Mwanzo BSB

Mwanzo 7

Genesis Chapter 7

1
Bwana akamwambia Nuhu, Ingia wewe na jamaa yako yote katika safina; kwa maana nimekuona wewe u mwenye haki mbele zangu katika kizazi hiki.
Then the LORD said to Noah, “Go into the ark, you and all your family, because I have found you righteous in this generation.
2
Katika wanyama wote walio safi ujitwalie saba saba, mume na mke; na katika wanyama wasio safi wawili wawili, mume na mke.
You are to take with you seven pairs of every kind of clean animal, a male and its mate; a pair of every kind of unclean animal, a male and its mate;
3
Tena katika ndege wa angani saba saba, mume na mke; ili kuhifadhi hai mbegu juu ya uso wa nchi yote.
and seven pairs of every kind of bird of the air, male and female, to preserve their offspring on the face of all the earth.
4
Kwa maana baada ya siku saba nitainyeshea dunia mvua, siku arobaini mchana na usiku; na kila kilicho hai nilichokifanya juu ya uso wa nchi nitakifutilia mbali.
For seven days from now I will send rain on the earth for forty days and forty nights, and I will wipe from the face of the earth every living thing I have made.”
5
Nuhu akafanya kama vile Bwana alivyomwamuru.
And Noah did all that the LORD had commanded him.
6
Naye Nuhu alikuwa mtu wa miaka mia sita hapo hiyo gharika ya maji ilipokuwa juu ya nchi.
Now Noah was 600 years old when the floodwaters came upon the earth.
7
Nuhu akaingia katika safina, yeye, na wanawe, na mkewe, na wake za wanawe pamoja naye; kwa sababu ya maji ya gharika.
And Noah and his wife, with his sons and their wives, entered the ark to escape the waters of the flood.
8
Na katika wanyama walio safi, na wanyama wasio safi, na ndege, navyo vyote vitambaavyo juu ya nchi,
The clean and unclean animals, the birds, and everything that crawls along the ground
9
wakaingia katika safina alimo Nuhu, wawili wawili, mume na mke, kama vile Mungu alivyomwamuru Nuhu.
came to Noah to enter the ark, two by two, male and female, as God had commanded Noah.
10
Ikawa baada ya siku hizo saba, maji ya gharika yakawa juu ya nchi.
And after seven days the floodwaters came upon the earth.
11
Katika mwaka wa mia sita wa maisha ya Nuhu, mwezi wa pili, siku ya kumi na saba ya mwezi, siku ile chemchemi zote za vilindi vikuu zilibubujika kwa nguvu, madirisha ya mbinguni yakafunguka.
In the six hundredth year of Noah’s life, on the seventeenth day of the second month, all the fountains of the great deep burst forth, and the floodgates of the heavens were opened.
12
Mvua ikanyesha juu ya nchi, siku arobaini mchana na usiku.
And the rain fell upon the earth for forty days and forty nights.
13
Siku ile ile Nuhu akaingia katika safina, yeye, na Shemu na Hamu na Yafethi, wana wa Nuhu, na mkewe Nuhu, na wake watatu wa wanawe pamoja naye;
On that very day Noah entered the ark, along with his sons Shem, Ham, and Japheth, and his wife, and the three wives of his sons—
14
wao na kila mnyama wa mwitu kwa jinsi yake, na kila mnyama wa kufugwa kwa jinsi yake, na kila kitambaacho, chenye kutambaa juu ya nchi, kwa jinsi yake, na kirukacho kwa jinsi yake, kila ndege wa namna yo yote.
they and every kind of wild animal, livestock, crawling creature, bird, and winged creature.
15
Waliingia katika safina alimo Nuhu, wawili wawili, wa kila chenye mwili kilicho na pumzi ya uhai ndani yake.
They came to Noah to enter the ark, two by two of every creature with the breath of life.
16
Na walioingia, waliingia mume na mke, wa kila kitu chenye mwili, kama vile alivyomwamuru Mungu; Bwana akamfungia.
And they entered, the male and female of every living thing, as God had commanded Noah. Then the LORD shut him in.
17
Ile gharika ilikuwako juu ya nchi siku arobaini; nayo maji yakazidi, yakaieleza safina, ikaelea juu ya nchi.
For forty days the flood kept coming on the earth, and the waters rose and lifted the ark high above the earth.
18
Maji yakapata nguvu, yakazidi sana juu ya nchi; na ile safina ikaelea juu ya uso wa maji.
So the waters continued to surge and rise greatly on the earth, and the ark floated on the surface of the waters.
19
Maji yakapata nguvu sana sana juu ya nchi; na milima mirefu yote iliyokuwako chini ya mbingu ikafunikizwa.
Finally, the waters completely prevailed upon the earth, so that all the high mountains under all the heavens were covered.
20
Maji yakapata nguvu, hata ikafunikwa milima kiasi cha mikono kumi na mitano.
The waters rose and covered the mountaintops to a depth of fifteen cubits.
21
Wakafa wote wenye mwili waendao juu ya nchi, na ndege, na wanyama wa kufugwa, na kila mnyama wa mwitu, na kila kitambaacho chenye kutambaa juu ya nchi, na kila mwanadamu;
And every living thing that moved upon the earth perished—birds, livestock, animals, every creature that swarms upon the earth, and all mankind.
22
kila kitu chenye pumzi ya roho ya uhai puani mwake kikafa, kila kilichokuwako katika nchi kavu.
Of all that was on dry land, everything that had the breath of life in its nostrils died.
23
Kila kilicho hai juu ya uso wa nchi kikafutiliwa mbali tangu mwanadamu hata mnyama wa kufugwa, na kitambaacho, na ndege wa angani; vilifutiliwa mbali katika nchi, akabaki Nuhu tu, na hao walio pamoja naye katika safina.
And every living thing on the face of the earth was destroyed—man and livestock, crawling creatures and birds of the air; they were blotted out from the earth, and only Noah and those with him in the ark remained.
24
Maji yakapata nguvu juu ya nchi siku mia na hamsini.
And the waters prevailed upon the earth for 150 days.

Chagua Sura