Isaya 48 Swahili & English
Listen/Download AudioIsaya 48 (Swahili) | Isaiah 48 (English) |
---|---|
Sikieni haya, enyi watu wa nyumba ya Yakobo, mnaoitwa kwa jina la Israeli, mliotoka katika maji ya Yuda; mnaoapa kwa jina la Bwana, na kumtaja Mungu wa Israeli, lakini si kwa kweli, wala si kwa haki. Isaya 48:1 |
Hear you this, house of Jacob, who are called by the name of Israel, and are come forth out of the waters of Judah; who swear by the name of Yahweh, and make mention of the God of Israel, but not in truth, nor in righteousness |
Maana hujiita wenyeji wa mji mtakatifu, hujitegemeza juu ya Mungu wa Israeli; Bwana wa majeshi ni jina lake. Isaya 48:2 |
(for they call themselves of the holy city, and stay themselves on the God of Israel; Yahweh of Hosts is his name): |
Mimi nimehubiri mambo ya kale tangu zamani; naam, yalitoka katika kinywa changu, nikayadhihirisha; naliyatenda kwa ghafula, yakatokea. Isaya 48:3 |
I have declared the former things from of old; yes, they went forth out of my mouth, and I shown them: suddenly I did them, and they happened. |
Kwa sababu nalijua ya kuwa wewe u mkaidi, na shingo yako ni shingo ya chuma, na kipaji cha uso wako ni shaba; Isaya 48:4 |
Because I knew that you are obstinate, and your neck is an iron sinew, and your brow brass; |
basi nimekuonyesha tangu zamani; kabla hayajatukia nalikuonyesha; usije ukasema, Sanamu yangu imetenda haya; sanamu yangu ya kuchonga, na sanamu yangu ya kuyeyusha, imeyaamuru. Isaya 48:5 |
therefore I have declared it to you from of old; before it came to pass I shown it you; lest you should say, My idol has done them, and my engraved image, and my molten image, has commanded them. |
Umesikia haya; tazama haya yote; nanyi, je! Hamtayahubiri? Nimekuonyesha mambo mapya tangu wakati huu, naam, mambo yaliyofichwa, usiyoyajua. Isaya 48:6 |
You have heard it; see all this; and you, will you not declare it? I have shown you new things from this time, even hidden things, which you have not known. |
Yameumbwa sasa, wala si tokea zamani; na kabla ya siku hii ya leo hukusikia habari yake; usije ukasema, Tazama, naliyajua. Isaya 48:7 |
They are created now, and not from of old; and before this day you didn't hear them; lest you should say, Behold, I knew them. |
Naam, hukusikia; naam, hukujua; naam, tokea zamani sikio lako halikuzibuka; maana nalijua ya kuwa wewe watenda kwa hila nyingi, nawe umeitwa mkosaji tangu kuzaliwa kwako; Isaya 48:8 |
Yes, you didn't hear; yes, you didn't know; yes, from of old your ear was not opened: for I knew that you did deal very treacherously, and was called a transgressor from the womb. |
kwa ajili ya jina langu nitaahirisha hasira yangu, na kwa ajili yako nitajizuia, ili nisifiwe, wala nisikukatilie mbali. Isaya 48:9 |
For my name's sake will I defer my anger, and for my praise will I refrain for you, that I not cut you off. |
Tazama, nimekusafisha, lakini si kama fedha; nimekuchagua katika tanuru ya mateso. Isaya 48:10 |
Behold, I have refined you, but not as silver; I have chosen you in the furnace of affliction. |
Kwa ajili ya nafsi yangu, kwa ajili ya nafsi yangu, nitatenda haya; je! Litiwe unajisi jina langu? Wala sitampa mwingine utukufu wangu. Isaya 48:11 |
For my own sake, for my own sake, will I do it; for how should [my name] be profaned? and my glory I will not give to another. |
Nisikilize mimi, Ee Yakobo; na Israeli, niliyekuita; mimi ndiye. Mimi ni wa kwanza, na mimi ni wa mwisho pia. Isaya 48:12 |
Listen to me, O Jacob, and Israel my called: I am he; I am the first, I also am the last. |
Naam, mkono wangu umeuweka msingi wa dunia, na mkono wangu wa kuume umezitanda mbingu; niziitapo husimama pamoja. Isaya 48:13 |
Yes, my hand has laid the foundation of the earth, and my right hand has spread out the heavens: when I call to them, they stand up together. |
Kusanyikeni, ninyi nyote, mkasikie; ni nani miongoni mwao aliyehubiri haya? Bwana amempenda; atatimiza mapenzi yake juu ya Babeli, na mkono wake utakuwa juu ya Wakaldayo. Isaya 48:14 |
Assemble yourselves, all you, and hear; who among them has declared these things? He whom Yahweh loves shall perform his pleasure on Babylon, and his arm [shall be on] the Chaldeans. |
Mimi, naam, mimi, nimenena; naam, nimemwita; nimemleta, naye ataifanikisha njia yake. Isaya 48:15 |
I, even I, have spoken; yes, I have called him; I have brought him, and he shall make his way prosperous. |
Nikaribieni, sikieni haya; tokea mwanzo sikunena kwa siri; tangu yalipokuwapo, mimi nipo; na sasa Bwana MUNGU amenituma, na roho yake. Isaya 48:16 |
Come you near to me, hear you this; from the beginning I have not spoken in secret; from the time that it was, there am I: and now the Lord Yahweh has sent me, and his Spirit. |
Bwana, mkombozi wako, mtakatifu wa Israeli, asema hivi; Mimi ni Bwana, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata. Isaya 48:17 |
Thus says Yahweh, your Redeemer, the Holy One of Israel: I am Yahweh your God, who teaches you to profit, who leads you by the way that you should go. |
Laiti ungalisikiliza amri zangu! Ndipo amani yako ingalikuwa kama mto wa maji, na haki yako kama mawimbi ya bahari; Isaya 48:18 |
Oh that you had listened to my commandments! then had your peace been as a river, and your righteousness as the waves of the sea: |
Tena wazao wako wangalikuwa kama mchanga, na hao waliotoka katika tumbo lako kama chembe zake; jina lake lisingalikatika, wala kufutwa mbele zangu. Isaya 48:19 |
your seed also had been as the sand, and the offspring of your loins like the grains of it: his name would not be cut off nor destroyed from before me. |
Haya, tokeni katika Babeli, Kimbieni kutoka kwa Wakaldayo; Hubirini kwa sauti ya kuimba, tangazeni haya, Yatamkeni mpaka mwisho wa dunia, semeni, Bwana amemkomboa mtumishi wake, Yakobo. Isaya 48:20 |
Go you forth from Babylon, flee you from the Chaldeans; with a voice of singing declare you, tell this, utter it even to the end of the earth: say you, Yahweh has redeemed his servant Jacob. |
Wala hawakuona kiu alipowaongoza jangwani; Alitoa maji katika mwamba kwa ajili yao; Pia akaupasua mwamba, maji yakatoka kwa nguvu. Isaya 48:21 |
They didn't thirst when he led them through the deserts; he caused the waters to flow out of the rock for them; he split the rock also, and the waters gushed out. |
Hapana amani kwa wabaya, asema Bwana. Isaya 48:22 |
There is no peace, says Yahweh, to the wicked. |