Isaya 1 Swahili & English
Listen/Download AudioIsaya 1 (Swahili) | Isaiah 1 (English) |
---|---|
Haya ni maono ya Isaya, mwana wa Amozi, aliyoyaona katika habari za Yuda na Yerusalemu, siku za Uzia na Yothamu na Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda. Isaya 1:1 |
The vision of Isaiah the son of Amoz, which he saw concerning Judah and Jerusalem, in the days of Uzziah, Jotham, Ahaz, and Hezekiah, kings of Judah. |
Sikieni, enyi mbingu, tega sikio, Ee nchi, kwa maana Bwana amenena; Nimewalisha watoto na kuwalea, nao wameniasi. Isaya 1:2 |
Hear, heavens, And listen, earth; for Yahweh has spoken: I have nourished and brought up children, And they have rebelled against me. |
Ng'ombe amjua bwana wake, Na punda ajua kibanda cha bwana wake; Bali Israeli hajui, watu wangu hawafikiri. Isaya 1:3 |
The ox knows his owner, And the donkey his master's crib; But Israel doesn't know, My people don't consider. |
Ole wake, taifa lenye dhambi, watu wanaochukua mzigo wa uovu, wazao wa watenda mabaya, watoto wanaoharibu; wamemwacha Bwana, wamemdharau yeye aliye Mtakatifu wa Israeli, wamefarakana naye na kurudi nyuma. Isaya 1:4 |
Ah sinful nation, A people loaded with iniquity, A seed of evil-doers, Children who deal corruptly! They have forsaken Yahweh. They have despised the Holy One of Israel. They are estranged and backward. |
Mbona mnataka kupigwa hata sasa, hata mkazidi kuasi? Kichwa chote ni kigonjwa, moyo wote umezimia. Isaya 1:5 |
Why should you be beaten more, That you revolt more and more? The whole head is sick, And the whole heart faint. |
Tangu wayo wa mguu hata kichwani hamna uzima ndani yake; bali jeraha na machubuko na vidonda vitokavyo usaha; havikufungwa, havikuzongwa-zongwa, wala havikulainishwa kwa mafuta. Isaya 1:6 |
From the sole of the foot even to the head there is no soundness in it: Wounds, welts, and open sores. They haven't been closed, neither bandaged, neither soothed with oil. |
Nchi yenu ni ukiwa; miji yenu imeteketezwa kwa moto; nchi yenu, wageni wameila mbele ya macho yenu; nayo ni ukiwa, kana kwamba imeangamizwa na wageni. Isaya 1:7 |
Your country is desolate. Your cities are burned with fire. Strangers devour your land in your presence, And it is desolate, As overthrown by strangers. |
Na binti Sayuni ameachwa kama kibanda katika shamba la mizabibu, kama kipenu katika shamba la matango, kama mji uliohusuriwa. Isaya 1:8 |
The daughter of Zion is left like a shelter in a vineyard, Like a hut in a field of melons, Like a besieged city. |
Kama Bwana wa majeshi asingalituachia mabaki machache sana, tungalikuwa kama Sodoma, tungalifanana na Gomora. Isaya 1:9 |
Unless Yahweh of hosts had left to us a very small remnant, We would have been as Sodom; We would have been like Gomorrah. |
Lisikieni neno la Bwana, enyi waamuzi wa Sodoma; tegeni masikio msikie sheria ya Mungu wetu, enyi watu wa Gomora. Isaya 1:10 |
Hear the word of Yahweh, you rulers of Sodom! Listen to the law of our God, you people of Gomorrah! |
Huu wingi wa sadaka zenu mnazonitolea una faida gani? Asema Bwana. Nimejaa mafuta ya kafara za kondoo waume, na mafuta ya wanyama walionona; nami siifurahii damu ya ng'ombe wala ya wana-kondoo wala ya mbuzi waume. Isaya 1:11 |
"What are the multitude of your sacrifices to me?," says Yahweh. "I have had enough of the burnt offerings of rams, And the fat of fed animals. I don't delight in the blood of bulls, Or of lambs, Or of male goats. |
Mjapo ili kuonekana mbele zangu, ni nani aliyetaka neno hili mikononi mwenu, kuzikanyaga nyua zangu? Isaya 1:12 |
When you come to appear before me, Who has required this at your hand, to trample my courts? |
Msilete tena matoleo ya ubatili; uvumba ni chukizo kwangu; mwezi mpya na sabato, kuita makutano; siyawezi maovu hayo na makutano ya ibada. Isaya 1:13 |
Bring no more vain offerings. Incense is an abomination to me; New moons, Sabbaths, and convocations: I can't bear with evil assemblies. |
Sikukuu zenu za mwezi mpya na karamu zenu zilizoamriwa, nafsi yangu yazichukia; mambo hayo yanilemea; nimechoka kuyachukua. Isaya 1:14 |
