Mithali 18 Swahili & English
Listen/Download AudioMithali 18 (Swahili) | Proverbs 18 (English) |
---|---|
Ajitengaye na wenzake hutafuta matakwa yake mwenyewe; Hushindana na kila shauri jema. Mithali 18:1 |
An unfriendly man pursues selfishness, And defies all sound judgment. |
Mpumbavu hapendezwi na ufahamu; Ila moyo wake udhihirike tu. Mithali 18:2 |
A fool has no delight in understanding, But only in revealing his own opinion. |
Ajapo asiye haki, huja dharau pia; Na pamoja na aibu huja lawama. Mithali 18:3 |
When wickedness comes, contempt also comes, And with shame comes disgrace. |
Maneno ya kinywa cha mtu ni kama maji ya vilindi; Kijito kibubujikacho; chemchemi ya hekima. Mithali 18:4 |
The words of a man's mouth are like deep waters. The fountain of wisdom is like a flowing brook. |
Kukubali uso wake asiye haki si vizuri; Wala kumpotosha mwenye haki hukumuni. Mithali 18:5 |
To be partial to the faces of the wicked is not good, Nor to deprive the innocent of justice. |
Midomo ya mpumbavu huingia katika fitina, Na kinywa chake huita mapigo. Mithali 18:6 |
A fool's lips come into strife, And his mouth invites beatings. |
Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake, Na midomo yake ni mtego wa nafsi yake. Mithali 18:7 |
A fool's mouth is his destruction, And his lips are a snare to his soul. |
Maneno ya mchongezi ni kama vitoweo; Nayo hushukia pande za ndani za tumbo. Mithali 18:8 |
The words of a gossip are like dainty morsels: They go down into a person's innermost parts. |
Yeye naye aliye mvivu katika kazi yake, Ni ndugu yake aliye mharabu. Mithali 18:9 |
One who is slack in his work Is brother to him who is a master of destruction. |
Jina la Bwana ni ngome imara; Mwenye haki huikimbilia, akawa salama. Mithali 18:10 |
The name of Yahweh is a strong tower: The righteous run to him, and are safe. |
Mali ya mtu tajiri ni mji wake wa nguvu; Ni kama ukuta mrefu katika mawazo yake. Mithali 18:11 |
The rich man's wealth is his strong city, Like an unscalable wall in his own imagination. |
Kabla ya uharibifu moyo wa mwanadamu hujivuna; Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu. Mithali 18:12 |
Before destruction the heart of man is proud, But before honor is humility. |
Yeye ajibuye kabla hajasikia, Ni upumbavu na aibu kwake. Mithali 18:13 |
He who gives answer before he hears, That is folly and shame to him. |
Roho ya mtu itastahimili udhaifu wake; Bali roho iliyovunjika nani awezaye kuistahimili? Mithali 18:14 |
A man's spirit will sustain him in sickness, But a crushed spirit, who can bear? |
Moyo wa mwenye busara hupata maarifa; Na sikio la mwenye hekima hutafuta maarifa. Mithali 18:15 |
The heart of the discerning gets knowledge. The ear of the wise seeks knowledge. |
Zawadi ya mtu humpatia nafasi; Humleta mbele ya watu wakuu. Mithali 18:16 |
A man's gift makes room for him, And brings him before great men. |
Ajiteteaye kwanza huonekana kuwa ana haki; Lakini jirani yake huja na kumchunguza. Mithali 18:17 |
He who pleads his cause first seems right; Until another comes and questions him. |
Kura hukomesha mashindano; Hukata maneno ya wakuu. Mithali 18:18 |
The lot settles disputes, And keeps strong ones apart. |
Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kuliko mji wa nguvu; Na mashindano ni kama mapingo ya ngome. Mithali 18:19 |
A brother offended is more difficult than a fortified city; And disputes are like the bars of a castle. |
Tumbo la mtu litajazwa matunda ya kinywa chake; Atashiba mazao ya midomo yake. Mithali 18:20 |
A man's stomach is filled with the fruit of his mouth. With the harvest of his lips he is satisfied. |
Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake. Mithali 18:21 |
Death and life are in the power of the tongue; Those who love it will eat its fruit. |
Apataye mke apata kitu chema; Naye ajipatia kibali kwa Bwana. Mithali 18:22 |
Whoever finds a wife finds a good thing, And obtains favor of Yahweh. |
Maskini hutumia maombi; Bali tajiri hujibu kwa ukali. Mithali 18:23 |
The poor plead for mercy, But the rich answer harshly. |
Ajifanyiaye rafiki wengi ni kwa uangamivu wake mwenyewe; Lakini yuko rafiki aambatanaye na mtu kuliko ndugu. Mithali 18:24 |
A man of many companions may be ruined, But there is a friend who sticks closer than a brother. |