Mwanzo BSB

Mwanzo 21

Genesis Chapter 21

1
Bwana akamjia Sara kama alivyonena, na Bwana akamfanyia kama alivyosema.
Now the LORD attended to Sarah as He had said, and the LORD did for Sarah what He had promised.
2
Sara akapata mimba akamzalia Ibrahimu mwana wa kiume katika uzee wake, kwa muhula alioambiwa na Mungu.
So Sarah conceived and bore a son to Abraham in his old age, at the very time God had promised.
3
Ibrahimu akamwita jina lake Isaka, yule mwana aliyezaliwa, ambaye Sara alimzalia.
And Abraham gave the name Isaac to the son Sarah bore to him.
4
Ibrahimu akamtahiri Isaka mwanawe, alipokuwa mwenye siku nane, kama Mungu alivyomwamuru.
When his son Isaac was eight days old, Abraham circumcised him, as God had commanded him.
5
Naye Ibrahimu alikuwa mtu wa miaka mia, alipozaliwa mwana wake Isaka.
Abraham was a hundred years old when his son Isaac was born to him.
6
Sara akasema, Mungu amenifanyia kicheko; kila asikiaye atacheka pamoja nami.
Then Sarah said, “God has made me laugh, and everyone who hears of this will laugh with me.”
7
Akasema, N'nani angemwambia Ibrahimu, Sara atanyonyesha wana? Maana nimemzalia mwana katika uzee wake.
She added, “Who would have told Abraham that Sarah would nurse children? Yet I have borne him a son in his old age.”
8
Mtoto akakua, akaachishwa kunyonya; Ibrahimu akafanya karamu kuu siku ile Isaka alipoachishwa kunyonya.
So the child grew and was weaned, and Abraham held a great feast on the day Isaac was weaned.
9
Sara akamwona yule mwana wa Hajiri Mmisri, ambaye alimzalia Ibrahimu, anafanya dhihaka.
But Sarah saw that the son whom Hagar the Egyptian had borne to Abraham was mocking her son,
10
Kwa hiyo akamwambia Ibrahimu, Mfukuze mjakazi huyu na mwanawe, maana mwana wa mjakazi hatarithi pamoja na mwanangu, Isaka.
and she said to Abraham, “Expel the slave woman and her son, for the slave woman’s son will never share in the inheritance with my son Isaac!”
11
Na neno hilo lilikuwa baya sana machoni pa Ibrahimu, kwa ajili ya mwanawe.
Now this matter distressed Abraham greatly because it concerned his son Ishmael.
12
Mungu akamwambia Ibrahimu, Neno hili lisiwe baya machoni pako, kwa ajili ya huyo mwana, na huyo mjakazi wako. Kila akuambialo Sara, sikiza sauti yake, kwa maana katika Isaka uzao wako utaitwa.
But God said to Abraham, “Do not be distressed about the boy and your maidservant. Listen to everything that Sarah tells you, for through Isaac your offspring will be reckoned.
13
Naye mwana wa mjakazi nitamfanya kuwa taifa, maana huyu naye ni uzao wako.
But I will also make a nation of the slave woman’s son, because he is your offspring.”
14
Ibrahimu akaamka asubuhi na mapema akatwaa mkate na kiriba cha maji, akampa Hajiri akimtwika begani pake, na kijana, akamruhusu; naye akatoka, akapotea katika jangwa la Beer-sheba.
Early in the morning, Abraham got up, took bread and a skin of water, put them on Hagar’s shoulders, and sent her away with the boy. She left and wandered in the Wilderness of Beersheba.
15
Yale maji yakaisha katika kiriba, akamlaza kijana chini ya kijiti kimoja.
When the water in the skin was gone, she left the boy under one of the bushes.
16
Akaenda akakaa akimkabili, mbali naye kadiri ya mtupo wa mshale; maana alisema, Nisimwone kijana akifa; naye akakaa akimkabili, akapaza sauti yake, akalia.
Then she went off and sat down nearby, about a bowshot away, for she said, “I cannot bear to watch the boy die!” And as she sat nearby, she lifted up her voice and wept.
17
Mungu akasikia sauti ya kijana. Malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia, Una nini, Hajiri? Usiogope, maana Mungu amesikia sauti ya kijana huko aliko.
