Isaya 18 Swahili & English
Listen/Download AudioIsaya 18 (Swahili) | Isaiah 18 (English) |
---|---|
Ole wa nchi ya uvumi wa mabawa, Iliyoko mbali kupita mito ya Kushi; Isaya 18:1 |
Ah, the land of the rustling of wings, which is beyond the rivers of Ethiopia; |
Ipelekayo wajumbe wake kwa njia ya bahari, Na katika vyombo vya manyasi juu ya maji. Nendeni, wajumbe wepesi,kwa watu warefu,laini; Watu watishao tangu mwanzo wao hata sasa; Taifa la wenye nguvu,wakanyagao watu, Ambao mito inakata nchi yao. Isaya 18:2 |
that sends ambassadors by the sea, even in vessels of papyrus on the waters, [saying], Go, you swift messengers, to a nation tall and smooth, to a people awesome from their beginning onward, a nation that measures out and treads down, whose land the rivers divide! |
Enyi watu mkaao katika ulimwengu wote, na wenyeji wa dunia, bendera ikiinuliwa milimani, angalieni; na wakipiga tarumbeta, sikieni. Isaya 18:3 |
All you inhabitants of the world, and you dwellers on the earth, when an ensign is lifted up on the mountains, look; and when the trumpet is blown, listen. |
Maana Bwana ameniambia hivi, Mimi nitatulia, na kuangalia katika makazi yangu, kama wakati wa mwangaza mweupe wa jua kali, mfano wa wingu la umande katika hari ya mavuno. Isaya 18:4 |
For thus has Yahweh said to me, I will be still, and I will see in my dwelling-place, like clear heat in sunshine, like a cloud of dew in the heat of harvest. |
Maana kabla ya mavuno, maua yaangukapo, na maua yakawa zabibu zianzazo kuiva, ndipo atakapoyakata matawi kwa miundu, na kuviondoa vitawi vilivyopanuka na kuvikata. Isaya 18:5 |
For before the harvest, when the blossom is over, and the flower becomes a ripening grape, he will cut off the sprigs with pruning-hooks, and the spreading branches will he take away [and] cut down. |
Wote pamoja wataachiwa ndege wakali wa milimani, na hayawani wa nchi; ndege wakali watakaa juu yao wakati wa jua, na hayawani wote wa nchi watakaa juu yao wakati wa baridi. Isaya 18:6 |
They shall be left together to the ravenous birds of the mountains, and to the animals of the earth; and the ravenous birds shall summer on them, and all the animals of the earth shall winter on them. |
Wakati huo Bwana wa majeshi ataletewa hedaya na watu warefu, laini; Watu watishao tangu mwanzo wao hata sasa; Taifa la wenye nguvu, wakanyagao watu, Ambao mito inakata nchi yao; mpaka mahali pa jina la Bwana wa majeshi,mlima Sayuni. Isaya 18:7 |
In that time shall a present be brought to Yahweh of Hosts [from] a people tall and smooth, even from a people awesome from their beginning onward, a nation that measures out and treads down, whose land the rivers divide, to the place of the name of Yahweh of Hosts, Mount Zion. |