2 Mambo ya Nyakati 13 Swahili & English

Listen/Download Audio
2 Mambo ya Nyakati 13 (Swahili) 2nd Chronicles 13 (English)

Katika mwaka wa kumi na nane wa mfalme Yeroboamu, akaanza Abiya kutawala juu ya Yuda. 2 Mambo ya Nyakati 13:1

In the eighteenth year of king Jeroboam began Abijah to reign over Judah.

Miaka mitatu akatawala huko Yerusalemu; na jina la mamaye aliitwa Maaka binti Urieli wa Gibea. Kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu. 2 Mambo ya Nyakati 13:2

Three years reigned he in Jerusalem: and his mother's name was Micaiah the daughter of Uriel of Gibeah. There was war between Abijah and Jeroboam.

Abiya akapanga vita mwenye jeshi la watu hodari wa vita, watu wateule mia nne elfu; naye Yeroboamu akapanga vita juu yake mwenye watu wateule mia nane elfu, waliokuwa waume mashujaa. 2 Mambo ya Nyakati 13:3

Abijah joined battle with an army of valiant men of war, even four hundred thousand chosen men: and Jeroboam set the battle in array against him with eight hundred thousand chosen men, who were mighty men of valor.

Basi Abiya akasimama juu ya kilima cha Semaraimu, kilichoko milimani mwa Efraimu, akasema, Nisikieni, enyi Yeroboamu na Israeli wote; 2 Mambo ya Nyakati 13:4

Abijah stood up on Mount Zemaraim, which is in the hill-country of Ephraim, and said, Hear me, Jeroboam and all Israel:

je! Haikuwapasa kujua ya kwamba Bwana, Mungu wa Israeli, alimpa Daudi ufalme juu ya Israeli milele, yeye na wanawe kwa agano la chumvi? 2 Mambo ya Nyakati 13:5

Ought you not to know that Yahweh, the God of Israel, gave the kingdom over Israel to David forever, even to him and to his sons by a covenant of salt?

Lakini Yeroboamu mwana wa Nebati, mtumwa wa Sulemani mwana wa Daudi, akainuka, akamfanyia fitina bwana wake. 2 Mambo ya Nyakati 13:6

Yet Jeroboam the son of Nebat, the servant of Solomon the son of David, rose up, and rebelled against his lord.

Wakamkusanyikia watu mabaradhuli, wasiofaa kitu, waliojitia nguvu juu ya Rehoboamu mwana wa Sulemani, Rehoboamu alipokuwa kijana na wa moyo mwororo, asiweze kuwazuia. 2 Mambo ya Nyakati 13:7

There were gathered to him worthless men, base fellows, who strengthened themselves against Rehoboam the son of Solomon, when Rehoboam was young and tender-hearted, and could not withstand them.

Hata sasa mwajidhania kuwa mtauzuia ufalme wa Bwana mikononi mwa wana wa Daudi; nanyi mmekuwa jamii kubwa, na kwenu mna ndama za dhahabu alizowafanyia Yeroboamu kuwa miungu. 2 Mambo ya Nyakati 13:8

Now you think to withstand the kingdom of Yahweh in the hand of the sons of David; and you are a great multitude, and there are with you the golden calves which Jeroboam made you for gods.

Je! Hamkuwafukuza makuhani wa Bwana, wana wa Haruni, na Walawi; mkajifanyia makuhani kama wafanyavyo watu wa nchi nyingine? Hata ye yote ajaye kujifanya wakfu na ndama, na kondoo waume saba, aweza kuwa kuhani wa hiyo isiyo miungu. 2 Mambo ya Nyakati 13:9

Haven't you driven out the priests of Yahweh, the sons of Aaron, and the Levites, and made you priests after the manner of the peoples of [other] lands? so that whoever comes to consecrate himself with a young bull and seven rams, the same may be a priest of [those who are] no gods.

