2 Mambo ya Nyakati 6 Swahili & English

Listen/Download Audio
2 Mambo ya Nyakati 6 (Swahili) 2nd Chronicles 6 (English)

Ndipo Sulemani akanena, Bwana alisema ya kwamba atakaa katika giza nene. 2 Mambo ya Nyakati 6:1

Then spoke Solomon, Yahweh has said that he would dwell in the thick darkness.

Lakini nimekujengea nyumba ya kukaa, iwe mahali pa makao yako milele. 2 Mambo ya Nyakati 6:2

But I have built you a house of habitation, and a place for you to dwell in forever.

Mfalme akageuza uso wake, akawabarikia mkutano wote wa Israeli; na mkutano wote wa Israeli wakasimama. 2 Mambo ya Nyakati 6:3

The king turned his face, and blessed all the assembly of Israel: and all the assembly of Israel stood.

Akasema, Bwana, Mungu wa Israeli, ahimidiwe, aliyenena kwa kinywa chake na baba yangu Daudi, akalitimiza kwa mikono yake, akasema, 2 Mambo ya Nyakati 6:4

He said, Blessed be Yahweh, the God of Israel, who spoke with his mouth to David my father, and has with his hands fulfilled it, saying,

Tangu siku ile nilipowatoa watu wangu katika nchi ya Misri, sikuchagua mji wo wote wa kabila zote za Israeli ili kujenga nyumba, jina langu liwe humo; wala sikumchagua mtu ye yote awe mkuu juu ya watu wangu Israeli; 2 Mambo ya Nyakati 6:5

Since the day that I brought forth my people out of the land of Egypt, I chose no city out of all the tribes of Israel to build a house in, that my name might be there; neither chose I any man to be prince over my people Israel:

lakini nimeuchagua Yerusalemu, jina langu liwe humo; na Daudi nimemchagua awe juu ya watu wangu Israeli. 2 Mambo ya Nyakati 6:6

but I have chosen Jerusalem, that my name might be there; and have chosen David to be over my people Israel.

Basi ilikuwa moyoni mwake Daudi, baba yangu, kujenga nyumba kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli. 2 Mambo ya Nyakati 6:7

Now it was in the heart of David my father to build a house for the name of Yahweh, the God of Israel.

Lakini Bwana akamwambia Daudi baba yangu, Kwa kuwa ilikuwa moyoni mwako kujenga nyumba kwa jina langu, ulifanya vema kuwaza hivi moyoni mwako; 2 Mambo ya Nyakati 6:8

But Yahweh said to David my father, Whereas it was in your heart to build a house for my name, you did well that it was in your heart:

lakini si wewe utakayeijenga nyumba hiyo; ila mwanao atakayetoka katika viuno vyako, yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa jina langu. 2 Mambo ya Nyakati 6:9

nevertheless you shall not build the house; but your son who shall come forth out of your loins, he shall build the house for my name.

Basi Bwana amelitimiza neno lile alilolinena; nami nimesimama mahali pa Daudi baba yangu, na kuketi katika kiti cha enzi cha Israeli, kama Bwana alivyoahidi, nami nimeijenga nyumba kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli. 2 Mambo ya Nyakati 6:10

Yahweh has performed his word that he spoke; for I am risen up in the room of David my father, and sit on the throne of Israel, as Yahweh promised, and have built the house for the name of Yahweh, the God of Israel.

Ndimo nilimoliweka hilo sanduku, ambalo ndani yake mna agano la Bwana, alilolifanya na wana wa Israeli. 2 Mambo ya Nyakati 6:11

There have I set the ark, in which is the covenant of Yahweh, which he made with the children of Israel.

