1 Samweli 9 Swahili & English

Listen/Download Audio
1 Samweli 9 (Swahili) 1st Samuel 9 (English)

Basi, kulikuwa na mtu mmoja wa Benyamini, jina lake akiitwa Kishi, mwana wa Abieli, mwana wa Serori, mwana wa Bekorathi, mwana wa Afia, mwana wa Mbenyamini, mtu shujaa, mwenye nguvu. 1 Samweli 9:1

Now there was a man of Benjamin, whose name was Kish, the son of Abiel, the son of Zeror, the son of Becorath, the son of Aphiah, the son of a Benjamite, a mighty man of valor.

Naye alikuwa na mwana, aliyeitwa jina lake Sauli, kijana, tena mzuri; wala katika wana wa Israeli hakuwako mtu mzuri kuliko yeye; tangu mabega yake kwenda juu alikuwa mrefu kuliko watu wote. 1 Samweli 9:2

He had a son, whose name was Saul, an impressive young man; and there was not among the children of Israel a better person than he. From his shoulders and upward he was higher than any of the people.

Na punda za Kishi, baba yake Sauli, walikuwa wamepotea. Kishi akamwambia Sauli mwanawe, Haya basi, twaa mtumishi mmoja pamoja nawe, uondoke, uende ukawatafute punda hao. 1 Samweli 9:3

The donkeys of Kish, Saul's father, were lost. Kish said to Saul his son, Take now one of the servants with you, and arise, go seek the donkeys.

Naye akapita kati ya nchi ya milima milima ya Efraimu, akapita na kati ya nchi ya Shalisha, lakini hawakuwaona; kisha wakapita kati ya nchi ya Shaalimu, wala huko hawakuwako; wakapita kati ya nchi ya Wabenyamini, lakini hawakuwapata. 1 Samweli 9:4

He passed through the hill-country of Ephraim, and passed through the land of Shalishah, but they didn't find them: then they passed through the land of Shaalim, and there they weren't there: and he passed through the land of the Benjamites, but they didn't find them.

Hata walipofika nchi ya Sufu, Sauli akamwambia yule mtumishi aliyefuatana naye, Haya, na turudi, baba yangu asije akaacha kufikiri habari za punda akatufikiri sisi. 1 Samweli 9:5

When they had come to the land of Zuph, Saul said to his servant who was with him, Come, and let us return, lest my father leave off caring for the donkeys, and be anxious for us.

Naye akamwambia, Tazama, katika mji huu mna mtu wa Mungu, naye ni mtu mwenye kuheshimiwa; yote asemayo hutukia kweli kweli; basi, twende huko; labda yeye aweza kutuambia habari ya safari yetu tunayoiendea. 1 Samweli 9:6

He said to him, See now, there is in this city a man of God, and he is a man who is held in honor; all that he says comes surely to pass: now let us go there; peradventure he can tell us concerning our journey whereon we go.

Ndipo Sauli akamwambia mtumishi wake, Lakini angalia, kama tukienda, tumpelekee mtu huyo kitu gani? Maana chakula kimekwisha vyomboni mwetu, wala hapana zawadi ya kumpelekea mtu wa Mungu; tuna nini sisi? 1 Samweli 9:7

Then said Saul to his servant, But, behold, if we go, what shall we bring the man? for the bread is spent in our vessels, and there is not a present to bring to the man of God: what have we?

Yule mtumishi akamjibu Sauli, akasema, Tazama, mkononi mwangu nina robo ya shekeli ya fedha; nitampa huyo mtu wa Mungu fedha hiyo, atuambie njia yetu. 1 Samweli 9:8

The servant answered Saul again, and said, Behold, I have in my hand the fourth part of a shekel of silver: that will I give to the man of God, to tell us our way.

(Hapo zamani katika Israeli, mtu alipokwenda kuuliza neno kwa Mungu, husema hivi, Haya! Twende kwa mwonaji; maana mtu aitwaye sasa Nabii hapo zamani aliitwa Mwonaji.) 1 Samweli 9:9

(In earlier times in Israel, when a man went to inquire of God, thus he said, Come, and let us go to the seer; for he who is now called a Prophet was before called a Seer.)

Basi Sauli akamwambia mtumishi wake, Umesema vema; haya! Twende. Wakaenda mpaka mji ule aliokuwamo mtu wa Mungu. 1 Samweli 9:10

Then said Saul to his servant, Well said; come, let us go. So they went to the city where the man of God was.

Hata walipokwea kwenda mjini, wakakutana na wasichana, wanatoka kwenda kuteka maji; wakawaambia, Je! Mwonaji yuko? 1 Samweli 9:11

As they went up the ascent to the city, they found young maidens going out to draw water, and said to them, Is the seer here?

Nao wakawajibu, wakasema, Yuko; tazama, yuko huko mbele yako; fanyeni haraka sasa, maana hivi leo amekuja mjini; kwa sababu watu wana dhabihu leo katika mahali pa juu; 1 Samweli 9:12

They answered them, and said, He is; behold, [he is] before you: make haste now, for he is come today into the city; for the people have a sacrifice today in the high place:

mkiingia mjini tu, mara mtamwona, kabla hajakwea kwenda mahali pa juu ale chakula; maana, watu hawatakula hata yeye atakapokuja; kwa sababu yeye ndiye anayeibarikia dhabihu; kisha hao watu walioalikwa hula. Basi, kweeni sasa; maana wakati huu ndio mtakapomwona. 1 Samweli 9:13

as soon as you are come into the city, you shall immediately find him, before he goes up to the high place to eat; for the people will not eat until he come, because he does bless the sacrifice; [and] afterwards they eat who are invited. Now therefore get you up; for at this time you shall find him.