Lakini sisi, Bwana ndiye Mungu wetu, wala sisi hatukumwacha; tena tunao makuhani wanaomtumikia Bwana, wana wa Haruni, na Walawi, kwa kazi yao; 2 Mambo ya Nyakati 13:10

But as for us, Yahweh is our God, and we have not forsaken him; and [we have] priests ministering to Yahweh, the sons of Aaron, and the Levites in their work:

nao humtolea Bwana kila asubuhi, na kila jioni, sadaka za kuteketezwa na fukizo la manukato; mikate ya wonyesho pia huiweka kwa taratibu yake juu ya meza takatifu, na kinara cha dhahabu chenye taa zake, kuwaka kila jioni; kwa maana sisi twayalinda malinzi ya Bwana, Mungu wetu; bali ninyi mmemwacha. 2 Mambo ya Nyakati 13:11

and they burn to Yahweh every morning and every evening burnt offerings and sweet incense: the show bread also [set they] in order on the pure table; and the lampstand of gold with the lamps of it, to burn every evening: for we keep the charge of Yahweh our God; but you have forsaken him.

Na tazama, Mungu yu pamoja nasi atutangulie, na makuhani wake wenye mapanda, ili wapige sauti ya kugutusha juu yenu. Enyi wana wa Israeli, msipigane na Bwana, Mungu wa baba zenu; kwani hamtafanikiwa. 2 Mambo ya Nyakati 13:12

Behold, God is with us at our head, and his priests with the trumpets of alarm to sound an alarm against you. Children of Israel, don't you fight against Yahweh, the God of your fathers; for you shall not prosper.

Lakini Yeroboamu aliwazungushia waviziao kwa nyuma; basi wao wakawa mbele ya Yuda, na wale waviziao nyuma yao. 2 Mambo ya Nyakati 13:13

But Jeroboam caused an ambush to come about behind them: so they were before Judah, and the ambush was behind them.

Na Yuda walipotazama nyuma, angalia, vita vikawa mbele na nyuma; wakamlilia Bwana, na makuhani wakapiga mapanda. 2 Mambo ya Nyakati 13:14

When Judah looked back, behold, the battle was before and behind them; and they cried to Yahweh, and the priests sounded with the trumpets.

Ndipo wakapiga kelele watu wa Yuda; ikawa, watu na Yuda walipopiga kelele, Mungu akampiga Yeroboamu na Israeli wote mbele ya Abiya na Yuda. 2 Mambo ya Nyakati 13:15

Then the men of Judah gave a shout: and as the men of Judah shouted, it happened, that God struck Jeroboam and all Israel before Abijah and Judah.

Wana wa Israeli wakakimbia mbele ya Yuda; naye Mungu akawaua mikononi mwao. 2 Mambo ya Nyakati 13:16

The children of Israel fled before Judah; and God delivered them into their hand.

Abiya na watu wake wakawapiga mapigo makuu; hata wakaanguka wameuawa wa Israeli mia tano elfu, watu wateule. 2 Mambo ya Nyakati 13:17

Abijah and his people killed them with a great slaughter: so there fell down slain of Israel five hundred thousand chosen men.

Ndivyo walivyotiishwa wana wa Israeli wakati ule, wakashinda wana wa Yuda, kwa kuwa walimtegemea Bwana, Mungu wa baba zao. 2 Mambo ya Nyakati 13:18

Thus the children of Israel were brought under at that time, and the children of Judah prevailed, because they relied on Yahweh, the God of their fathers.

Abiya akamfuata Yeroboamu, akamnyang'anya miji, Betheli na miji yake, na Yeshana na miji yake, na Efroni na miji yake. 2 Mambo ya Nyakati 13:19

Abijah pursued after Jeroboam, and took cities from him, Bethel with the towns of it, and Jeshanah with the towns of it, and Ephron with the towns of it.

Wala Yeroboamu hakupata nguvu tena siku za Abiya; kisha Bwana akampiga, akafa. 2 Mambo ya Nyakati 13:20

Neither did Jeroboam recover strength again in the days of Abijah: and Yahweh struck him, and he died.

Ila Abiya akapata nguvu, akaoa wake kumi na wanne, akazaa wana ishirini na wawili, na binti kumi na sita. 2 Mambo ya Nyakati 13:21

But Abijah grew mighty, and took to himself fourteen wives, and became the father of twenty-two sons, and sixteen daughters.

Na mambo ya Abiya yaliyosalia, na njia zake, na maneno yake, yameandikwa katika kitabu cha maelezo cha nabii Ido. 2 Mambo ya Nyakati 13:22

The rest of the acts of Abijah, and his ways, and his sayings, are written in the commentary of the prophet Iddo.