2 Mambo ya Nyakati 24 Swahili & English

Listen/Download Audio
2 Mambo ya Nyakati 24 (Swahili) 2nd Chronicles 24 (English)

Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala; akatawala miaka arobaini huko Yerusalemu; na jina la mamaye aliitwa Sibia wa Beer-sheba. 2 Mambo ya Nyakati 24:1

Joash was seven years old when he began to reign; and he reigned forty years in Jerusalem: and his mother's name was Zibiah, of Beersheba.

Yoashi akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana siku zote za Yehoyada kuhani. 2 Mambo ya Nyakati 24:2

Joash did that which was right in the eyes of Yahweh all the days of Jehoiada the priest.

Yehoyada akamwoza wake wawili, naye akazaa wana na binti. 2 Mambo ya Nyakati 24:3

Jehoiada took for him two wives; and he became the father of sons and daughters.

Ikawa baada ya haya, Yoashi alikuwa na nia ya kuitengeneza nyumba ya Mungu. 2 Mambo ya Nyakati 24:4

It happened after this, that Joash was minded to restore the house of Yahweh.

Akawakusanya makuhani na Walawi, akawaambia, Nendeni mijini mwa Yuda, mkakusanye katika Israeli wote fedha, ili kuitengeneza nyumba ya Mungu wenu mwaka kwa mwaka, mkafanye bidii kuliharakisha neno hili. Walakini Walawi hawakuliharakisha. 2 Mambo ya Nyakati 24:5

He gathered together the priests and the Levites, and said to them, Go out to the cities of Judah, and gather of all Israel money to repair the house of your God from year to year; and see that you hasten the matter. However the Levites didn't hurry.

Mfalme akamwita Yehoyada mkuu wao, akamwambia, Mbona hukuwataka Walawi waitoze Yuda na Yerusalemu kodi ya Musa mtumishi wa Bwana, na ya kusanyiko la Israeli, kwa ajili ya hema ya ushuhuda? 2 Mambo ya Nyakati 24:6

The king called for Jehoiada the chief, and said to him, Why haven't you required of the Levites to bring in out of Judah and out of Jerusalem the tax of Moses the servant of Yahweh, and of the assembly of Israel, for the tent of the testimony?

Kwa kuwa wana wa Athalia, yule mwanamke mwovu, walikuwa wameibomoa nyumba ya Mungu; na vitakatifu vyote vya nyumba ya Bwana wamewapatia mabaali. 2 Mambo ya Nyakati 24:7

For the sons of Athaliah, that wicked woman, had broken up the house of God; and also all the dedicated things of the house of Yahweh did they bestow on the Baals.

Basi mfalme akaamuru, nao wakafanyiza kasha, wakaliweka nje langoni pa nyumba ya Bwana. 2 Mambo ya Nyakati 24:8

So the king commanded, and they made a chest, and set it outside at the gate of the house of Yahweh.

Wakapiga mbiu katika Yuda na Yerusalemu, kumletea Bwana kodi aliyoiweka Musa mtumishi wa Mungu, juu ya Israeli jangwani. 2 Mambo ya Nyakati 24:9

They made a proclamation through Judah and Jerusalem, to bring in for Yahweh the tax that Moses the servant of God laid on Israel in the wilderness.

Wakafurahi maakida wote na watu wote, wakaleta na kutia ndani ya kasha, hata wakaisha. 2 Mambo ya Nyakati 24:10

All the princes and all the people rejoiced, and brought in, and cast into the chest, until they had made an end.

Ikawa wakati walipoletewa kasha wasimamizi wa mfalme kwa mkono wa Walawi, nao wakaona ya kwamba kuna fedha nyingi, huja karani wa mfalme, na msimamizi wake kuhani mkuu, wakatoa yaliyomo kashani, kisha hulichukua kasha, na kulirudisha mahali pake. Ndivyo walivyofanya siku kwa siku, wakakusanya fedha tele. 2 Mambo ya Nyakati 24:11

It was so, that whenever the chest was brought to the king's officers by the hand of the Levites, and when they saw that there was much money, the king's scribe and the chief priest's officer came and emptied the chest, and took it, and carried it to its place again. Thus they did day by day, and gathered money in abundance.

Na mfalme na Yehoyada waliwapa hao waliofanya kazi ya utumishi wa nyumba ya Bwana; nao wakawaajiri waashi na maseremala ili kuitengeza nyumba ya Bwana, na hao pia wafuao chuma na shaba ili kuitengeza nyumba ya Bwana. 2 Mambo ya Nyakati 24:12

The king and Jehoiada gave it to such as did the work of the service of the house of Yahweh; and they hired masons and carpenters to restore the house of Yahweh, and also such as worked iron and brass to repair the house of Yahweh.

Hivyo mafundi wakafanya kazi yao, nao wakaimaliza, wakaisimamisha nyumba ya Mungu kama ilivyopasa, wakaifanya imara. 2 Mambo ya Nyakati 24:13

So the workmen worked, and the work of repairing went forward in their hands, and they set up the house of God in its state, and strengthened it.

Nao walipokwisha, wakaleta mbele ya mfalme na Yehoyada fedha iliyobaki, vikafanyizwa kwayo vyombo vya nyumba ya Bwana, vyombo vya utumishi, navyo vya kutolea, na miiko, na vyombo vya dhahabu na fedha. Wakatoa sadaka za kuteketezwa katika nyumba ya Bwana, daima, siku zote za Yehoyada. 2 Mambo ya Nyakati 24:14

When they had made an end, they brought the rest of the money before the king and Jehoiada, of which were made vessels for the house of Yahweh, even vessels with which to minister and to offer, and spoons, and vessels of gold and silver. They offered burnt offerings in the house of Yahweh continually all the days of Jehoiada.