Nao wakakwea kwenda mjini; nao walipokuwa wakiingia mjini, tazama, Samweli akawatokea, kwenda mahali pa juu. 1 Samweli 9:14

They went up to the city; [and] as they came within the city, behold, Samuel came out toward them, to go up to the high place.

Basi Bwana alikuwa amemfunulia Samweli, siku moja kabla Sauli hajamwendea, akisema, 1 Samweli 9:15

Now Yahweh had revealed to Samuel a day before Saul came, saying,

Kesho, wakati kama huu, nitakuletea mtu kutoka nchi ya Benyamini, nawe mtie mafuta ili awe mkuu juu ya watu wangu Israeli, naye atawaokoa watu wangu na mikono ya Wafilisti; maana nimewaangalia watu wangu, kwa sababu kilio chao kimenifikilia. 1 Samweli 9:16

Tomorrow about this time I will send you a man out of the land of Benjamin, and you shall anoint him to be prince over my people Israel; and he shall save my people out of the hand of the Philistines: for I have looked on my people, because their cry is come to me.

Hata Samweli alipomwona Sauli, Bwana akamwambia, Huyu ndiye niliyekuambia habari zake; huyu ndiye atakayewamiliki watu wangu. 1 Samweli 9:17

When Samuel saw Saul, Yahweh said to him, Behold, the man of whom I spoke to you! this same shall have authority over my people.

Ndipo Sauli akamkaribia Samweli langoni, akasema, Tafadhali, uniambie, nyumba ya mwonaji iko wapi? 1 Samweli 9:18

Then Saul drew near to Samuel in the gate, and said, Tell me, Please, where the seer's house is.

Samweli akamjibu Sauli, akasema, Mimi ndimi mwonaji; tangulia mbele yangu ukwee mpaka mahali pa juu, kwa maana mtakula pamoja nami leo; kisha, asubuhi nitakuacha uende zako, nami nitakuambia yote uliyo nayo moyoni mwako. 1 Samweli 9:19

Samuel answered Saul, and said, I am the seer; go up before me to the high place, for you shall eat with me today: and in the morning I will let you go, and will tell you all that is in your heart.

Na wale punda zako waliopotea siku hizi tatu, usijiudhi kwa ajili yao; maana wameonekana. Na yote yaliyotamanika katika Israeli amewekewa nani? Si wewe, na nyumba yote ya baba yako? 1 Samweli 9:20

As for your donkeys who were lost three days ago, don't set your mind on them; for they are found. For whom is all that is desirable in Israel? Is it not for you, and for all your father's house?

Basi Sauli akajibu, akasema, Je! Mimi si Mbenyamini, mtu wa kabila iliyo ndogo kuliko kabila zote za Israeli? Na jamaa yangu nayo si ndogo kuliko jamaa zote za kabila ya Benyamini? Kwa nini basi, kuniambia hivyo? 1 Samweli 9:21

Saul answered, Am I not a Benjamite, of the smallest of the tribes of Israel? and my family the least of all the families of the tribe of Benjamin? why then speak you to me after this manner?

Naye Samweli akamtwaa Sauli na mtumishi wake, akawaleta ndani sebuleni, akawaketisha mahali pa heshima kati ya watu walioalikwa, nao jumla yao walikuwa kama watu thelathini. 1 Samweli 9:22

Samuel took Saul and his servant, and brought them into the guest-chamber, and made them sit in the best place among those who were invited, who were about thirty persons.

Samweli akamwambia mpishi, Lete ile sehemu niliyokupa, hiyo niliyokuambia, Iweke akiba. 1 Samweli 9:23

Samuel said to the cook, Bring the portion which I gave you, of which I said to you, Set it by you.

Basi mpishi akatwaa paja, na nyama iliyokuwa juu yake, akaiweka mbele ya Sauli. Samweli akasema, Iliyowekwa akiba ndiyo hiyo! Iweke mbele yako ule, kwa sababu umewekewa hiyo wewe hata wakati uliokusudiwa, maana nalisema, Nimewaalika watu. Basi Sauli akala pamoja na Samweli siku hiyo. 1 Samweli 9:24

The cook took up the thigh, and that which was on it, and set it before Saul. [Samuel] said, Behold, that which has been reserved! set it before you and eat; because to the appointed time has it been kept for you, for I said, I have invited the people. So Saul ate with Samuel that day.

Hata waliposhuka kutoka mahali pa juu na kufika mjini, akaongea na Sauli darini. 1 Samweli 9:25

When they were come down from the high place into the city, he talked with Saul on the housetop.

Nao wakaamka alfajiri; kisha ikawa, kulipopambazuka, Samweli akamwita Sauli darini, akisema, Inuka, nikupeleke kwenu. Basi Sauli akainuka, nao wakatoka wote wawili, yeye na Samweli. 1 Samweli 9:26

They arose early: and it happened about the spring of the day, that Samuel called to Saul on the housetop, saying, Up, that I may send you away. Saul arose, and they went out both of them, he and Samuel, abroad.

Hata walipokuwa wakishuka mwisho wa mji, Samweli akamwambia Sauli, Mwambie mtumishi atangulie, (naye akatangulia), bali wewe simama hapa sasa, ili nikuambie neno la Mungu.

1 Samweli 9:27

As they were going down at the end of the city, Samuel said to Saul, Bid the servant pass on before us (and he passed on), but stand you still first, that I may cause you to hear the word of God.