Afadhali maskini aendaye katika unyofu wake, Kuliko mpotofu wa midomo aliye mpumbavu.
Better is the poor who walks in his integrity Than he who is perverse in his lips and is a fool.
Tena si vizuri nafsi ya mtu ikose maarifa; Naye afanyaye haraka kwa miguu hutenda dhambi.
It isn't good to have zeal without knowledge; Nor being hasty with one's feet and missing the way.
Upumbavu wa mtu hupotosha njia yake; Na moyo wake hununa juu ya Bwana.
The foolishness of man subverts his way; His heart rages against Yahweh.
Utajiri huongeza rafiki wengi; Bali maskini hutengwa na rafiki yake.
Wealth adds many friends, But the poor is separated from his friend.
Shahidi wa uongo hakosi ataadhibiwa; Wala asemaye uongo hataokoka.
A false witness shall not be unpunished. He who pours out lies shall not go free.
Watu wengi watamsihi mkuu ili awafadhili; Na kila mtu ni rafiki yake atoaye tunu.
Many will entreat the favor of a ruler, And everyone is a friend to a man who gives gifts.
Ndugu zote wa maskini humchukia; Jinsi gani rafiki zake huzidi kujitenga naye! Huwafuata kwa maneno, lakini wametoweka.
All the relatives of the poor shun him: How much more do his friends avoid him! He pursues them with pleas, but they are gone.
Apataye hekima hujipenda nafsi yake; Ashikaye ufahamu atapata mema.
He who gets wisdom loves his own soul. He who keeps understanding shall find good.
Shahidi wa uongo hakosi ataadhibiwa; Naye asemaye uongo ataangamia.
A false witness shall not be unpunished. He who utters lies shall perish.
Maisha ya anasa hayampasi mpumbavu; Sembuse mtumwa awatawale wakuu.
Delicate living is not appropriate for a fool, Much less for a servant to have rule over princes.
Busara ya mtu huiahirisha hasira yake; Nayo ni fahari yake kusamehe makosa.
The discretion of a man makes him slow to anger. It is his glory to overlook an offense.
Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba; Bali hisani yake kama umande juu ya majani.
The king's wrath is like the roaring of a lion, But his favor is like dew on the grass.
Mwana mpumbavu ni msiba kwa babaye; Na ugomvi wa mke kama kutona-tona daima.
A foolish son is the calamity of his father. A wife's quarrels are a continual dripping.
Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa babaye; Bali mke mwenye busara, mtu hupewa na Bwana.
House and riches are an inheritance from fathers, But a prudent wife is from Yahweh.
Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito; Na nafsi yake mvivu itaona njaa.
Slothfulness casts into a deep sleep. The idle soul shall suffer hunger.
Yeye aihifadhiye amri huihifadhi nafsi yake; Bali yeye asiyeziangalia njia zake atakufa.
He who keeps the commandment keeps his soul, But he who is contemptuous in his ways shall die.
Amhurumiaye maskini humkopesha Bwana; Naye atamlipa kwa tendo lake jema.
He who has pity on the poor lends to Yahweh; He will reward him.
Mrudi mwanao, kwa maana liko tumaini; Wala usiikaze nafsi yako kwa kuangamia kwake.
Discipline your son, for there is hope; Don't be a willing party to his death.
Mtu wa hasira nyingi atachukua adhabu yake, Maana ujapomwokoa huna budi kufanya tena.
A hot-tempered man must pay the penalty, For if you rescue him, you must do it again.
Sikiliza mashauri, ukapokee mafundisho, Upate kuwa na hekima siku zako za mwisho.
Listen to counsel and receive instruction, That you may be wise in your latter end.
Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama.
There are many plans in a man's heart, But Yahweh's counsel will prevail.
Haja ya mwanadamu ni hisani yake; Ni afadhali maskini kuliko mwongo.
That which makes a man to be desired is his kindness. A poor man is better than a liar.
Kumcha Bwana huelekea uhai; Atakaa ameshiba; hatajiliwa na ubaya.
The fear of Yahweh leads to life, then contentment; He rests and will not be touched by trouble.
Mtu mvivu hutia mkono wake sahanini; Ila hataki hata kuupeleka kinywani pake.
The sluggard buries his hand in the dish; He will not so much as bring it to his mouth again.
Mpige mwenye mzaha, na mjinga atapata busara; Mwonye mwenye ufahamu, naye atatambua maarifa.
Flog a scoffer, and the simple will learn prudence; Rebuke one who has understanding, and he will gain knowledge.
Apotezaye mali za babaye na kumfukuza mamaye, Ni mwana aaibishaye, na kuleta lawama.
He who robs his father and drives away his mother, Is a son who causes shame and brings reproach.
Mwanangu, acha kusikia mafundisho, Ukitaka tu kuyaasi maneno ya maarifa.
If you stop listening to instruction, my son, You will stray from the words of knowledge.
Shahidi asiyefaa kitu hudhihaki hukumu, Na vinywa vya wasio haki humeza uovu.
A corrupt witness mocks justice, And the mouth of the wicked gulps down iniquity.
Hukumu zimewekwa tayari kwa wenye mzaha; Na mapigo kwa mgongo wa wapumbavu.
Penalties are prepared for scoffers, And beatings for the backs of fools.