Lakini Yehoyada akawa mzee, mwenye umri mwingi, akafa; alipokufa alikuwa na umri wa miaka mia na thelathini. 2 Mambo ya Nyakati 24:15

But Jehoiada grew old and was full of days, and he died; one hundred thirty years old was he when he died.

Wakamzika katika mji wa Daudi kati ya wafalme, kwa sababu ametenda mema katika Israeli, na kwa Mungu, na katika nyumba yake. 2 Mambo ya Nyakati 24:16

They buried him in the city of David among the kings, because he had done good in Israel, and toward God and his house.

Hata baada ya kufa kwake Yehoyada, wakuu wa Yuda wakamwendea mfalme, wakamsujudia. Naye mfalme akawasikiliza maneno yao. 2 Mambo ya Nyakati 24:17

Now after the death of Jehoiada came the princes of Judah, and made obeisance to the king. Then the king listened to them.

Wakaiacha nyumba ya Bwana, Mungu wa baba zao; wakatumikia maashera na sanamu; ghadhabu ikawajia Yuda na Yerusalemu kwa sababu ya hiyo hatia yao. 2 Mambo ya Nyakati 24:18

They forsook the house of Yahweh, the God of their fathers, and served the Asherim and the idols: and wrath came on Judah and Jerusalem for this their guiltiness.

Hata hivyo akawapelekea manabii, ili kuwarudisha kwa Bwana; nao wakawashuhudia; lakini hawakukubali kuwasikiliza. 2 Mambo ya Nyakati 24:19

Yet he sent prophets to them, to bring them again to Yahweh; and they testified against them: but they would not give ear.

Na roho ya Mungu ikamjia Zekaria, mwana wa Yehoyada, kuhani; naye akasimama juu ya watu, akawaambia, Mungu asema hivi, Kwani ninyi kuzihalifu amri za Bwana, hata msiweze kufanikiwa? Kwa kuwa mmemwacha Bwana, yeye naye amewaacha ninyi. 2 Mambo ya Nyakati 24:20

The Spirit of God came on Zechariah the son of Jehoiada the priest; and he stood above the people, and said to them, Thus says God, Why disobey you the commandments of Yahweh, so that you can't prosper? because you have forsaken Yahweh, he has also forsaken you.

Basi, wakafanya shauri juu yake, wakampiga kwa mawe kwa amri ya mfalme katika ua wa nyumba ya Bwana. 2 Mambo ya Nyakati 24:21

They conspired against him, and stoned him with stones at the commandment of the king in the court of the house of Yahweh.

Basi hivyo mfalme Yoashi hakuukumbuka wema, ambao Yehoyada, baba yake, alimfanyia, bali alimwua mwanawe. Naye alipokufa, alisema, Bwana na ayaangalie haya, akayatakie kisasi. 2 Mambo ya Nyakati 24:22

Thus Joash the king didn't remember the kindness which Jehoiada his father had done to him, but killed his son. When he died, he said, Yahweh look on it, and require it.

Ikawa mwisho wa mwaka, wakakwea juu yake jeshi la Washami; wakafika Yuda na Yerusalemu, wakawaangamiza wakuu wa watu wote miongoni mwa watu, wakamletea mfalme wa Dameski nyara zao zote. 2 Mambo ya Nyakati 24:23

It happened at the end of the year, that the army of the Syrians came up against him: and they came to Judah and Jerusalem, and destroyed all the princes of the people from among the people, and sent all the spoil of them to the king of Damascus.

Maana wakaja jeshi la Washami watu haba; Bwana akatia mikononi mwao jeshi kubwa mno, kwa sababu wamemwacha Bwana, Mungu wa baba zao. Hivyo wakamfanyia Yoashi hukumu. 2 Mambo ya Nyakati 24:24

For the army of the Syrians came with a small company of men; and Yahweh delivered a very great host into their hand, because they had forsaken Yahweh, the God of their fathers. So they executed judgment on Joash.

Hata walipoondoka kwake, (nao walimwacha ameshikwa sana na maradhi,) watumishi wake mwenyewe wakamfanyia fitina kwa ajili ya damu ya mwana wa Yehoyada kuhani, wakamwua kitandani pake, akafa; wakamzika mjini mwa Daudi, lakini hawakumzika katika makaburi ya wafalme. 2 Mambo ya Nyakati 24:25

When they were departed for him (for they left him very sick), his own servants conspired against him for the blood of the sons of Jehoiada the priest, and killed him on his bed, and he died; and they buried him in the city of David, but they didn't bury him in the tombs of the kings.

Na hawa ndio waliomfanyia fitina, Zabadi mwana wa Shimeathi mwanamke Mwamoni, na Yehozabadi mwana wa Shimrithi mwanamke Mmoabi. 2 Mambo ya Nyakati 24:26

These are those who conspired against him: Zabad the son of Shimeath the Ammonitess, and Jehozabad the son of Shimrith the Moabitess.

Basi kwa habari ya wanawe, na ukubwa wa mizigo aliolemewa, na majengo ya nyumba ya Mungu, tazama, hayo yameandikwa katika maelezo ya kitabu cha wafalme. Na Amazia mwanawe akatawala mahali pake.

2 Mambo ya Nyakati 24:27

Now concerning his sons, and the greatness of the burdens [laid] on him, and the rebuilding of the house of God, behold, they are written in the commentary of the book of the kings. Amaziah his son reigned in his place.