Mithali 29 Swahili & English
Listen/Download AudioMithali 29 (Swahili) | Proverbs 29 (English) |
---|---|
Aonywaye mara nyingi akishupaza shingo, Atavunjika ghafula, wala hapati dawa. Mithali 29:1 |
He who is often rebuked and stiffens his neck Will be destroyed suddenly, with no remedy. |
Wenye haki wakiwa na amri, watu hufurahi; Bali mwovu atawalapo, watu huugua. Mithali 29:2 |
When the righteous thrive, the people rejoice; But when the wicked rule, the people groan. |
Apendaye hekima humfurahisha babaye; Bali ashikamanaye na makahaba hutapanya mali. Mithali 29:3 |
Whoever loves wisdom brings joy to his father; But a companion of prostitutes squanders his wealth. |
Mfalme huithibitisha nchi kwa hukumu; Bali yeye apokeaye rushwa huipindua. Mithali 29:4 |
The king by justice makes the land stable, But he who takes bribes tears it down. |
Mwenye kujipendekeza kwa jirani yake, Hutandika wavu ili kuitega miguu yake. Mithali 29:5 |
A man who flatters his neighbor, Spreads a net for his feet. |
Kuna mtego katika kosa la mtu mbaya; Bali mwenye haki huimba na kufurahi. Mithali 29:6 |
An evil man is snared by his sin, But the righteous can sing and be glad. |
Mwenye haki huyaangalia madai ya maskini; Bali mtu mbaya hana ufahamu hata ayajue. Mithali 29:7 |
The righteous care about justice for the poor. The wicked aren't concerned about knowledge. |
Watu wenye dharau huwasha mji moto; Bali wenye hekima hugeuzia mbali ghadhabu. Mithali 29:8 |
Mockers stir up a city, But wise men turn away anger. |
Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu; Akikasirika au akicheka, pia hapana raha. Mithali 29:9 |
If a wise man goes to court with a foolish man, The fool rages or scoffs, and there is no peace. |
Wamwagao damu humchukia mtu mkamilifu; Bali wenye haki humtunza nafsi yake. Mithali 29:10 |
The bloodthirsty hate a man of integrity; And they seek the life of the upright. |
Mpumbavu hudhihirisha hasira yake yote; Bali mwenye hekima huizuia na kuituliza. Mithali 29:11 |
A fool vents all of his anger, But a wise man brings himself under control. |
Mwenye kutawala akisikiliza uongo; Basi watumishi wake wote watakuwa waovu. Mithali 29:12 |
If a ruler listens to lies, All of his officials are wicked. |
Maskini na mdhalimu hukutana pamoja; Bwana huwatia nuru macho yao wote wawili. Mithali 29:13 |
The poor man and the oppressor have this in common: Yahweh gives sight to the eyes of both. |
Mfalme awahukumuye maskini kwa uaminifu; Kiti chake cha enzi kitathibitika milele. Mithali 29:14 |
The king who fairly judges the poor, His throne shall be established forever. |
Fimbo na maonyo hutia hekima; Bali mwana aliyeachiliwa humwaibisha mamaye. Mithali 29:15 |
The rod of correction gives wisdom, But a child left to himself causes shame to his mother. |
Waovu wakiongezeka, maasi huongezeka; Bali wenye haki watayatazama maanguko yao. Mithali 29:16 |
When the wicked increase, sin increases; But the righteous will see their downfall. |
Mrudi mwanao naye atakustarehesha; Naam, atakufurahisha nafsi yako. Mithali 29:17 |
Correct your son, and he will give you peace; Yes, he will bring delight to your soul. |
Pasipo maono, watu huacha kujizuia; Bali ana heri mtu yule aishikaye sheria. Mithali 29:18 |
Where there is no revelation, the people cast off restraint; But one who keeps the law is blessed. |
Haitoshi mtumwa kuonywa kwa maneno; Maana ajapoyafahamu hataitika. Mithali 29:19 |
A servant can't be corrected by words. Though he understands, yet he will not respond. |
Je! Umemwona mtu mwenye kuhamaki katika maneno? Afadhali kumtumaini mpumbavu kuliko yeye. Mithali 29:20 |
Do you see a man who is hasty in his words? There is more hope for a fool than for him. |
Amtunduiaye mtumwa wake tangu utoto, Mwisho wake atakuwa ni mwanawe. Mithali 29:21 |
He who pampers his servant from youth Will have him become a son in the end. |
Mtu wa hasira huchochea ugomvi; Na mtu mwenye ghadhabu huasi sana. Mithali 29:22 |
An angry man stirs up strife, And a wrathful man abounds in sin. |
Kiburi cha mtu kitamshusha; Bali mwenye roho ya unyenyekevu ataheshimiwa. Mithali 29:23 |
A man's pride brings him low, But one of lowly spirit gains honor. |
Mshiriki wa mwivi huichukia nafsi yake mwenyewe; Asikia maapizo, wala hana neno. Mithali 29:24 |
Whoever is an accomplice of a thief is an enemy of his own soul. He takes an oath, but dares not testify. |
Kuwaogopa wanadamu huleta mtego; Bali amtumainiye Bwana atakuwa salama. Mithali 29:25 |
The fear of man proves to be a snare, But whoever puts his trust in Yahweh is kept safe. |
Watu wengi hutafuta upendeleo wa mkuu; Bali hukumu ya kila mtu hutoka kwa Bwana Mithali 29:26 |
Many seek the ruler's favor, But a man's justice comes from Yahweh. |
Mtu aliye dhalimu ni chukizo kwa wenye haki; Na mnyofu wa mwenendo ni chukizo kwa waovu. Mithali 29:27 |
A dishonest man detests the righteous, And the upright in their ways detest the wicked. |