Isaya 57 Swahili & English
Listen/Download AudioIsaya 57 (Swahili) | Isaiah 57 (English) |
---|---|
Mwenye haki hupotea, wala hakuna atiaye hayo moyoni; na watu watauwa huondolewa, wala hakuna afikiriye ya kuwa mwenye haki ameondolewa asipatikane na mabaya. Isaya 57:1 |
The righteous perishes, and no man lays it to heart; and merciful men are taken away, none considering that the righteous is taken away from the evil [to come]. |
Yeye huingia katika amani; wao hustarehe katika vitanda vyao, kila mtu aendaye katika unyofu wake. Isaya 57:2 |
He enters into peace; they rest in their beds, each one who walks in his uprightness. |
Lakini ninyi karibuni hapa, enyi wana wa mwanamke mchawi, uzao wa mzinzi na kahaba. Isaya 57:3 |
But draw near here, you sons of the sorceress, the seed of the adulterer and the prostitute. |
Mnafanya dhihaka yenu juu ya nani? Mmepanua vinywa vyenu, na kutoa ndimi zenu? Je, ninyi si wana wa uasi, uzao wa uongo; Isaya 57:4 |
Against whom do you sport yourselves? against whom make you a wide mouth, and put out the tongue? Aren't you children of disobedience, a seed of falsehood, |
ninyi mnaowasha tamaa zenu kati ya mialoni, chini ya kila mti wenye majani mabichi; ninyi mnaoua watoto mabondeni, chini ya mianya ya majabali? Isaya 57:5 |
you who inflame yourselves among the oaks, under every green tree; who kill the children in the valleys, under the clefts of the rocks? |
Sehemu yako i katika makokoto ya bonde; hayo ndiyo kura yako; umeyamwagia hayo sadaka ya kinywaji, umeyatolea sadaka ya unga; je! Niwe radhi na mambo hayo? Isaya 57:6 |
Among the smooth [stones] of the valley is your portion; they, they are your lot; even to them have you poured a drink-offering, you have offered an offering. Shall I be appeased for these things? |
Umeweka kitanda chako juu ya mlima mrefu ulioinuka sana; ukaenda huko ili kutoa dhabihu. Isaya 57:7 |
On a high and lofty mountain have you set your bed; there also you went up to offer sacrifice. |
Na nyuma ya milango na miimo umeweka kumbukumbu lako; kwa maana umejifunua nafsi yako kwa ajili ya mwingine, si kwa ajili yangu, ukakwea juu; umekipanua kitanda chako, nawe umefanya maagano na hao; ulikipenda kitanda chao hapo ulipokiona. Isaya 57:8 |
Behind the doors and the posts have you set up your memorial: for you have uncovered [yourself] to another than me, and are gone up; you have enlarged your bed, and made you a covenant with them: you loved their bed where you saw it. |
Ulimwendea mfalme na mafuta ya marhamu, ukaongeza manukato yako, ukawatuma wajumbe wako waende mbali, ukajidhili sana hata kuzimu. Isaya 57:9 |
You went to the king with oil, and did increase your perfumes, and did send your ambassadors far off, and did debase yourself even to Sheol. |
Ulikuwa umechoka kwa ajili ya urefu wa njia yako; lakini hukusema, Hapana matumaini; ulipata kuhuishwa nguvu zako; kwa sababu hiyo hukuugua. Isaya 57:10 |
You were wearied with the length of your way; yet you didn't say, It is in vain: you found a reviving of your strength; therefore you weren't faint. |
Tena ni nani uliyemwogopa na kumhofu, hata ukasema uongo, wala hukunikumbuka mimi, wala kuweka hayo moyoni? Je! Mimi sikunyamaza tangu zamani, hata huniogopi? Isaya 57:11 |
Of whom have you been afraid and in fear, that you lie, and have not remembered me, nor laid it to your heart? Haven't I held my peace even of long time, and you don't fear me? |
Mimi nitatangaza haki yako, na matendo yako hayatakufaa. Isaya 57:12 |
I will declare your righteousness; and as for your works, they shall not profit you. |
Utakapolia, na wakuponye hao uliowakusanya; lakini upepo utawachukua; uvuvio tu utawachukulia mbali; lakini yeye anayenitumaini ataimiliki nchi, na kuurithi mlima wangu mtakatifu. Isaya 57:13 |
When you cry, let those who you have gathered deliver you; but the wind shall take them, a breath shall carry them all away: but he who takes refuge in me shall possess the land, and shall inherit my holy mountain. |
Naye atasema, Tutieni, tutieni, Itengenezeni njia, Kiondoeni kila kikwazacho Katika njia ya watu wangu. Isaya 57:14 |
He will say, Cast up, cast up, prepare the way, take up the stumbling-block out of the way of my people. |
Maana yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu. Isaya 57:15 |
For thus says the high and lofty One who inhabits eternity, whose name is Holy: I dwell in the high and holy place, with him also who is of a contrite and humble spirit, to revive the spirit of the humble, and to revive the heart of the contrite. |
Kwa kuwa sitashindana na watu siku zote, wala sitakuwa na hasira siku zote; maana roho ingezimia mbele zangu, na hizo nafsi nilizozifanya. Isaya 57:16 |
For I will not contend forever, neither will I be always angry; for the spirit would faint before me, and the souls who I have made. |
Kwa sababu ya uovu wa kutamani kwake naliona hasira, nikampiga; nalificha uso wangu, nikaona ghadhabu; naye akaendelea kwa ukaidi, kuifuata njia ya moyo wake mwenyewe. Isaya 57:17 |
For the iniquity of his covetousness was I angry, and struck him; I hid [my face] and was angry; and he went on backsliding in the way of his heart. |
Nimeziona njia zake; nami nitamponya; nitamwongoza pia, nitamrudishia faraja zake, yeye na hao wanaomlilia. Isaya 57:18 |
I have seen his ways, and will heal him: I will lead him also, and restore comforts to him and to his mourners. |
Mimi nayaumba matunda ya midomo; Amani, amani, kwake yeye aliye mbali, na kwake yeye aliye karibu; asema Bwana; nami nitamponya. Isaya 57:19 |
I create the fruit of the lips: Peace, peace, to him who is far off and to him who is near, says Yahweh; and I will heal him. |
Bali wabaya wanafanana na bahari iliyochafuka; maana haiwezi kutulia, na maji yake hutoa tope na takataka. Isaya 57:20 |
But the wicked are like the troubled sea; for it can't rest, and its waters cast up mire and dirt. |
Hapana amani kwa wabaya; asema Mungu wangu. Isaya 57:21 |
There is no peace, says my God, to the wicked. |