2 Mambo ya Nyakati 23 Swahili & English

Listen/Download Audio
2 Mambo ya Nyakati 23 (Swahili) 2nd Chronicles 23 (English)

Hata mwaka wa saba Yehoyada akajitia nguvu, akawatwaa maakida wa mamia, Azaria mwana wa Yerohamu, na Ishmaeli mwana wa Yehohanani, na Azaria mwana wa Obedi, na Maaseya mwana wa Adaya, na Elishafati mwana wa Zikri, akapatana nao. 2 Mambo ya Nyakati 23:1

In the seventh year Jehoiada strengthened himself, and took the captains of hundreds, Azariah the son of Jeroham, and Ishmael the son of Jehohanan, and Azariah the son of Obed, and Maaseiah the son of Adaiah, and Elishaphat the son of Zichri, into covenant with him.

Wakazunguka katikati ya Yuda, wakawakusanya Walawi kutoka katika miji yote ya Yuda, na wakuu wa nyumba za mababa wa Israeli, wakaja Yerusalemu. 2 Mambo ya Nyakati 23:2

They went about in Judah, and gathered the Levites out of all the cities of Judah, and the heads of fathers' [houses] of Israel, and they came to Jerusalem.

Na kusanyiko lote wakafanya agano na mfalme nyumbani mwa Mungu. Akawaambia, Angalieni, mwana wa mfalme atatawala, kama Bwana alivyonena juu ya wana wa Daudi. 2 Mambo ya Nyakati 23:3

All the assembly made a covenant with the king in the house of God. He said to them, Behold, the king's son shall reign, as Yahweh has spoken concerning the sons of David.

Hili ndilo neno mtakalolifanya; theluthi yenu, ninyi mwingiao siku ya sabato, wa makuhani, na wa Walawi, mtalinda milangoni; 2 Mambo ya Nyakati 23:4

This is the thing that you shall do: a third part of you, who come in on the Sabbath, of the priests and of the Levites, shall be porters of the thresholds;

na theluthi nyumbani pa mfalme; na theluthi mlangoni pa msingi; na watu wote watakuwapo nyuani mwa nyumba ya Bwana. 2 Mambo ya Nyakati 23:5

and a third part shall be at the king's house; and a third part at the gate of the foundation: and all the people shall be in the courts of the house of Yahweh.

Wala asiingie mtu nyumbani mwa Bwana, ila makuhani, na hao watumikao wa Walawi; hao wataingia, kwa kuwa hao ni watakatifu; ila watu wote watalinda malinzi ya Bwana. 2 Mambo ya Nyakati 23:6

But let none come into the house of Yahweh, save the priests, and those who minister of the Levites; they shall come in, for they are holy: but all the people shall keep the charge of Yahweh.

Nao Walawi watamzunguka mfalme pande zote, kila mtu mwenye silaha zake mkononi; naye awaye yote aingiaye nyumbani na auawe; nanyi mfuatane na mfalme, aingiapo na atokapo. 2 Mambo ya Nyakati 23:7

The Levites shall compass the king round about, every man with his weapons in his hand; and whoever comes into the house, let him be slain: and be you with the king when he comes in, and when he goes out.

Basi Walawi na Yuda wote wakafanya sawasawa na yote aliyowaamuru Yehoyada kuhani; wakawatwaa kila mtu watu wake, hao watakaoingia siku ya sabato, na wale watakaotoka siku ya sabato; kwa maana Yehoyada kuhani hakuzifumua zamu. 2 Mambo ya Nyakati 23:8

So the Levites and all Judah did according to all that Jehoiada the priest commanded: and they took every man his men, those who were to come in on the Sabbath; with those who were to go out on the Sabbath; for Jehoiada the priest didn't dismiss the shift.

Naye Yehoyada kuhani akawapa maakida wa mamia mikuki, na ngao, na vigao, vilivyokuwa vya mfalme Daudi, vilivyokuwamo nyumbani mwa Mungu. 2 Mambo ya Nyakati 23:9

Jehoiada the priest delivered to the captains of hundreds the spears, and bucklers, and shields, that had been king David's, which were in the house of God.

Akawasimamisha watu wote, kila mtu mwenye silaha yake mkononi, toka pembe ya kuume ya nyumba mpaka pembe ya kushoto, upande wa madhabahu na nyumba, kumzunguka mfalme pande zote. 2 Mambo ya Nyakati 23:10

He set all the people, every man with his weapon in his hand, from the right side of the house to the left side of the house, along by the altar and the house, by the king round about.

