Mithali 18 Swahili & English

Listen/Download Audio
Mithali 18 (Swahili) Proverbs 18 (English)

Ajitengaye na wenzake hutafuta matakwa yake mwenyewe; Hushindana na kila shauri jema. Mithali 18:1

An unfriendly man pursues selfishness, And defies all sound judgment.

Mpumbavu hapendezwi na ufahamu; Ila moyo wake udhihirike tu. Mithali 18:2

A fool has no delight in understanding, But only in revealing his own opinion.

Ajapo asiye haki, huja dharau pia; Na pamoja na aibu huja lawama. Mithali 18:3

When wickedness comes, contempt also comes, And with shame comes disgrace.

Maneno ya kinywa cha mtu ni kama maji ya vilindi; Kijito kibubujikacho; chemchemi ya hekima. Mithali 18:4

The words of a man's mouth are like deep waters. The fountain of wisdom is like a flowing brook.

Kukubali uso wake asiye haki si vizuri; Wala kumpotosha mwenye haki hukumuni. Mithali 18:5

To be partial to the faces of the wicked is not good, Nor to deprive the innocent of justice.

Midomo ya mpumbavu huingia katika fitina, Na kinywa chake huita mapigo. Mithali 18:6

A fool's lips come into strife, And his mouth invites beatings.

Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake, Na midomo yake ni mtego wa nafsi yake. Mithali 18:7

A fool's mouth is his destruction, And his lips are a snare to his soul.

Maneno ya mchongezi ni kama vitoweo; Nayo hushukia pande za ndani za tumbo. Mithali 18:8

The words of a gossip are like dainty morsels: They go down into a person's innermost parts.

Yeye naye aliye mvivu katika kazi yake, Ni ndugu yake aliye mharabu. Mithali 18:9

One who is slack in his work Is brother to him who is a master of destruction.

Jina la Bwana ni ngome imara; Mwenye haki huikimbilia, akawa salama. Mithali 18:10

The name of Yahweh is a strong tower: The righteous run to him, and are safe.

Mali ya mtu tajiri ni mji wake wa nguvu; Ni kama ukuta mrefu katika mawazo yake. Mithali 18:11

The rich man's wealth is his strong city, Like an unscalable wall in his own imagination.

Kabla ya uharibifu moyo wa mwanadamu hujivuna; Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu. Mithali 18:12

Before destruction the heart of man is proud, But before honor is humility.

Yeye ajibuye kabla hajasikia, Ni upumbavu na aibu kwake. Mithali 18:13

He who gives answer before he hears, That is folly and shame to him.

Roho ya mtu itastahimili udhaifu wake; Bali roho iliyovunjika nani awezaye kuistahimili? Mithali 18:14

A man's spirit will sustain him in sickness, But a crushed spirit, who can bear?

Moyo wa mwenye busara hupata maarifa; Na sikio la mwenye hekima hutafuta maarifa. Mithali 18:15

The heart of the discerning gets knowledge. The ear of the wise seeks knowledge.

Zawadi ya mtu humpatia nafasi; Humleta mbele ya watu wakuu. Mithali 18:16

A man's gift makes room for him, And brings him before great men.

Ajiteteaye kwanza huonekana kuwa ana haki; Lakini jirani yake huja na kumchunguza. Mithali 18:17

He who pleads his cause first seems right; Until another comes and questions him.

Kura hukomesha mashindano; Hukata maneno ya wakuu. Mithali 18:18

The lot settles disputes, And keeps strong ones apart.

Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kuliko mji wa nguvu; Na mashindano ni kama mapingo ya ngome. Mithali 18:19

A brother offended is more difficult than a fortified city; And disputes are like the bars of a castle.

Tumbo la mtu litajazwa matunda ya kinywa chake; Atashiba mazao ya midomo yake. Mithali 18:20

A man's stomach is filled with the fruit of his mouth. With the harvest of his lips he is satisfied.

Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake. Mithali 18:21

Death and life are in the power of the tongue; Those who love it will eat its fruit.

Apataye mke apata kitu chema; Naye ajipatia kibali kwa Bwana. Mithali 18:22

Whoever finds a wife finds a good thing, And obtains favor of Yahweh.

Maskini hutumia maombi; Bali tajiri hujibu kwa ukali. Mithali 18:23

The poor plead for mercy, But the rich answer harshly.

Ajifanyiaye rafiki wengi ni kwa uangamivu wake mwenyewe; Lakini yuko rafiki aambatanaye na mtu kuliko ndugu. Mithali 18:24

A man of many companions may be ruined, But there is a friend who sticks closer than a brother.