Isaya 61 Swahili & English
Listen/Download AudioIsaya 61 (Swahili) | Isaiah 61 (English) |
---|---|
Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu Bwana amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao. Isaya 61:1 |
The Spirit of the Lord Yahweh is on me; because Yahweh has anointed me to preach good news to the humble; he has sent me to bind up the broken-hearted, to proclaim liberty to the captives, and the opening [of the prison] to those who are bound; |
Kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa, na siku ya kisasi cha Mungu wetu; kuwafariji wote waliao; Isaya 61:2 |
to proclaim the year of Yahweh's favor, and the day of vengeance of our God; to comfort all who mourn; |
kuwaagizia hao waliao katika Sayuni, wapewe taji ya maua badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho nzito; wapate kuitwa miti ya haki, iliyopandwa na Bwana, ili atukuzwe. Isaya 61:3 |
to appoint to those who mourn in Zion, to give to them a garland for ashes, the oil of joy for mourning, the garment of praise for the spirit of heaviness; that they may be called trees of righteousness, the planting of Yahweh, that he may be glorified. |
Nao watajenga mahali pa kale palipoharibiwa, watapainua mahali palipokuwa ukiwa zamani, watatengeneza miji iliyoharibiwa, mahali palipoachwa kizazi baada ya kizazi. Isaya 61:4 |
They shall build the old wastes, they shall raise up the former desolations, and they shall repair the waste cities, the desolations of many generations. |
Na wageni watasimama na kulisha makundi yenu, na watu wa kabila nyingine watakuwa wakulima wenu, na watunzaji wa mizabibu yenu. Isaya 61:5 |
Strangers shall stand and feed your flocks, and foreigners shall be your plowmen and your vine-dressers. |
Bali ninyi mtaitwa makuhani wa Bwana; watu watawaiteni wahudumu wa Mungu wetu; mtakula utajiri wa mataifa, na kujisifia utukufu wao. Isaya 61:6 |
But you shall be named the priests of Yahweh; men shall call you the ministers of our God: you shall eat the wealth of the nations, and in their glory shall you boast yourselves. |
Badala ya aibu yenu mtapata maradufu, na badala ya fedheha wataifurahia sehemu yao; basi katika nchi yao watamiliki maradufu; furaha yao itakuwa ya milele. Isaya 61:7 |
Instead of your shame [you shall have] double; and instead of dishonor they shall rejoice in their portion: therefore in their land they shall possess double; everlasting joy shall be to them. |
Maana mimi, Bwana, naipenda hukumu ya haki, nauchukia wivi na uovu; nami nitawalipa malipo katika kweli, nitaagana nao agano la milele. Isaya 61:8 |
For I, Yahweh, love justice, I hate robbery with iniquity; and I will give them their recompense in truth, and I will make an everlasting covenant with them. |
Na kizazi chao kitajulikana katika mataifa, na uzao wao katika kabila za watu; wote wawaonao watakiri ya kuwa wao ni kizazi kilichobarikiwa na Bwana. Isaya 61:9 |
Their seed shall be known among the nations, and their offspring among the peoples; all who see them shall acknowledge them, that they are the seed which Yahweh has blessed. |
Nitafurahi sana katika Bwana, nafsi yangu itashangilia katika Mungu wangu; maana amenivika mavazi ya wokovu, amenifunika vazi la haki, kama bwana arusi ajipambavyo kwa kilemba cha maua, na kama bibi arusi ajipambavyo kwa vyombo vya dhahabu. Isaya 61:10 |
I will greatly rejoice in Yahweh, my soul shall be joyful in my God; for he has clothed me with the garments of salvation, he has covered me with the robe of righteousness, as a bridegroom decks himself with a garland, and as a bride adorns herself with her jewels. |
Maana kama nchi itoavyo machipuko yake, na kama bustani ioteshavyo vitu vilivyopandwa ndani yake; ndivyo Bwana MUNGU atakavyootesha haki na sifa mbele ya mataifa yote. Isaya 61:11 |
For as the earth brings forth its bud, and as the garden causes the things that are sown in it to spring forth; so the Lord Yahweh will cause righteousness and praise to spring forth before all the nations. |