Akasimama mbele ya madhabahu ya Bwana, machoni pa mkutano wote wa Israeli, akainyosha mikono; 2 Mambo ya Nyakati 6:12

He stood before the altar of Yahweh in the presence of all the assembly of Israel, and spread forth his hands

(maana Sulemani alikuwa amefanya mimbari ya shaba, urefu wake mikono mitano, na upana wake mikono mitano, na kwenda juu kwake mikono mitatu, na kuisimamisha katikati ya ua; akasimama juu yake, akapiga magoti mbele ya mkutano wote wa Israeli, akaikunjua mikono yake kuelekea mbinguni); 2 Mambo ya Nyakati 6:13

(for Solomon had made a brazen scaffold, five cubits long, and five cubits broad, and three cubits high, and had set it in the midst of the court; and on it he stood, and kneeled down on his knees before all the assembly of Israel, and spread forth his hands toward heaven;)

akasema, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe, mbinguni, wala duniani; ushikaye maagano na rehema kwa watumishi wako, waendao mbele zako kwa moyo wao wote; 2 Mambo ya Nyakati 6:14

and he said, Yahweh, the God of Israel, there is no God like you, in heaven, or on earth; who keep covenant and loving kindness with your servants, who walk before you with all their heart;

uliyemtimizia mtumishi wako Daudi, baba yangu, ahadi uliyomwahidi; naam, ulinena kwa kinywa chako, ukayatimiza kwa mkono wako, kama ilivyo leo. 2 Mambo ya Nyakati 6:15

who have kept with your servant David my father that which you did promise him: yes, you spoke with your mouth, and have fulfilled it with your hand, as it is this day.

Sasa, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, umfikilizie mtumishi wako Daudi, baba yangu, ahadi uliyomwahidia, ukisema, Hutakosa kuwa na mtu machoni pangu, wa kuketi katika kiti cha enzi cha Israeli; wakiwa tu watoto wako wataiangalia njia yao, ili kuiendea torati yangu, kama wewe ulivyokwenda mbele zangu. 2 Mambo ya Nyakati 6:16

Now therefore, Yahweh, the God of Israel, keep with your servant David my father that which you have promised him, saying, There shall not fail you a man in my sight to sit on the throne of Israel, if only your children take heed to their way, to walk in my law as you have walked before me.

Basi sasa, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, ulithibitishe neno lako, ulilomwambia mtumishi wako Daudi. 2 Mambo ya Nyakati 6:17

Now therefore, Yahweh, the God of Israel, let your word be verified, which you spoke to your servant David.

Lakini Mungu je! Yamkini atakaa na watu duniani? Tazama, mbingu na mbingu za mbingu za mbingu hazikutoshi; siuze nyumba hii niliyoijenga! 2 Mambo ya Nyakati 6:18

But will God in very deed dwell with men on the earth? behold, heaven and the heaven of heavens can't contain you; how much less this house which I have built!

Walakini umwangalie mtumwa wako anayoyaomba, na kusihi, Ee Bwana, Mungu wangu, usikie kilio na maombi anayoyaomba mtumwa wako mbele zako; 2 Mambo ya Nyakati 6:19

Yet have you respect to the prayer of your servant, and to his supplication, Yahweh my God, to listen to the cry and to the prayer which your servant prays before you;

ili macho yako yafumbuke kwa nyumba hii mchana na usiku, mahali uliponena, ndipo utakapoliweka jina lako; usikie maombi atakayoomba mtumwa wako, akikabili mahali hapa. 2 Mambo ya Nyakati 6:20

that your eyes may be open toward this house day and night, even toward the place where you have said that you would put your name there; to listen to the prayer which your servant shall pray toward this place.

Uyasikie atakayosihi mtumwa wako, na watu wako Israeli, watakapoomba wakikabili mahali hapa; naam, usikie toka makaoni mwako, toka mbinguni, nawe usikiapo, samehe. 2 Mambo ya Nyakati 6:21

Listen you to the petitions of your servant, and of your people Israel, when they shall pray toward this place: yes, hear from your dwelling-place, even from heaven; and when you hear, forgive.

