1 Samweli 6 Swahili & English

Listen/Download Audio
1 Samweli 6 (Swahili) 1st Samuel 6 (English)

Basi, hilo sanduku la Bwana lilikuwamo katika nchi ya Wafilisti muda wa miezi saba. 1 Samweli 6:1

The ark of Yahweh was in the country of the Philistines seven months.

Nao Wafilisti wakawaita makuhani na waaguzi, wakasema, Tulifanyieje sanduku la Bwana? Tuonyesheni jinsi tuwezavyo kulirudisha mahali pake. 1 Samweli 6:2

The Philistines called for the priests and the diviners, saying, "What shall we do with the ark of Yahweh? Show us with which we shall send it to its place."

Nao wakajibu, Mkilirudisha hilo sanduku la Mungu wa Israeli, msilirudishe kitupu; lakini msikose kumpelekea na matoleo ya kosa; hivyo mtapona, tena mtafunuliwa ni kwa sababu gani mkono wake haukuondolewa kwenu. 1 Samweli 6:3

They said, "If you send away the ark of the God of Israel, don't send it empty; but by all means return him a trespass-offering: then you shall be healed, and it shall be known to you why his hand is not removed from you."

Ndipo wakauliza, Na hayo matoleo ya kosa yatakuwa ya namna gani, hayo tutakayompelekea? Nao wakajibu, Na yawe majipu ya dhahabu matano, na panya wa dhahabu watano, sawasawa na idadi ya mashehe wa Wafilisti; kwa kuwa tauni moja ilikuwa juu yenu nyote, na juu ya mashehe wenu. 1 Samweli 6:4

Then they said, "What shall be the trespass-offering which we shall return to him?" They said, "Five golden tumors, and five golden mice, [according to] the number of the lords of the Philistines; for one plague was on you all, and on your lords.

Kwa hiyo mtafanyiza sanamu za majipu yenu, na sanamu za panya wenu waiharibuo nchi; nanyi mtamtukuza huyo Mungu wa Israeli; huenda ataupunguza uzito wa mkono wake juu yenu, na juu ya miungu yenu, na juu ya nchi yenu. 1 Samweli 6:5

Therefore you shall make images of your tumors, and images of your mice that mar the land; and you shall give glory to the God of Israel: peradventure he will lighten his hand from off you, and from off your gods, and from off your land.

Mbona, basi, mnaifanya migumu mioyo yenu, kama vile wale Wamisri, naye yule Farao, walivyoifanya migumu mioyo yao? Hata na hao, hapo alipokwisha kuwadhihaki, je! Hawakuwaruhusu watu, nao wakaenda zao? 1 Samweli 6:6

Why then do you harden your hearts, as the Egyptians and Pharaoh hardened their hearts? When he had worked wonderfully among them, didn't they let the people go, and they departed?

Basi sasa jifanyizieni gari jipya, mtwae na ng'ombe wake wawili wakamwao, ambao hawajafungwa nira, nanyi mkawafunge hao ng'ombe garini, na kuwaondoa ndama zao na kuwatia zizini; 1 Samweli 6:7

Now therefore take and prepare yourselves a new cart, and two milk cattle, on which there has come no yoke; and tie the cattle to the cart, and bring their calves home from them;

kisha, litwaeni hilo sanduku la Bwana, na kuliweka juu ya gari; na hivyo vitu vya dhahabu, mtakavyompelekea kuwa matoleo ya kosa, mvitie katika kasha kando yake; mkalipeleke sanduku, lipate kwenda. 1 Samweli 6:8

and take the ark of Yahweh, and lay it on the cart; and put the jewels of gold, which you return him for a trespass-offering, in a coffer by the side of it; and send it away, that it may go.

Kisha angalieni, likikwea kwa njia ya mpakani mwake kwenda Beth-shemeshi, basi, ndiye aliyetutenda uovu huo mkuu; la, sivyo, ndipo tutakapojua ya kwamba si mkono wake uliotupiga; ilikuwa ni ajali iliyotupata. 1 Samweli 6:9

Behold; if it goes up by the way of its own border to Beth-shemesh, then he has done us this great evil: but if not, then we shall know that it is not his hand that struck us; it was a chance that happened to us."

Basi watu wale walifanya hivyo; wakatwaa ng'ombe wawili wakamwao, wakawafunga garini, na ndama zao wakawafunga zizini; 1 Samweli 6:10

The men did so, and took two milk cattle, and tied them to the cart, and shut up their calves at home;

kisha wakaliweka sanduku la Bwana juu ya gari, pamoja na kasha lenye panya wa dhahabu na sanamu za majipu yao. 1 Samweli 6:11

and they put the ark of Yahweh on the cart, and the coffer with the mice of gold and the images of their tumors.

