Isaya 43 Swahili & English
Listen/Download AudioIsaya 43 (Swahili) | Isaiah 43 (English) |
---|---|
Lakini sasa, Bwana aliyekuhuluku, Ee Yakobo, yeye aliyekuumba, Ee Israeli, asema hivi, Usiogope, maana nimekukomboa; nimekuita kwa jina lako, wewe u wangu. Isaya 43:1 |
But now thus says Yahweh who created you, Jacob, and he who formed you, Israel: Don't be afraid, for I have redeemed you; I have called you by your name, you are mine. |
Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe; na katika mito, haitakugharikisha; uendapo katika moto, hutateketea; wala mwali wa moto hautakuunguza. Isaya 43:2 |
When you pass through the waters, I will be with you; and through the rivers, they shall not overflow you: when you walk through the fire, you shall not be burned, neither shall the flame kindle on you. |
Maana mimi ni Bwana, Mungu wako; Mtakatifu wa Israeli, mwokozi wako, nimetoa Misri kuwa ukombozi wako; nimetoa Kushi na Seba kwa ajili yako. Isaya 43:3 |
For I am Yahweh your God, the Holy One of Israel, your Savior; I have given Egypt as your ransom, Ethiopia and Seba in your place. |
Kwa kuwa ulikuwa wa thamani machoni pangu, na mwenye kuheshimiwa, nami nimekupenda; kwa sababu hiyo nitatoa watu kwa ajili yako; na kabila za watu kwa ajili ya maisha yako. Isaya 43:4 |
Since you have been precious in my sight, [and] honorable, and I have loved you; therefore will I give men in your place, and peoples instead of your life. |
Usiogope; maana mimi ni pamoja nawe; nitaleta wazao wako toka mashariki, nitakukusanya toka magharibi; Isaya 43:5 |
Don't be afraid; for I am with you: I will bring your seed from the east, and gather you from the west; |
nitaiambia kaskazi, Toa; nayo kusi, Usizuie; waleteni wana wangu kutoka mbali, na binti zangu kutoka miisho ya dunia. Isaya 43:6 |
I will tell the north, Give up; and to the south, Don't keep back; bring my sons from far, and my daughters from the end of the earth; |
Kila mmoja aliyeitwa kwa jina langu, niliyemwumba kwa ajili ya utukufu wangu; mimi nimemwumba, naam, mimi nimemfanya. Isaya 43:7 |
everyone who is called by my name, and whom I have created for my glory, whom I have formed, yes, whom I have made. |
Walete vipofu walio na macho, na viziwi walio na masikio. Isaya 43:8 |
Bring forth the blind people who have eyes, and the deaf who have ears. |
Na wakusanyike mataifa yote, kabila zote wakutanike; ni nani miongoni mwao awezaye kuhubiri neno hili, na kutuonyesha mambo ya zamani? Na walete mashahidi wao, wapate kuhesabiwa kuwa na haki; au na wasikie, wakaseme, Ni kweli. Isaya 43:9 |
Let all the nations be gathered together, and let the peoples be assembled: who among them can declare this, and show us former things? let them bring their witnesses, that they may be justified; or let them hear, and say, It is truth. |
Ninyi ni mashahidi wangu, asema Bwana, na mtumishi niliyemchagua; mpate kujua, na kuniamini, na kufahamu ya kuwa mimi ndiye; kabla yangu hakuumbwa Mungu awaye yote, wala baada yangu mimi hatakuwapo mwingine. Isaya 43:10 |
You are my witnesses, says Yahweh, and my servant whom I have chosen; that you may know and believe me, and understand that I am he: before me there was no God formed, neither shall there be after me. |
Mimi, naam, mimi, ni Bwana, zaidi yangu mimi hapana mwokozi. Isaya 43:11 |
I, even I, am Yahweh; and besides me there is no savior. |
Nimetangaza habari, nimeokoa, nimeonyesha, na hapakuwa mungu wa kigeni kati yenu; kwa sababu hiyo ninyi ni mashahidi wangu, asema Bwana, nami ni Mungu. Isaya 43:12 |
I have declared, and I have saved, and I have shown; and there was no strange [god] among you: therefore you are my witnesses, says Yahweh, and I am God. |
Naam, tangu siku ya leo, mimi ndiye; wala hapana awezaye kuokoa katika mkono wangu; mimi nitatenda kazi, naye ni nani awezaye kuizuia? Isaya 43:13 |
