Tazama, mfalme atamiliki kwa haki, na wakuu watatawala kwa hukumu.
Behold, a king shall reign in righteousness, and princes shall rule in justice.
Na mwanadamu atakuwa kama mahali pa kujificha na upepo, na mahali pa kujisitiri na dhoruba; kama mito ya maji mahali pakavu, kama kivuli cha mwamba mkubwa katika nchi yenye uchovu.
A man shall be as a hiding-place from the wind, and a covert from the tempest, as streams of water in a dry place, as the shade of a great rock in a weary land.
Tena macho yao waonao hayatakuwa na kiwi, na masikio yao wasikiao yatasikiliza.
The eyes of those who see shall not be dim, and the ears of those who hear shall listen.
Tena moyo wa mtu mwenye hamaki utafahamu maarifa, na ndimi zao wenye kigugumizi zitakuwa tayari kunena sawasawa.
The heart of the rash shall understand knowledge, and the tongue of the stammerers shall be ready to speak plainly.
Mpumbavu hataitwa tena mwungwana, wala ayari hatasemwa kwamba ni karimu.
The fool shall be no more called noble, nor the scoundrel be highly respected.
Maana mpumbavu atanena yaliyo upumbavu, na moyo wake utafanya maovu, ili kutenda hila na kusema yasiyo kweli juu ya Bwana, ili kuziacha nafsi za watu wenye njaa hazina kitu, na kukikomesha kinywaji chake mwenye kiu.
For the fool will speak folly, and his heart will work iniquity, to practice profanity, and to utter error against Yahweh, to make empty the soul of the hungry, and to cause the drink of the thirsty to fail.
Tena vyombo vyake ayari ni vibaya; hutunga hila mbaya, ili kuwaangamiza wanyonge kwa maneno ya uongo, mtu mhitaji ajaposema maneno yenye haki.
The instruments of the churl are evil: he devises wicked devices to destroy the humble with lying words, even when the needy speaks right.
Bali mwungwana huwaza mambo ya kiungwana, naye hushika sana mambo ya kiungwana.
But the noble devises noble things; and in noble things shall he continue.
Inukeni, enyi wanawake wenye raha, isikieni sauti yangu; enyi binti za watu msiokuwa na uangalifu, tegeni masikio yenu msikie matamko yangu.
Rise up, you women who are at ease, [and] hear my voice; you careless daughters, give ear to my speech.
Maana mtataabishwa siku kadha wa kadha zaidi ya mwaka, enyi wanawake mliojikinai; kwa sababu mavuno ya mizabibu yatakoma, wakati wa kuvuna vitu vya mashamba hautakuja.
For days beyond a year shall you be troubled, you careless women; for the vintage shall fail, the harvest shall not come.
Tetemekeni, enyi wanawake wenye raha; taabikeni, enyi msiokuwa na uangalifu; jivueni, jivueni nguo zenu kabisa, jivikeni viuno nguo za magunia.
Tremble, you women who are at ease; be troubled, you careless ones; strip yourselves, and make yourselves naked, and gird [sackcloth] on your loins.
Watajipiga vifua kwa ajili ya mashamba mazuri, kwa ajili ya mzabibu uliozaa sana.
They shall strike on the breasts for the pleasant fields, for the fruitful vine.
Juu ya nchi ya watu wangu itamea michongoma na mibigili; naam, juu ya nyumba za furaha katika mji ulio na shangwe;
On the land of my people shall come up thorns and briers; yes, on all the houses of joy in the joyous city.
maana jumba la mfalme litaachwa; mji uliokuwa na watu wengi utakuwa hauna mtu; kilima na mnara utakuwa makao ya wanyama milele, furaha ya punda-mwitu, malisho ya makundi ya kondoo;
For the palace shall be forsaken; the populous city shall be deserted; the hill and the watch-tower shall be for dens forever, a joy of wild donkeys, a pasture of flocks;
hata roho itakapomwagwa juu yetu kutoka juu; hata jangwa litakapokuwa shamba lizaalo sana; nalo shamba lizaalo sana litakapohesabiwa kuwa msitu.
until the Spirit be poured on us from on high, and the wilderness become a fruitful field, and the fruitful field be esteemed as a forest.
Ndipo hukumu itakaa katika jangwa, na haki itakaa katika shamba lizaalo sana.
Then justice shall dwell in the wilderness; and righteousness shall abide in the fruitful field.
Na kazi ya haki itakuwa amani; na mazao ya haki yatakuwa ni utulivu na matumaini daima.
The work of righteousness shall be peace; and the effect of righteousness, quietness and confidence forever.
Na watu wangu watakaa katika kao la amani; na katika maskani zilizo salama, na katika mahali pa kupumzikia penye utulivu.
My people shall abide in a peaceable habitation, and in safe dwellings, and in quiet resting-places.
Lakini mvua ya mawe itakunya, wakati wa kuangushwa miti ya msituni; na huo mji utadhilika.
But it shall hail in the downfall of the forest; and the city shall be utterly laid low.
Heri ninyi mpandao mbegu kando ya maji yote, na kuiacha miguu ya ng'ombe na punda waende ko kote.</p>
Blessed are you who sow beside all waters, who send forth the feet of the ox and the donkey.