Ndipo wakamleta nje mwana wa mfalme, wakamvika taji, na kumpa ule ushuhuda, wakamtawaza awe mfalme; Yehoyada na wanawe wakamtia mafuta, wakasema, Mfalme na aishi. 2 Mambo ya Nyakati 23:11

Then they brought out the king's son, and put the crown on him, and [gave him] the testimony, and made him king: and Jehoiada and his sons anointed him; and they said, [Long] live the king.

Na Athalia alipoisikia sauti ya watu, na ya walinzi, na ya hao waliomsifu mfalme, akaingia kwa watu nyumbani mwa Bwana; 2 Mambo ya Nyakati 23:12

When Athaliah heard the noise of the people running and praising the king, she came to the people into the house of Yahweh:

akatazama, na angalia, mfalme amesimama karibu na nguzo yake mlangoni, nao maakida na wenye mapanda karibu na mfalme; wakafurahi watu wote wa nchi, wakapiga mapanda; waimbaji pia wakipiga vinanda, wakaongoza nyimbo za kusifu. Ndipo Athalia akararua mavazi yake, akasema, Fitina! Fitina! 2 Mambo ya Nyakati 23:13

and she looked, and, behold, the king stood by his pillar at the entrance, and the captains and the trumpets by the king; and all the people of the land rejoiced, and blew trumpets; the singers also [played] on instruments of music, and led the singing of praise. Then Athaliah tore her clothes, and said, Treason! treason!

Yehoyada kuhani akawaleta nje maakida wa mamia, waliowekwa juu ya jeshi, akawaambia, Mtoeni nje kati ya safu; naye ye yote amfuataye, na auawe kwa upanga; kwani kuhani amesema, Msimwue katika nyumba ya Bwana. 2 Mambo ya Nyakati 23:14

Jehoiada the priest brought out the captains of hundreds who were set over the host, and said to them, Have her forth between the ranks; and whoever follows her, let him be slain with the sword: for the priest said, Don't kill her in the house of Yahweh.

Basi wakampisha njia; akaenda kwa kuingia pa mlango wa farasi nyumbani mwa mfalme; nao wakamwua huko. 2 Mambo ya Nyakati 23:15

So they made way for her; and she went to the entrance of the horse gate to the king's house: and they killed her there.

Kisha, Yehoyada akafanya agano, yeye na watu wote, na mfalme, kwamba watakuwa watu wa Bwana. 2 Mambo ya Nyakati 23:16

Jehoiada made a covenant between himself, and all the people, and the king, that they should be Yahweh's people.

Na watu wote wakaiendea nyumba ya Baali, wakaibomoa; wakavunja-vunja madhabahu zake na sanamu zake, wakamwua Matani kuhani wa Baali mbele ya madhabahu. 2 Mambo ya Nyakati 23:17

All the people went to the house of Baal, and broke it down, and broke his altars and his images in pieces, and killed Mattan the priest of Baal before the altars.

Yehoyada akauamuru usimamizi wa nyumba ya Bwana chini ya mkono wa makuhani Walawi, aliowagawa Daudi nyumbani mwa Bwana, ili wazisongeze sadaka za kuteketezwa za Bwana, kama ilivyoandikwa katika torati ya Musa, kwa kufurahi na kuimba, kama alivyoamuru Daudi. 2 Mambo ya Nyakati 23:18

Jehoiada appointed the officers of the house of Yahweh under the hand of the priests the Levites, whom David had distributed in the house of Yahweh, to offer the burnt offerings of Yahweh, as it is written in the law of Moses, with rejoicing and with singing, according to the order of David.

Akawasimamisha walinzi malangoni pa nyumba ya Bwana, asiingie aliye mchafu kwa vyo vyote. 2 Mambo ya Nyakati 23:19

He set the porters at the gates of the house of Yahweh, that no one who was unclean in anything should enter in.

Akawatwaa maakida wa mamia, na watu wakubwa, na hao watawalao watu, na watu wote wa nchi, akamtelemsha mfalme kutoka nyumba ya Bwana; wakalipitia lango la juu waende nyumbani kwa mfalme, wakamketisha mfalme katika kiti cha ufalme. 2 Mambo ya Nyakati 23:20

He took the captains of hundreds, and the nobles, and the governors of the people, and all the people of the land, and brought down the king from the house of Yahweh: and they came through the upper gate to the king's house, and set the king on the throne of the kingdom.

Basi wakafurahi watu wote wa nchi, na mji ukatulia; naye Athalia wakamwua kwa upanga.

2 Mambo ya Nyakati 23:21

So all the people of the land rejoiced, and the city was quiet. Athaliah they had slain with the sword.