:20

but all the Israelites went down to the Philistines, to sharpen every man his plowshare, mattock, axe, and sickle;

ila walikuwa na tupa za kunolea sululu, na miundu, na mauma, na mashoka; na kwa kuinoa michokoo. 1 Samweli 13:21

yet they had a file for the mattocks, and for the plowshares, and for the forks, and for the axes, and to set the goads.

Hivyo ikawa, siku ya vita, haukuonekana mkononi mwa mtu ye yote, miongoni mwa watu waliokuwa pamoja na Sauli na Yonathani, upanga wala mkuki; isipokuwa Sauli mwenyewe na mwanawe Yonathani walikuwa navyo. 1 Samweli 13:22

So it came to pass in the day of battle, that there was neither sword nor spear found in the hand of any of the people who were with Saul and Jonathan: but with Saul and with Jonathan his son was there found.

Na jeshi la Wafilisti wakatoka hata mwanya wa Mikmashi. 1 Samweli 13:23

The garrison of the Philistines went out to the pass of Michmash.