1
Basi mbingu na nchi zikamalizika, na jeshi lake lote.
Thus the heavens and the earth were completed in all their vast array.
2
Na siku ya saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyoifanya; akastarehe siku ya saba, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoifanya.
And by the seventh day God had finished the work He had been doing; so on that day He rested from all His work.
3
Mungu akaibarikia siku ya saba, akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya.
Then God blessed the seventh day and sanctified it, because on that day He rested from all the work of creation that He had accomplished.
4
Hivyo ndivyo vizazi vya mbingu na nchi zilipoumbwa. Siku ile Bwana Mungu alipoziumba mbingu na nchi
This is the account of the heavens and the earth when they were created, in the day that the LORD God made them.
5
hapakuwa na mche wa kondeni bado, wala mboga ya kondeni haijachipuka bado, kwa maana Bwana Mungu hajainyeshea nchi mvua, wala hapana mtu wa kuilima ardhi;
Now no shrub of the field had yet appeared on the earth, nor had any plant of the field sprouted, for the LORD God had not yet sent rain upon the earth, and there was no man to cultivate the ground.
6
ukungu ukapanda katika nchi, ukatia maji juu ya uso wote wa ardhi.
But springs welled up from the earth and watered the whole surface of the ground.
7
Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.
Then the LORD God formed man from the dust of the ground and breathed the breath of life into his nostrils, and the man became a living being.
8
Bwana Mungu akapanda bustani upande wa mashariki wa Edeni, akamweka ndani yake huyo mtu aliyemfanya.
And the LORD God planted a garden in Eden, in the east, where He placed the man He had formed.
9
Bwana Mungu akachipusha katika ardhi kila mti unaotamanika kwa macho na kufaa kwa kuliwa; na mti wa uzima katikati ya bustani, na mti wa ujuzi wa mema na mabaya.
Out of the ground the LORD God gave growth to every tree that is pleasing to the eye and good for food. And in the middle of the garden were the tree of life and the tree of the knowledge of good and evil.
10
Ukatoka mto katika Edeni wa kuitilia bustani maji, na kutokea hapo ukagawanyika kuwa vichwa vinne.
Now a river flowed out of Eden to water the garden, and from there it branched into four headwaters:
11
Jina la wa kwanza ni Pishoni; ndio unaozunguka nchi yote ya Havila, ambako kuna dhahabu;
The name of the first river is the Pishon; it winds through the whole land of Havilah, where there is gold.
12
na dhahabu ya nchi ile ni njema; huko kuna bedola, na vito shoham.
And the gold of that land is pure, and bdellium and onyx are found there.
13
Na jina la mto wa pili ni Gihoni; ndio unaozunguka nchi yote ya Kushi.
The name of the second river is the Gihon; it winds through the whole land of Cush.
14
Na jina la mto wa tatu ni Hidekeli; ndio unaopita mbele ya Ashuru. Na mto wa nne ni Frati.
The name of the third river is the Tigris; it runs along the east side of Assyria. And the fourth river is the Euphrates.
15
Bwana Mungu akamtwaa huyo mtu, akamweka katika bustani ya Edeni, ailime na kuitunza.
Then the LORD God took the man and placed him in the Garden of Eden to cultivate and keep it.
16
Bwana Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula,
And the LORD God commanded him, “You may eat freely from every tree of the garden,
17
walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.
but you must not eat from the tree of the knowledge of good and evil; for in the day that you eat of it, you will surely die.”
18
Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.
The LORD God also said, “It is not good for the man to be alone. I will make for him a suitable helper.”
19
Bwana Mungu akafanyiza kutoka katika ardhi kila mnyama wa msituni, na kila ndege wa angani, akamletea Adamu ili aone atawaitaje; kila kiumbe hai, jina alilokiita Adamu likawa ndilo jina lake.
And out of the ground the LORD God formed every beast of the field and every bird of the air, and He brought them to the man to see what he would name each one. And whatever the man called each living creature, that was its name.
20
Adamu akawapa majina yao kila mnyama wa kufugwa, na ndege wa angani, na kila mnyama wa mwituni; lakini hakuonekana wa kumsaidia Adamu aliyefanana naye.
The man gave names to all the livestock, to the birds of the air, and to every beast of the field. But for Adam no suitable helper was found.
21
Bwana Mungu akamletea Adamu usingizi mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake,
So the LORD God caused the man to fall into a deep sleep, and while he slept, He took one of the man’s ribs and closed up the area with flesh.
22
na ule ubavu alioutwaa katika Adamu Bwana Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu.
And from the rib that the LORD God had taken from the man, He made a woman and brought her to him.
23
Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume.
And the man said: “This is now bone of my bones and flesh of my flesh; she shall be called ‘woman,’ for out of man she was taken.”
24
Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.
For this reason a man will leave his father and mother and be united to his wife, and they will become one flesh.
25
Nao walikuwa uchi wote wawili, Adamu na mkewe, wala hawakuona haya.
And the man and his wife were both naked, and they were not ashamed.