Mithali 15 Swahili & English

Listen/Download Audio
Mithali 15 (Swahili) Proverbs 15 (English)

Jawabu la upole hugeuza hasira; Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu. Mithali 15:1

A gentle answer turns away wrath, But a harsh word stirs up anger.

Ulimi wa mwenye hekima hutamka maarifa vizuri; Bali vinywa vya wapumbavu humwaga upumbavu. Mithali 15:2

The tongue of the wise commends knowledge, But the mouth of fools gush out folly.

Macho ya Bwana yako kila mahali; Yakimchunguza mbaya na mwema. Mithali 15:3

Yahweh's eyes are everywhere, Keeping watch on the evil and the good.

Ulimi safi ni mti wa uzima; Bali ukorofi wa ulimi huvunja moyo. Mithali 15:4

A gentle tongue is a tree of life, But deceit in it crushes the spirit.

Mpumbavu hudharau kurudiwa na babaye; Bali yeye aangaliaye maonyo hupata busara. Mithali 15:5

A fool despises his father's correction, But he who heeds reproof shows prudence.

Katika nyumba ya mwenye haki mna akiba nyingi; Bali mapato ya mtu mbaya huwa taabu tu. Mithali 15:6

In the house of the righteous is much treasure, But the income of the wicked brings trouble.

Midomo ya mwenye haki hueneza maarifa; Bali moyo wa mpumbavu haufanyi hivyo. Mithali 15:7

The lips of the wise spread knowledge; Not so with the heart of fools.

Sadaka ya mtu mbaya ni chukizo kwa Bwana; Bali maombi ya mtu mnyofu ni furaha yake. Mithali 15:8

The sacrifice made by the wicked is an abomination to Yahweh, But the prayer of the upright is his delight.

Njia ya mtu mbaya ni chukizo kwa Bwana; Bali humpenda mtu afuatiaye wema. Mithali 15:9

The way of the wicked is an abomination to Yahweh, But he loves him who follows after righteousness.

Adhabu kali ina yeye aiachaye njia; Naye achukiaye kukemewa atakufa. Mithali 15:10

There is stern discipline for one who forsakes the way: Whoever hates reproof shall die.

Kuzimu na Uharibifu vi wazi mbele za Bwana; Si zaidi basi, mioyo ya wanadamu? Mithali 15:11

Sheol and Abaddon are before Yahweh-- How much more then the hearts of the children of men!

Mwenye mzaha hapendi kukaripiwa; Wala yeye hawaendei wenye hekima. Mithali 15:12

A scoffer doesn't love to be reproved; He will not go to the wise.

Moyo wa furaha huchangamsha uso; Bali kwa huzuni ya moyo roho hupondeka. Mithali 15:13

A glad heart makes a cheerful face; But an aching heart breaks the spirit.

Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa; Bali kinywa cha wapumbavu hula upumbavu. Mithali 15:14

The heart of one who has understanding seeks knowledge, But the mouths of fools feed on folly.

Siku zote za mtu ateswaye ni mbaya; Bali ukunjufu wa moyo ni karamu ya daima. Mithali 15:15

All the days of the afflicted are wretched, But one who has a cheerful heart enjoys a continual feast.

Kuwa na mali chache pamoja na kumcha Bwana; Ni bora kuliko mali nyingi pamoja na taabu. Mithali 15:16

Better is little, with the fear of Yahweh, Than great treasure with trouble.

Chakula cha mboga penye mapendano; Ni bora kuliko ng'ombe aliyenona pamoja na kuchukiana. Mithali 15:17

Better is a dinner of herbs, where love is, Than a fattened calf with hatred.

Mtu wa hasira huchochea ugomvi; Bali asiye mwepesi wa hasira hutuliza mashindano. Mithali 15:18

A wrathful man stirs up contention, But one who is slow to anger appeases strife.

Njia ya mtu mvivu ni kama boma la miiba; Bali mapito yao wenye unyofu hufanyika njia kuu. Mithali 15:19

The way of the sluggard is like a thorn patch, But the path of the upright is a highway.

Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye; Bali mpumbavu humdharau mamaye. Mithali 15:20

A wise son makes a father glad, But a foolish man despises his mother.

Upumbavu ni furaha kwake aliyepungukiwa na akili; Bali mwenye ufahamu huunyosha mwenendo wake. Mithali 15:21

Folly is joy to one who is void of wisdom, But a man of understanding keeps his way straight.

Pasipo mashauri makusudi hubatilika; Bali kwa wingi wa washauri huthibithika. Mithali 15:22

Where there is no counsel, plans fail; But in a multitude of counselors they are established.

Mtu hulifurahia jibu la kinywa chake; Na neno linenwalo wakati wa kufaa ni jema kama nini! Mithali 15:23

Joy comes to a man with the reply of his mouth. How good is a word at the right time!

Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu; Ili atoke katika kuzimu chini. Mithali 15:24

The path of life leads upward for the wise, To keep him from going downward to Sheol.

Bwana ataing'oa nyumba ya mwenye kiburi; Bali atauthibitisha mpaka wa mjane. Mithali 15:25

Yahweh will uproot the house of the proud, But he will keep the widow's borders intact.

Mashauri mabaya ni chukizo kwa Bwana; Bali maneno yapendezayo ni safi. Mithali 15:26

Yahweh detests the thoughts of the wicked, But the thoughts of the pure are pleasing.

Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe; Bali achukiaye zawadi ataishi. Mithali 15:27

He who is greedy for gain troubles his own house, But he who hates bribes will live.

Moyo wa mwenye haki hufikiri jinsi atakavyojibu; Bali kinywa cha wasio haki humwaga mabaya. Mithali 15:28

The heart of the righteous weighs answers, But the mouth of the wicked gushes out evil.

Bwana yu mbali na wasio haki; Bali huisikia sala ya mwenye haki. Mithali 15:29

Yahweh is far from the wicked, But he hears the prayer of the righteous.

Mng'ao wa macho huufurahisha moyo; Habari njema huinenepesha mifupa. Mithali 15:30

The light of the eyes rejoices the heart. Good news gives health to the bones.

Sikio lisikilizalo lawama yenye uhai Litakaa kati yao wenye hekima. Mithali 15:31

The ear that listens to reproof lives, And will be at home among the wise.

Akataaye maonyo huidharau nafsi yake mwenyewe; Bali yeye asikilizaye lawama hujipatia ufahamu. Mithali 15:32

He who refuses correction despises his own soul, But he who listens to reproof gets understanding.

Kumcha Bwana ni maonyo ya hekima; Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu. Mithali 15:33

The fear of Yahweh teaches wisdom. Before honor is humility.