Then God heard the voice of the boy, and the angel of God called to Hagar from heaven, “What is wrong, Hagar? Do not be afraid, for God has heard the voice of the boy where he lies.
18
Ondoka, ukamwinue kijana, ukamshike mkononi mwako, kwa kuwa nitamfanya kuwa taifa kubwa.
Get up, lift up the boy, and take him by the hand, for I will make him into a great nation.”
19
Mungu akamfumbua macho, naye akaona kisima cha maji; akaenda akakijaza kiriba maji, akamnywesha kijana.
Then God opened her eyes, and she saw a well of water. So she went and filled the skin with water and gave the boy a drink.
20
Mungu akawa pamoja na huyo kijana, naye akakua, akakaa katika jangwa, akawa mpiga upinde.
And God was with the boy, and he grew up and settled in the wilderness and became a great archer.
21
Akakaa katika jangwa la Parani; mama yake akamtwalia mke katika nchi ya Misri.
And while he was dwelling in the Wilderness of Paran, his mother got a wife for him from the land of Egypt.
22
Ikawa wakati ule Abimeleki, na Fikoli mkuu wa jeshi lake, wakamwambia Ibrahimu, wakinena, Mungu yu pamoja nawe katika yote unayotenda.
At that time Abimelech and Phicol the commander of his army said to Abraham, “God is with you in all that you do.
23
Basi sasa uniapie kwa Mungu, ya kuwa hutanitenda hila, wala mwanangu, wala mjukuu wangu, lakini kwa kadiri ya fadhili niliyokutendea utanitendea mimi, na nchi hii ambayo umetembea ndani yake.
Now, therefore, swear to me here before God that you will not deal falsely with me or my children or descendants. Show to me and to the country in which you reside the same kindness that I have shown to you.”
24
Ibrahimu akasema, Nitaapa.
And Abraham replied, “I swear it.”
25
Kisha Ibrahimu akamlaumu Abimeleki kwa sababu ya kisima cha maji ambacho watumwa wa Abimeleki wamekinyang'anya.
But when Abraham complained to Abimelech about a well that Abimelech’s servants had seized,
26
Abimeleki akasema, Mimi sijui ni nani aliyetenda neno hili, wala hukuniambia, wala sikusikia habari hii ila leo tu.
Abimelech replied, “I do not know who has done this. You did not tell me, so I have not heard about it until today.”
27
Ibrahimu akatwaa kondoo na ng'ombe akampa Abimeleki, na hao wawili wakafanya mapatano.
So Abraham brought sheep and cattle and gave them to Abimelech, and the two men made a covenant.
28
Ibrahimu akaweka wana kondoo wa kike saba peke yao.
Abraham separated seven ewe lambs from the flock,
29
Abimeleki akamwambia Ibrahimu, Hawa wana kondoo wa kike saba, uliowaweka peke yao, maana yake nini?
and Abimelech asked him, “Why have you set apart these seven ewe lambs?”
30
Akasema, Hawa wana kondoo wa kike saba utawapokea mkononi mwangu, wawe ushuhuda ya kuwa ni mimi niliyekichimba kisima hiki.
He replied, “You are to accept the seven ewe lambs from my hand as my witness that I dug this well.”
31
Kwa hiyo akapaita mahali pale Beer-sheba, kwa sababu waliapa huko wote wawili.
So that place was called Beersheba, because it was there that the two of them swore an oath.
32
Basi wakafanya mapatano huko Beer-sheba. Abimeleki, na Fikoli mkuu wa jeshi lake, wakaondoka wakarudi hata nchi ya Wafilisti.
After they had made the covenant at Beersheba, Abimelech and Phicol the commander of his army got up and returned to the land of the Philistines.
33
Ibrahimu akapanda mkwaju huko Beer-sheba, akaliitia huko jina la Bwana Mungu wa milele.
And Abraham planted a tamarisk tree in Beersheba, and there he called upon the name of the LORD, the Eternal God.
34
Ibrahimu akakaa hali ya ugeni katika nchi ya Wafilisti siku nyingi.
And Abraham resided in the land of the Philistines for a long time.

Chagua Sura