Mithali BSB

Mithali 20

Proverbs Chapter 20

1
Mvinyo hudhihaki, kileo huleta ugomvi; Na akosaye kwa vitu hivyo hana hekima.
Wine is a mocker, strong drink is a brawler, and whoever is led astray by them is not wise.
2
Utisho wa mfalme ni kama ngurumo ya simba; Amkasirishaye huitendea dhambi nafsi yake.
The terror of a king is like the roar of a lion; whoever provokes him forfeits his own life.
3
Mtu kujitenga na ugomvi ni heshima kwake; Bali kila mpumbavu ataka kugombana.
It is honorable for a man to resolve a dispute, but any fool will quarrel.
4
Mtu mvivu hataki kulima wakati wa baridi; Hivyo wakati wa mavuno ataomba, hana kitu.
The slacker does not plow in season; at harvest time he looks, but nothing is there.
5
Mashauri ya moyoni ni kama kilindi; Lakini mtu mwenye ufahamu atayateka.
The intentions of a man’s heart are deep waters, but a man of understanding draws them out.
6
Wanadamu hutangaza kila mtu hisani yake mwenyewe; Bali mtu aliye mwaminifu, ni nani awezaye kumpata?
Many a man proclaims his loving devotion, but who can find a trustworthy man?
7
Mwenye haki aendaye katika unyofu wake, Watoto wake wabarikiwa baada yake.
The righteous man walks with integrity; blessed are his children after him.
8
Mfalme aketiye katika kiti cha hukumu, Huyapepeta mabaya yote kwa macho yake.
A king who sits on a throne to judge sifts out all evil with his eyes.
9
Nani awezaye kusema, Nimesafisha moyo wangu; Nimetakasika dhambi yangu?
Who can say, “I have kept my heart pure; I am cleansed from my sin”?
10
Vipimo mbalimbali, na pishi mbalimbali, Vyote viwili ni chukizo kwa Bwana.
Differing weights and unequal measures—both are detestable to the LORD.
11
Hata mtoto hujijulisha kwa matendo yake; Kwamba kazi yake ni safi, kwamba ni adili.
Even a young man is known by his actions—whether his conduct is pure and upright.
12
Sikio lisikialo, na jicho lionalo, Bwana ndiye aliyeyafanya yote mawili.
Ears that hear and eyes that see—the LORD has made them both.
13
Usipende usingizi usije ukawa maskini; Fumbua macho yako nawe utashiba chakula.
Do not love sleep, or you will grow poor; open your eyes, and you will have plenty of food.
14
Haifai kitu, haifai kitu, asema mnunuzi; Lakini akiisha kwenda zake hujisifu.
“Worthless, worthless!” says the buyer, but on the way out, he gloats.
15
Dhahabu iko, na marijani tele; Lakini midomo ya maarifa ni kito cha thamani.
There is an abundance of gold and rubies, but lips of knowledge are a rare treasure.
16
Twaa nguo yake amdhaminiye mgeni; Mtoze rehani aliye mdhamini wa wageni.
Take the garment of the one who posts security for a stranger; get collateral if it is for a foreigner.
17
Chakula cha uongo ni kitamu kwa mtu; Lakini halafu kinywa chake kitajaa changarawe.
Food gained by fraud is sweet to a man, but later his mouth is full of gravel.
18
Kila kusudi huthibitika kwa kushauriana; Na kwa shauri la akili fanya vita.
Set plans by consultation, and wage war under sound guidance.
19
Mwenye kitango akisingizia hufunua siri; Basi, usishirikiane naye afunuaye midomo yake sana.
He who reveals secrets is a constant gossip; avoid the one who babbles with his lips.
20
Amlaaniye babaye au mamaye, Taa yake itazimika katika giza kuu.
Whoever curses his father or mother, his lamp will be extinguished in deepest darkness.
21
Urithi uliopatikana mwanzo kwa haraka, Mwisho wake, lakini, hautabarikiwa.
An inheritance gained quickly will not be blessed in the end.
22
Usiseme, Mimi nitalipa mabaya; Mngojee Bwana, naye atakuokoa.
Do not say, “I will avenge this evil!” Wait on the LORD, and He will save you.
23
Vipimo mbalimbali ni chukizo kwa Bwana; Tena mizani ya hila si njema.
Unequal weights are detestable to the LORD, and dishonest scales are no good.
24
Mwenendo wa mtu watoka kwa Bwana; Basi, awezaje mtu kuelewa na njia yake?
A man’s steps are from the LORD, so how can anyone understand his own way?
25
Ni mtego, mtu aseme kwa haraka, Kitu hiki ni wakfu; Na baada ya kuweka nadhiri kuuliza-uliza habari.
It is a trap for a man to dedicate something rashly, only later to reconsider his vows.
26
Mfalme mwenye hekima huwapepeta wasio haki; Naye hulipitisha gurudumo la kupuria juu yao.
A wise king separates out the wicked and drives the threshing wheel over them.
27
Pumzi ya mwanadamu ni taa ya Bwana; Hupeleleza yote yaliyomo ndani yake.
The spirit of a man is the lamp of the LORD, searching out his inmost being.
28
Fadhili na uaminifu humhifadhi mfalme, Na kiti chake cha enzi huthibitishwa kwa fadhili.
Loving devotion and faithfulness preserve a king; by these he maintains his throne.
29
Fahari ya vijana ni nguvu zao, Na uzuri wa wazee ni kichwa chenye mvi.
The glory of young men is their strength, and gray hair is the splendor of the old.
30
Machubuko ya fimbo husafisha uovu, Na mapigo hufikilia ndani ya mtima.
Lashes and wounds scour evil, and beatings cleanse the inmost parts.

Chagua Sura