My soul hates your New Moons and your appointed feasts; They are a burden to me. I am weary of bearing them. |
Nanyi mkunjuapo mikono yenu, nitaficha macho yangu nisiwaone; naam, mwombapo maombi mengi, sitasikia; mikono yenu imejaa damu. Isaya 1:15 |
When you spread forth your hands, I will hide my eyes from you; Yes, when you make many prayers, I will not hear. Your hands are full of blood. |
Jiosheni, jitakaseni; ondoeni uovu wa matendo yenu usiwe mbele za macho yangu; acheni kutenda mabaya; Isaya 1:16 |
Wash yourselves, make yourself clean. Put away the evil of your doings from before my eyes; Cease to do evil. |
jifunzeni kutenda mema; takeni hukumu na haki; wasaidieni walioonewa; mpatieni yatima haki yake; mteteeni mjane. Isaya 1:17 |
Learn to do well. Seek justice, Relieve the oppressed, Judge the fatherless, Plead for the widow." |
Haya, njoni, tusemezane, asema Bwana. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu. Isaya 1:18 |
"Come now, and let us reason together," says Yahweh: "Though your sins be as scarlet, they shall be as white as snow. Though they be red like crimson, they shall be as wool. |
Kama mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi; Isaya 1:19 |
If you are willing and obedient, You shall eat the good of the land; |
bali kama mkikataa na kuasi mtaangamizwa kwa upanga; maana kinywa cha Bwana kimenena haya. Isaya 1:20 |
But if you refuse and rebel, you shall be devoured with the sword; For the mouth of Yahweh has spoken it." |
Mji huu uliokuwa mwaminifu umekuwaje kahaba! Yeye aliyejaa hukumu ya haki; haki ilikaa ndani yake, bali sasa wauaji! Isaya 1:21 |
How the faithful city has become a prostitute! She was full of justice; righteousness lodged in her, But now murderers. |
Fedha yako imekuwa takataka, divai yako imechanganywa na maji. Isaya 1:22 |
Your silver has become dross, Your wine mixed with water. |
Wakuu wako ni waasi, na rafiki za wevi; kila mtu hupenda rushwa, hufuata malipo; hawampatii yatima haki yake, wala maneno ya mjane hayawawasilii. Isaya 1:23 |
Your princes are rebellious, and companions of thieves. Everyone loves bribes, and follows after rewards. They don't judge the fatherless, Neither does the cause of the widow come to them. |
Kwa hiyo, asema Bwana, Bwana wa majeshi, Mwenye enzi, wa Israeli, Nitapata faraja kwa hao wanipingao, nitatwaa kisasi kwa adui zangu; Isaya 1:24 |
Therefore the Lord, Yahweh of Hosts, The Mighty One of Israel, says: "Ah, I will get relief from my adversaries, And avenge myself of my enemies; |
nami nitakuelekezea wewe mkono wangu, na kukutakasa takataka zako kabisa, na kukuondolea bati lako lote; Isaya 1:25 |
And I will turn my hand on you, Thoroughly purge away your dross, And will take away all your tin. |
nami nitarejeza upya waamuzi wako kama walivyokuwa hapo kwanza, na washauri wako kama hapo mwanzo; baada ya hayo utaitwa, Mji wa haki, mji mwaminifu. Isaya 1:26 |
I will restore your judges as at the first, And your counselors as at the beginning. Afterward you shall be called 'The city of righteousness, A faithful town.' |
Sayuni itakombolewa kwa hukumu, na waongofu wake kwa haki. Isaya 1:27 |
Zion shall be redeemed with justice, And her converts with righteousness. |
Lakini kuharibika kwao wakosao nao wenye dhambi kutatokea wakati mmoja, nao wamwachao Bwana watateketezwa. Isaya 1:28 |
But the destruction of transgressors and sinners shall be together, And those who forsake Yahweh shall be consumed. |
Kwa maana watatahayarika kwa sababu ya mialoni mliyoitamani, nanyi mtaaibishwa kwa sababu ya bustani mlizozichagua. Isaya 1:29 |
For they shall be ashamed of the oaks which you have desired, And you shall be confounded for the gardens that you have chosen. |
Maana mtakuwa kama mwaloni ambao majani yake yakauka, na kama bustani isiyo na maji. Isaya 1:30 |
For you shall be as an oak whose leaf fades, And as a garden that has no water. |
Na mtu hodari atakuwa kama makumbi, na kazi yake kama cheche ya moto; nao watawaka pamoja, wala hapana atakayewazima. Isaya 1:31 |
The strong will be like tinder, And his work like a spark. They will both burn together, And no one will quench them." |