Na hao ng'ombe wakashika njia moja kwa moja kwenda Beth-shemeshi; wakaiandama njia ya barabara, wakaenda wakilia, lakini hawakugeukia upande wa kuume wala wa kushoto; na mashehe wa Wafilisti wakawafuata hata kuufikia mpaka wa Beth-shemeshi. 1 Samweli 6:12

The cattle took the straight way by the way to Beth-shemesh; they went along the highway, lowing as they went, and didn't turn aside to the right hand or to the left; and the lords of the Philistines went after them to the border of Beth-shemesh.

Nao watu wa Beth-shemeshi walikuwa wakivuna ngano yao bondeni; wakainua macho yao, wakaliona sanduku, wakafurahi sana kuliona. 1 Samweli 6:13

They of Beth-shemesh were reaping their wheat harvest in the valley; and they lifted up their eyes, and saw the ark, and rejoiced to see it.

Na lile gari likaingia katika konde la Yoshua wa Beth-shemeshi, na kusimama pale pale, palipokuwapo jiwe kubwa; basi wakaipasua miti ya lile gari, wakawatoa wale ng'ombe kuwa ni sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana. 1 Samweli 6:14

The cart came into the field of Joshua the Beth-shemite, and stood there, where there was a great stone: and they split the wood of the cart, and offered up the cattle for a burnt offering to Yahweh.

Nao Walawi walilishusha sanduku la Bwana, na lile kasha lililokuwa pamoja nalo, lenye vile vitu vya dhahabu; wakaviweka juu ya lile jiwe kubwa; nao watu wa Beth-shemeshi wakatoa sadaka za kuteketezwa, na kuchinja dhabihu siku iyo hiyo kwa Bwana. 1 Samweli 6:15

The Levites took down the ark of Yahweh, and the coffer that was with it, in which the jewels of gold were, and put them on the great stone: and the men of Beth-shemesh offered burnt offerings and sacrificed sacrifices the same day to Yahweh.

Na hao mashehe watano wa Wafilisti, hapo walipokwisha kuyaona hayo, walirejea Ekroni siku iyo hiyo. 1 Samweli 6:16

When the five lords of the Philistines had seen it, they returned to Ekron the same day.

Hii ndiyo hesabu ya yale majipu waliyoyapeleka wale Wafilisti, yawe matoleo ya kosa kwa Bwana; kwa Ashdodi moja, kwa Gaza moja, kwa Ashkeloni moja, kwa Gathi moja, na kwa Ekroni moja; 1 Samweli 6:17

These are the golden tumors which the Philistines returned for a trespass-offering to Yahweh: for Ashdod one, for Gaza one, for Ashkelon one, for Gath one, for Ekron one;

na panya wa dhahabu, kwa idadi ya miji yote ya Wafilisti, milki zao wale mashehe watano, miji yenye maboma na vijiji vya mashamba pia. Nalo lile jiwe kubwa, ambalo juu yake waliliweka sanduku la Bwana, liko hata hivi leo hapo kondeni pa Yoshua wa Beth-shemeshi. 1 Samweli 6:18

and the golden mice, according to the number of all the cities of the Philistines belonging to the five lords, both of fortified cities and of country villages, even to the great stone, whereon they set down the ark of Yahweh, [which stone remains] to this day in the field of Joshua the Beth-shemite.

Basi Bwana aliwapiga baadhi ya watu wa Beth-shemeshi, kwa sababu wamechungulia ndani ya hilo sanduku la Bwana, wapata watu sabini, na watu hamsini elfu; nao watu wakalalamika, kwa kuwa Bwana amewapiga watu kwa uuaji mkuu. 1 Samweli 6:19

He struck of the men of Beth-shemesh, because they had looked into the ark of Yahweh, he struck of the people fifty thousand seventy men; and the people mourned, because Yahweh had struck the people with a great slaughter.

Nao watu wa Beth-shemeshi wakasema, Ni nani awezaye kusimama mbele za Bwana, huyu Mungu mtakatifu? Naye atapanda kwenda kwa nani kutoka kwetu? 1 Samweli 6:20

The men of Beth-shemesh said, Who is able to stand before Yahweh, this holy God? and to whom shall he go up from us?

Nao wakatuma wajumbe waende kwa wenyeji wa Kiriath-yearimu, kusema, Wafilisti wamelirudisha sanduku la Bwana; basi shukeni, mkalichukue kwenu. 1 Samweli 6:21

They sent messengers to the inhabitants of Kiriath Jearim, saying, The Philistines have brought back the ark of Yahweh; come you down, and bring it up to you.