2 Mambo ya Nyakati 15 Swahili & English

Listen/Download Audio
2 Mambo ya Nyakati 15 (Swahili) 2nd Chronicles 15 (English)

Ndipo roho ya Mungu ikamjia Azaria mwana wa Odedi; 2 Mambo ya Nyakati 15:1

The Spirit of God came on Azariah the son of Oded:

naye akatoka ili amlaki Asa, akamwambia, Nisikieni, Ee Asa, na Yuda wote na Benyamini; Bwana yu pamoja nanyi, mkiwa pamoja naye; nanyi mkimtafuta ataonekana kwenu; lakini mkimwacha atawaacha ninyi. 2 Mambo ya Nyakati 15:2

and he went out to meet Asa, and said to him, Hear you me, Asa, and all Judah and Benjamin: Yahweh is with you, while you are with him; and if you seek him, he will be found of you; but if you forsake him, he will forsake you.

Basi tangu siku nyingi Israeli wamekuwa hawana Mungu wa kweli, wala hawana kuhani afundishaye, wala hawana torati; 2 Mambo ya Nyakati 15:3

Now for a long season Israel was without the true God, and without a teaching priest, and without law:

lakini walipomgeukia Bwana, Mungu wa Israeli, katika msiba wao, na kumtafuta, akaonekana kwao. 2 Mambo ya Nyakati 15:4

But when in their distress they turned to Yahweh, the God of Israel, and sought him, he was found of them.

Hata na zamani zile hakukuwa na amani kwake atokaye, wala kwake aingiaye, ila fadhaa kubwa juu yao wote wakaao katika nchi. 2 Mambo ya Nyakati 15:5

In those times there was no peace to him who went out, nor to him who came in; but great vexations were on all the inhabitants of the lands.

Wakavunjika-vunjika, taifa juu ya taifa, na mji juu ya mji; kwani Mungu aliwafadhaisha kwa shida zote. 2 Mambo ya Nyakati 15:6

They were broken in pieces, nation against nation, and city against city; for God did vex them with all adversity.

Nanyi jipeni nguvu, wala mikono yenu isilegee; kwa maana kazi yenu itakuwa na ijara. 2 Mambo ya Nyakati 15:7

But be you strong, and don't let your hands be slack; for your work shall be rewarded.

Naye Asa alipoyasikia maneno hayo, yaani, unabii wa mwana wa Odedi nabii, akatiwa nguvu, akayaondolea mbali machukizo yote katika nchi ya Yuda na Benyamini, na katika miji aliyoitwaa milimani mwa Efraimu; akaifanyiza tena madhabahu ya Bwana, iliyokuwako mbele ya ukumbi wa Bwana. 2 Mambo ya Nyakati 15:8

When Asa heard these words, and the prophecy of Oded the prophet, he took courage, and put away the abominations out of all the land of Judah and Benjamin, and out of the cities which he had taken from the hill-country of Ephraim; and he renewed the altar of Yahweh, that was before the porch of Yahweh.

Akakusanya Yuda wote na Benyamini, na hao wageni waliokaa kwao, wa Efraimu, na wa Manase, na wa Simeoni; kwa kuwa walimwangukia wengi katika Israeli, walipoona kwamba Bwana, Mungu wake, alikuwa pamoja naye. 2 Mambo ya Nyakati 15:9

He gathered all Judah and Benjamin, and those who sojourned with them out of Ephraim and Manasseh, and out of Simeon: for they fell to him out of Israel in abundance, when they saw that Yahweh his God was with him.

Basi wakakusanyika huko Yerusalemu mwezi wa tatu, katika mwaka wa kumi na tano wa kumiliki kwake Asa. 2 Mambo ya Nyakati 15:10

So they gathered themselves together at Jerusalem in the third month, in the fifteenth year of the reign of Asa.

Wakamchinjia Bwana siku ile, katika nyara walizozileta, dhabihu za ng'ombe mia saba, na kondoo elfu saba. 2 Mambo ya Nyakati 15:11

They sacrificed to Yahweh in that day, of the spoil which they had brought, seven hundred oxen and seven thousand sheep.

Wakafanya agano, ya kuwa watamtafuta Bwana, Mungu wa baba zao, kwa mioyo yao yote, na kwa roho zao zote; 2 Mambo ya Nyakati 15:12

They entered into the covenant to seek Yahweh, the God of their fathers, with all their heart and with all their soul;

na ya kwamba ye yote asiyemtafuta Bwana, Mungu wa Israeli, atauawa, akiwa mdogo au mkubwa, kwamba ni mwanamume au mwanamke. 2 Mambo ya Nyakati 15:13

and that whoever would not seek Yahweh, the God of Israel, should be put to death, whether small or great, whether man or woman.

Wakamwapia Bwana kwa sauti kuu, na kwa kelele, na kwa mapanda, na kwa baragumu. 2 Mambo ya Nyakati 15:14

They swore to Yahweh with a loud voice, and with shouting, and with trumpets, and with cornets.

Na Yuda wote wakakifurahia kile kiapo; kwani wameapa kwa moyo wao wote, na kumtafuta kwa mapenzi yao pia; naye ameonekana kwao; naye Bwana akawastarehesha pande zote. 2 Mambo ya Nyakati 15:15

All Judah rejoiced at the oath; for they had sworn with all their heart, and sought him with their whole desire; and he was found of them: and Yahweh gave them rest round about.

Hata na Maaka mamaye Asa, mfalme akamwondolea daraja yake asiwe malkia, kwa kuwa amefanya sanamu ya kuchukiza kwa Ashera; basi Asa akaikata sanamu yake, akaiponda, akaiteketeza penye kijito cha Kidroni. 2 Mambo ya Nyakati 15:16

Also Maacah, the mother of Asa the king, he removed from being queen, because she had made an abominable image for an Asherah; and Asa cut down her image, and made dust of it, and burnt it at the brook Kidron.

Lakini mahali pa juu hapakuondolewa katika Israeli; ila moyo wake Asa ulikuwa mkamilifu siku zake zote. 2 Mambo ya Nyakati 15:17

But the high places were not taken away out of Israel: nevertheless the heart of Asa was perfect all his days.

Akavileta nyumbani mwa Mungu vitu alivyovitakasa babaye, na vile alivyovitakasa mwenyewe, fedha, na dhahabu, na vyombo. 2 Mambo ya Nyakati 15:18

He brought into the house of God the things that his father had dedicated, and that he himself had dedicated, silver, and gold, and vessels.

Wala hapakuwa na vita tena hata mwaka wa thelathini na tano wa kutawala kwake Asa. 2 Mambo ya Nyakati 15:19

There was no more war to the five and thirtieth year of the reign of Asa.