Ikiwa mtu amemkosea mwenzake, akitiwa kiapo, aapishwe, naye akija na kuapa hapa mbele ya madhabahu yako nyumbani humu; 2 Mambo ya Nyakati 6:22

If a man sin against his neighbor, and an oath is laid on him to cause him to swear, and he comes and swears before your altar in this house;

basi, usikie mbinguni, ukatende, ukawahukumu watumwa wako; ukimlipiza mwovu, kumpatilizia njia yake kichwani; ukamfanyie haki mwenye haki, ukimjalia kwa kadiri ya haki yake. 2 Mambo ya Nyakati 6:23

then hear from heaven, and do, and judge your servants, requiting the wicked, to bring his way on his own head; and justifying the righteous, to give him according to his righteousness.

Ikiwa watu wako Israeli wamepigwa mbele ya adui zao, kwa sababu wamekukosa wewe; kama wakirejea kwako, na kulikiri jina lako, wakikuomba na kukusihi nyumbani humu; 2 Mambo ya Nyakati 6:24

If your people Israel be struck down before the enemy, because they have sinned against you, and shall turn again and confess your name, and pray and make supplication before you in this house;

basi usikie huko mbinguni, ukaisamehe dhambi ya watu wako Israeli, na kuwarejeza tena katika nchi uliyowapa wao na baba zao. 2 Mambo ya Nyakati 6:25

then hear from heaven, and forgive the sin of your people Israel, and bring them again to the land which you gave to them and to their fathers.

Ikiwa mbingu zimefungwa, hata hakuna mvua, kwa sababu wamekukosa wewe; kama wakiomba wakikabili mahali hapa, na kulikiri jina lako, na kuiacha dhambi yao, uwatesapo; 2 Mambo ya Nyakati 6:26

When the sky is shut up, and there is no rain, because they have sinned against you; if they pray toward this place, and confess your name, and turn from their sin, when you do afflict them:

basi usikie huko mbinguni, ukaisamehe dhambi ya watumwa wako, na ya watu wako Israeli; uwafundishapo njia njema iwapasayo waiendee; ukainyeshee mvua nchi yako, uliyowapa watu wako iwe urithi. 2 Mambo ya Nyakati 6:27

then hear in heaven, and forgive the sin of your servants, and of your people Israel, when you teach them the good way in which they should walk; and send rain on your land, which you have given to your people for an inheritance.

Ikiwa nchi imeingia njaa, au tauni, au ukosefu wa mvua, au ukungu, au nzige, au panzi; ikiwa adui wamewahusuru katika nchi ya miji yao, au ukiwapo msiba wo wote, au uele wo wote; 2 Mambo ya Nyakati 6:28

If there be in the land famine, if there be pestilence, if there be blasting or mildew, locust or caterpillar; if their enemies besiege them in the land of their cities; whatever plague or whatever sickness there be;

yo yote atakayoyaomba na kusihi mtu awaye yote, au watu wako Israeli wote pamoja, watakaojua kila mtu pigo lake mwenyewe, na msiba wake mwenyewe, akiinyoshea mikono nyumba hii; 2 Mambo ya Nyakati 6:29

whatever prayer and supplication be made by any man, or by all your people Israel, who shall know every man his own plague and his own sorrow, and shall spread forth his hands toward this house:

basi usikie huko mbinguni, ukaapo, ukasamehe, ukampatilize kila mtu kwa kadiri ya njia zake zote; wewe umjuaye moyo; (maana wewe peke yako ndiwe uijuaye mioyo ya wanadamu); 2 Mambo ya Nyakati 6:30

then hear from heaven, your dwelling-place and forgive, and render to every man according to all his ways, whose heart you know; (for you, even you only, know the hearts of the children of men;)

ili wakuche wewe, waziendee njia zako, siku zote watakazoishi katika nchi uliyowapa baba zetu. 2 Mambo ya Nyakati 6:31

that they may fear you, to walk in your ways, so long as they live in the land which you gave to our fathers.

