1
Hiki ndicho kitabu cha vizazi vya Adamu. Siku ile Mungu alipoumba mtu, kwa sura ya Mungu alimfanya;
This is the book of the generations of Adam. In the day that God created man, He made him in His own likeness.
2
mwanamume na mwanamke aliwaumba, akawabariki akawaita jina lao Adamu, siku ile walipoumbwa.
Male and female He created them, and He blessed them. And in the day they were created, He called them “man.”
3
Adamu akaishi miaka mia na thelathini, akazaa mwana kwa sura yake, kwa mfano wake, akamwita jina lake Sethi.
When Adam was 130 years old, he had a son in his own likeness, after his own image; and he named him Seth.
4
Siku za Adamu baada ya kumzaa Sethi zilikuwa miaka mia nane, akazaa wana, waume na wake.
And after he had become the father of Seth, Adam lived 800 years and had other sons and daughters.
5
Siku zote za Adamu alizoishi ni miaka mia kenda na thelathini, naye akafa.
So Adam lived a total of 930 years, and then he died.
6
Sethi akaishi miaka mia na mitano, akamzaa Enoshi.
When Seth was 105 years old, he became the father of Enosh.
7
Sethi akaishi baada ya kumzaa Enoshi miaka mia nane na saba, akazaa wana, waume na wake.
And after he had become the father of Enosh, Seth lived 807 years and had other sons and daughters.
8
Siku zote za Sethi ni miaka mia kenda na kumi na miwili, akafa.
So Seth lived a total of 912 years, and then he died.
9
Enoshi akaishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
When Enosh was 90 years old, he became the father of Kenan.
10
Enoshi akaishi baada ya kumzaa Kenani miaka mia nane na kumi na mitano, akazaa wana, waume na wake.
And after he had become the father of Kenan, Enosh lived 815 years and had other sons and daughters.
11
Siku zote za Enoshi ni miaka mia kenda na mitano, akafa.
So Enosh lived a total of 905 years, and then he died.
12
Kenani akaishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
When Kenan was 70 years old, he became the father of Mahalalel.
13
Kenani akaishi baada ya kumzaa Mahalaleli miaka mia nane na arobaini, akazaa wana, waume na wake.
And after he had become the father of Mahalalel, Kenan lived 840 years and had other sons and daughters.
14
Siku zote za Kenani ni miaka mia kenda na kumi, akafa.
So Kenan lived a total of 910 years, and then he died.
15
Mahalaleli akaishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi.
When Mahalalel was 65 years old, he became the father of Jared.
16
Mahalaleli akaishi baada ya kumzaa Yaredi miaka mia nane na thelathini, akazaa wana, waume na wake.
And after he had become the father of Jared, Mahalalel lived 830 years and had other sons and daughters.
17
Siku zote za Mahalaleli ni miaka mia nane na tisini na mitano, akafa.
So Mahalalel lived a total of 895 years, and then he died.
18
Yaredi akaishi miaka mia na sitini na miwili, akamzaa Henoko.
When Jared was 162 years old, he became the father of Enoch.
19
Yaredi akaishi baada ya kumzaa Henoko miaka mia nane, akazaa wana, waume na wake.
And after he had become the father of Enoch, Jared lived 800 years and had other sons and daughters.
20
Siku zote za Yaredi ni miaka mia kenda na sitini na miwili, akafa.
So Jared lived a total of 962 years, and then he died.
21
Henoko akaishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela.
When Enoch was 65 years old, he became the father of Methuselah.
22
Henoko akaenda pamoja na Mungu baada ya kumzaa Methusela miaka mia tatu, akazaa wana, waume na wake.
And after he had become the father of Methuselah, Enoch walked with God 300 years and had other sons and daughters.
23
Siku zote za Henoko ni miaka mia tatu na sitini na mitano.
So Enoch lived a total of 365 years.
24
Henoko akaenda pamoja na Mungu, naye akatoweka, maana Mungu alimtwaa.
Enoch walked with God, and then he was no more, because God had taken him away.
25
Methusela akaishi miaka mia na themanini na saba, akamzaa Lameki.
When Methuselah was 187 years old, he became the father of Lamech.
26
Methusela akaishi baada ya kumzaa Lameki miaka mia saba na themanini na miwili, akazaa wana, waume na wake.
And after he had become the father of Lamech, Methuselah lived 782 years and had other sons and daughters.
27
Siku zote za Methusela ni miaka mia kenda na sitini na kenda, akafa.
So Methuselah lived a total of 969 years, and then he died.
28
Lameki akaishi miaka mia na themanini na miwili, akazaa mwana.
When Lamech was 182 years old, he had a son.
29
Akamwita jina lake Nuhu, akinena, Huyu ndiye atakayetufariji kwa kazi yetu na kwa taabu ya mikono yetu katika nchi aliyoilaani Bwana.
And he named him Noah, saying, “May this one comfort us in the labor and toil of our hands caused by the ground that the LORD has cursed.”
30
Lameki akaishi baada ya kumzaa Nuhu miaka mia na tisini na mitano, akazaa wana, waume na wake.
And after he had become the father of Noah, Lamech lived 595 years and had other sons and daughters.
31
Siku zote za Lameki ni miaka mia saba na sabini na saba, akafa.
So Lamech lived a total of 777 years, and then he died.
32
Nuhu alikuwa mwenye miaka mia tano, Nuhu akawazaa Shemu, na Hamu, na Yafethi.
After Noah was 500 years old, he became the father of Shem, Ham, and Japheth.