2 Mambo ya Nyakati 27 Swahili & English

Listen/Download Audio
2 Mambo ya Nyakati 27 (Swahili) 2nd Chronicles 27 (English)

Yothamu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala; akatawala katika Yerusalemu miaka kumi na sita; na jina la mamaye aliitwa Yerusha binti Sadoki. 2 Mambo ya Nyakati 27:1

Jotham was twenty-five years old when he began to reign; and he reigned sixteen years in Jerusalem: and his mother's name was Jerushah the daughter of Zadok.

Akafanya yaliyo ya adili machoni pa Bwana, sawasawa na yote aliyoyafanya Uzia babaye; isipokuwa hakuingia hekaluni mwa Bwana. Lakini watu walikuwa wakali kufanya maovu. 2 Mambo ya Nyakati 27:2

He did that which was right in the eyes of Yahweh, according to all that his father Uzziah had done: however he didn't enter into the temple of Yahweh. The people did yet corruptly.

Ndiye aliyelijenga lango la juu la nyumba ya Bwana, na juu ya ukuta wa Ofeli akajenga sana. 2 Mambo ya Nyakati 27:3

He built the upper gate of the house of Yahweh, and on the wall of Ophel he built much.

Tena akajenga miji katika milima ya Yuda, na mwituni akajenga ngome na minara. 2 Mambo ya Nyakati 27:4

Moreover he built cities in the hill-country of Judah, and in the forests he built castles and towers.

Kisha akapigana na mfalme wa wana wa Amoni, akawashinda. Na wana wa Amoni wakampa mwaka ule ule talanta mia za fedha, na kori elfu kumi za ngano, na elfu kumi za shayiri. Hayo ndiyo waliyomtolea wana wa Amoni, mwaka wa pili pia, na mwaka wa tatu. 2 Mambo ya Nyakati 27:5

He fought also with the king of the children of Ammon, and prevailed against them. The children of Ammon gave him the same year one hundred talents of silver, and ten thousand measures of wheat, and ten thousand of barley. So much did the children of Ammon render to him, in the second year also, and in the third.

Basi Yothamu akawa na nguvu, kwa kuwa alizitengeneza njia zake mbele za Bwana, Mungu wake. 2 Mambo ya Nyakati 27:6

So Jotham became mighty, because he ordered his ways before Yahweh his God.

Na mambo yote ya Yothamu yaliyosalia, na vita vyake vyote, na njia zake, tazama, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda. 2 Mambo ya Nyakati 27:7

Now the rest of the acts of Jotham, and all his wars, and his ways, behold, they are written in the book of the kings of Israel and Judah.

Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala; akatawala miaka kumi na sita huko Yerusalemu. 2 Mambo ya Nyakati 27:8

He was five and twenty years old when he began to reign, and reigned sixteen years in Jerusalem.

Yothamu akalala na babaze, wakamzika katika mji wa Daudi; na Ahazi mwanawe akatawala mahali pake. 2 Mambo ya Nyakati 27:9

Jotham slept with his fathers, and they buried him in the city of David: and Ahaz his son reigned in his place.