Yes, since the day was I am he; and there is none who can deliver out of my hand: I will work, and who can hinder it? |
Bwana, Mkombozi wenu, Mtakatifu wa Israeli, asema hivi; Kwa ajili yenu nimetuma ujumbe Babeli nami nitawashusha wote mfano wa wakimbizi, naam, Wakaldayo, katika merikebu zao walizozifurahia. Isaya 43:14 |
Thus says Yahweh, your Redeemer, the Holy One of Israel: For your sake I have sent to Babylon, and I will bring down all of them as fugitives, even the Chaldeans, in the ships of their rejoicing. |
Mimi ni Bwana, Mtakatifu wenu, Muumba wa Israeli, mfalme wenu. Isaya 43:15 |
I am Yahweh, your Holy One, the Creator of Israel, your King. |
Bwana asema hivi, yeye afanyaye njia katika bahari; na mahali pa kupita katika maji yenye nguvu; Isaya 43:16 |
Thus says Yahweh, who makes a way in the sea, and a path in the mighty waters; |
atoaye gari na farasi, jeshi la askari na uwezo; wamelala, hawataondoka; wametoweka, wamezimwa mfano wa utambi. Isaya 43:17 |
who brings forth the chariot and horse, the army and the mighty man (they lie down together, they shall not rise; they are extinct, they are quenched as a wick): |
Msiyakumbuke mambo ya kwanza, wala msiyatafakari mambo ya zamani. Isaya 43:18 |
Don't remember the former things, neither consider the things of old. |
Tazama, nitatenda neno jipya; sasa litachipuka; je! Hamtalijua sasa? Nitafanya njia hata jangwani, na mito ya maji nyikani. Isaya 43:19 |
Behold, I will do a new thing; now shall it spring forth; shall you not know it? I will even make a way in the wilderness, and rivers in the desert. |
Wanyama wa kondeni wataniheshimu, mbweha pia na mbuni; kwa sababu nimewapa maji jangwani, na mito nyikani, ili kuwanywesha watu wangu, wateule wangu; Isaya 43:20 |
The animals of the field shall honor me, the jackals and the ostriches; because I give waters in the wilderness, and rivers in the desert, to give drink to my people, my chosen, |
watu wale niliojiumbia nafsi yangu, ili wazitangaze sifa zangu. Isaya 43:21 |
the people which I formed for myself, that they might set forth my praise. |
Lakini hukuniita, Ee Yakobo, bali umechoka nami, Ee Israeli. Isaya 43:22 |
Yet you have not called on me, Jacob; but you have been weary of me, Israel. |
Hukuniletea wana-kondoo kuwa kafara zako, wala hukuniheshimu kwa dhabihu zako. Sikukutumikisha kwa matoleo, wala sikukuchosha kwa ubani. Isaya 43:23 |
You have not brought me of your sheep for burnt offerings; neither have you honored me with your sacrifices. I have not burdened you with offerings, nor wearied you with frankincense. |
Hukuninunulia manukato kwa fedha, wala hukunishibisha kwa mafuta ya sadaka zako; bali umenitumikisha kwa dhambi zako, umenichosha kwa maovu yako. Isaya 43:24 |
You have bought me no sweet cane with money, neither have you filled me with the fat of your sacrifices; but you have burdened me with your sins, you have wearied me with your iniquities. |
Mimi, naam, mimi, ndimi niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka dhambi zako. Isaya 43:25 |
I, even I, am he who blots out your transgressions for my own sake; and I will not remember your sins. |
Unikumbushe, na tuhojiane; eleza mambo yako, upate kupewa haki yako. Isaya 43:26 |
Put me in remembrance; let us plead together: set you forth [your cause], that you may be justified. |
Baba yako wa kwanza alifanya dhambi, na wakalimani wako wameniasi. Isaya 43:27 |
Your first father sinned, and your teachers have transgressed against me. |
Kwa hiyo nitawatia unajisi wakuu wa patakatifu, nami nitamfanya Yakobo kuwalaani, na Israeli kuwa tukano. Isaya 43:28 |
Therefore I will profane the princes of the sanctuary; and I will make Jacob a curse, and Israel a reviling. |