Hata na mgeni naye, asiyekuwa mmoja wa watu wako Israeli, atakapokuja kutoka nchi iliyo mbali sana kwa ajili ya jina lako kuu, na mkono wako ulio hodari, na mkono wako ulionyoshwa; hao watakapokuja na kuomba wakiielekea nyumba hii; 2 Mambo ya Nyakati 6:32

Moreover concerning the foreigner, who is not of your people Israel, when he shall come from a far country for your great name's sake, and your mighty hand, and your outstretched arm; when they shall come and pray toward this house:

basi usikie huko mbinguni, toka makaoni mwako, ukatende yote atakayokuomba huyo mgeni; ili watu wote wa dunia wapate kulijua jina lako, na kukucha wewe, kama watu wako Israeli, tena wajue ya kuwa nyumba hii niliyoijenga imeitwa kwa jina lako. 2 Mambo ya Nyakati 6:33

then hear from heaven, even from your dwelling-place, and do according to all that the foreigner calls to you for; that all the peoples of the earth may know your name, and fear you, as does your people Israel, and that they may know that this house which I have built is called by your name.

Ikiwa watu wako wametoka kupigana na adui zao, utakakowatuma ko kote, wakikuomba kuuelekea mji huu uliouchagua, na nyumba hii niliyoijenga kwa jina lako; 2 Mambo ya Nyakati 6:34

If your people go out to battle against their enemies, by whatever way you shall send them, and they pray to you toward this city which you have chosen, and the house which I have built for your name;

basi uyasikie huko mbinguni wayaombayo, na kusihi, ukaitetee haki yao. 2 Mambo ya Nyakati 6:35

then hear from heaven their prayer and their supplication, and maintain their cause.

Wakikukosa, (maana hakuna mtu asiyekosa), hata uwakasirikie, na kuwatia mikononi mwa adui zao, wawahamishe, na kuwachukua mateka mpaka nchi iliyo mbali au iliyo karibu; 2 Mambo ya Nyakati 6:36

If they sin against you (for there is no man who doesn't sin), and you are angry with them, and deliver them to the enemy, so that they carry them away captive to a land far off or near;

basi wakikumbuka katika nchi walikohamishwa, na kutubu, na kukusihi katika nchi ya uhamisho wao, wakisema, Tumekosa, tumetenda kwa ukaidi, tumefanya maovu; 2 Mambo ya Nyakati 6:37

yet if they shall repent themselves in the land where they are carried captive, and turn again, and make supplication to you in the land of their captivity, saying, We have sinned, we have done perversely, and have dealt wickedly;

wakurudiapo kwa mioyo yao yote, na kwa nia zao zote, katika nchi ya uhamisho wao, adui walikowahamisha, wakiomba na kuielekea nchi uliyowapa baba zao, na mji huu uliouchagua, na nyumba hii niliyoijenga kwa jina lako; 2 Mambo ya Nyakati 6:38

if they return to you with all their heart and with all their soul in the land of their captivity, where they have carried them captive, and pray toward their land, which you gave to their fathers, and the city which you have chosen, and toward the house which I have built for your name:

basi uyasikie toka mbinguni, toka makaoni mwako, wayaombayo, na kusihi, ukaitetee haki yao; ukawasamehe watu wako, waliokosa juu yako. 2 Mambo ya Nyakati 6:39

then hear from heaven, even from your dwelling-place, their prayer and their petitions, and maintain their cause, and forgive your people who have sinned against you.

Na sasa, Ee Mungu wangu, macho yako yafumbuke, nakusihi, masikio yako yakasikilize maombi yaombwayo mahali hapa. 2 Mambo ya Nyakati 6:40

Now, my God, let, I beg you, your eyes be open, and let your ears be attentive, to the prayer that is made in this place.

Sasa, Ee Bwana, Mungu, uondoke, uende kwenye raha yako, wewe na sanduku la nguvu zako; makuhani wako, Ee Bwana, Mungu, wavikwe wokovu, watakatifu wako na washangilie mema. 2 Mambo ya Nyakati 6:41

Now therefore arise, Yahweh God, into your resting-place, you, and the ark of your strength: let your priests, Yahweh God, be clothed with salvation, and let your saints rejoice in goodness.

Ee Bwana, Mungu, usiurudishe nyuma uso wa masihi wako,uzikumbuke fadhili za Daudi mtumishi wako. 2 Mambo ya Nyakati 6:42

Yahweh God, don't turn away the face of your anointed: remember [your] loving kindnesses to David your servant.