2 Mambo ya Nyakati 8 Swahili & English

Listen/Download Audio
2 Mambo ya Nyakati 8 (Swahili) 2nd Chronicles 8 (English)

Ikawa miaka ishirini ilipopita, ambayo katika hiyo Sulemani aliijenga nyumba ya Bwana, na nyumba yake mwenyewe; 2 Mambo ya Nyakati 8:1

It happened at the end of twenty years, in which Solomon had built the house of Yahweh, and his own house,

ndipo Sulemani akaijenga miji ile Hiramu aliyompa Sulemani, akawakalisha humo wana wa Israeli. 2 Mambo ya Nyakati 8:2

that the cities which Huram had given to Solomon, Solomon built them, and caused the children of Israel to dwell there.

Naye Sulemani akaenda Hamath-zoba, akaushinda. 2 Mambo ya Nyakati 8:3

Solomon went to Hamath-zobah, and prevailed against it.

Akaujenga Tadmori wa nyikani, na miji yote ya hazina, aliyoijenga katika Hamathi. 2 Mambo ya Nyakati 8:4

He built Tadmor in the wilderness, and all the store-cities, which he built in Hamath.

Tena akaujenga Beth-horoni wa juu, na Beth-horoni wa chini, miji yenye boma, yenye kuta, na malango, na makomeo; 2 Mambo ya Nyakati 8:5

Also he built Beth Horon the upper, and Beth Horon the lower, fortified cities, with walls, gates, and bars;

na Baalathi, na miji yote ya hazina Sulemani aliyokuwa nayo, na miji yote ya magari yake, na miji ya wapanda farasi wake, na ya anasa yote aliyopenda Sulemani kujenga humo Yerusalemu, na katika Lebanoni, na katika nchi yote ya mamlaka yake. 2 Mambo ya Nyakati 8:6

and Baalath, and all the store-cities that Solomon had, and all the cities for his chariots, and the cities for his horsemen, and all that Solomon desired to build for his pleasure in Jerusalem, and in Lebanon, and in all the land of his dominion.

Basi kwa habari ya watu wote waliosalia wa Wahiti, na wa Waamori, na wa Waperizi, na wa Wahivi, na wa Wayebusi, wasiokuwa wa Israeli; 2 Mambo ya Nyakati 8:7

As for all the people who were left of the Hittites, and the Amorites, and the Perizzites, and the Hivites, and the Jebusites, who were not of Israel;

wa watoto wao waliosalia baada yao katika nchi, ambao wana wa Israeli hawakuwakomesha, katika hao Sulemani akawatumikisha shokoa hata leo. 2 Mambo ya Nyakati 8:8

of their children who were left after them in the land, whom the children of Israel didn't consume, of them did Solomon raise a levy [of bondservants] to this day.

Wala katika wana wa Israeli Sulemani hakuwafanya watumwa kazini mwake; lakini hao walikuwa watu wa vita, na wakuu wa majemadari wake, na maakida wa magari yake na wa wapanda farasi wake. 2 Mambo ya Nyakati 8:9

But of the children of Israel did Solomon make no servants for his work; but they were men of war, and chief of his captains, and rulers of his chariots and of his horsemen.

Na hao walikuwa maakida wakuu wa Sulemani, watu mia mbili na hamsini, waliotawala juu ya watu. 2 Mambo ya Nyakati 8:10

These were the chief officers of king Solomon, even two hundred fifty, who ruled over the people.

Sulemani akamleta binti Farao kutoka mji wa Daudi mpaka nyumba aliyomjengea; kwa kuwa alisema, Mke wangu hatakaa nyumbani mwa Daudi mfalme wa Israeli, kwa kuwa ni patakatifu, mahali palipofika sanduku la Bwana. 2 Mambo ya Nyakati 8:11

Solomon brought up the daughter of Pharaoh out of the city of David to the house that he had built for her; for he said, My wife shall not dwell in the house of David king of Israel, because the places are holy, whereunto the ark of Yahweh has come.

Ndipo Sulemani akamtolea Bwana sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana, aliyoijenga mbele ya ukumbi, 2 Mambo ya Nyakati 8:12

Then Solomon offered burnt-offerings to Yahweh on the altar of Yahweh, which he had built before the porch,

kadiri ilivyohitajiwa huduma ya kila siku, akitoa sawasawa na amri ya Musa, siku za sabato, na za mwezi mpya, na za sikukuu zilizoamriwa, mara tatu kila mwaka, yaani, sikukuu ya mikate isiyochachwa, na sikukuu ya majuma, na sikukuu ya vibanda. 2 Mambo ya Nyakati 8:13

even as the duty of every day required, offering according to the commandment of Moses, on the Sabbaths, and on the new moons, and on the set feasts, three times in the year, [even] in the feast of unleavened bread, and in the feast of weeks, and in the feast of tents.

Akaziamuru, sawasawa na agizo la Daudi babaye, zamu za makuhani za kutumika, nao Walawi kwa kadiri ya malinzi yao, ili kusifu, na kuhudumu mbele ya makuhani, kama ilivyohitajiwa kila siku; tena mabawabu kwa zamu zao za kila mlango; maana ndivyo alivyoamuru Daudi mtu wa Mungu. 2 Mambo ya Nyakati 8:14

He appointed, according to the ordinance of David his father, the divisions of the priests to their service, and the Levites to their offices, to praise, and to minister before the priests, as the duty of every day required; the doorkeepers also by their divisions at every gate: for so had David the man of God commanded.

Wala hawakuyaacha maagizo ya mfalme aliyowaamuru makuhani na Walawi kwa neno lo lote, wala kwa habari ya hazina. 2 Mambo ya Nyakati 8:15

They didn't depart from the commandment of the king to the priests and Levites concerning any matter, or concerning the treasures.

Basi ikatengenezwa kazi yote ya Sulemani hata siku ya kutiwa msingi wa nyumba ya Bwana, na hata ilipokwisha. Hivyo ikamalizika nyumba ya Bwana. 2 Mambo ya Nyakati 8:16

Now all the work of Solomon was prepared to the day of the foundation of the house of Yahweh, and until it was finished. [So] the house of Yahweh was completed.

Ndipo Sulemani akaenda Esion-geberi, na Elothi, pwani ya nchi ya Edomu. 2 Mambo ya Nyakati 8:17

Then went Solomon to Ezion Geber, and to Eloth, on the seashore in the land of Edom.

Naye Hiramu akamletea merikebu kwa mikono ya watumishi wake, na watumishi waliokuwa wana-maji; nao wakafika Ofiri pamoja na watumishi wa Sulemani, wakachukua kutoka huko talanta mia nne na hamsini za dhahabu, wakamletea mfalme Sulemani. 2 Mambo ya Nyakati 8:18

Huram sent him by the hands of his servants ships, and servants who had knowledge of the sea; and they came with the servants of Solomon to Ophir, and fetched from there four hundred fifty talents of gold, and brought them to king Solomon.