Ayabu 6 Swahili & English
Listen/Download AudioAyabu 6 (Swahili) | Job 6 (English) |
---|---|
Ndipo Ayubu akajibu na kusema, Ayabu 6:1 |
Then Job answered, |
Laiti uchungu wangu ungepimwa, Na msiba wangu kutiwa katika mizani pamoja! Ayabu 6:2 |
"Oh that my anguish were weighed, And all my calamity laid in the balances! |
Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa bahari; Kwa hiyo maneno yangu yamekuwa ya haraka. Ayabu 6:3 |
For now it would be heavier than the sand of the seas, Therefore have my words been rash. |
Kwa kuwa mishale ya huyo Mwenyezi i ndani yangu, Na roho yangu inainywa sumu yake; Vitisho vya Mungu vimejipanga juu yangu. Ayabu 6:4 |
For the arrows of the Almighty are within me, My spirit drinks up their poison. The terrors of God set themselves in array against me. |
Je! Huyo punda-mwitu hulia akiwa na majani? Au, ng'ombe hulia malishoni? Ayabu 6:5 |
Does the wild donkey bray when he has grass? Or does the ox low over his fodder? |
Je! Kitu kisicho na ladha yumkini kulika pasipo chumvi? Au je, uto wa yai una tamu iwayo yote? Ayabu 6:6 |
Can that which has no flavor be eaten without salt? Or is there any taste in the white of an egg? |
Roho yangu inakataa hata kuvigusa; Kwangu mimi ni kama chakula kichukizacho. Ayabu 6:7 |
My soul refuses to touch them; They are as loathsome food to me. |
Laiti ningepewa haja yangu, Naye Mungu angenipa neno hilo ninalolitamani sana! Ayabu 6:8 |
"Oh that I might have my request; That God would grant the thing that I long for! |
Kwamba Mungu angekuwa radhi kuniseta; Kwamba angeulegeza mkono wake na kunikatilia mbali! Ayabu 6:9 |
Even that it would please God to crush me; That he would let loose his hand, and cut me off! |
Hapo ndipo ningefarijika hata sasa; Naam, ningejikuza katika maumivu yasiyoniacha; Kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu. Ayabu 6:10 |
Be it still my consolation, Yes, let me exult in pain that doesn't spare, That I have not denied the words of the Holy One. |
Nguvu zangu ni zipi, hata ningoje? Na mwisho wangu ni nini, hata nisubiri? Ayabu 6:11 |
What is my strength, that I should wait? What is my end, that I should be patient? |
Je! Nguvu zangu ni nguvu za mawe? Au mwili wangu, je! Ni shaba? Ayabu 6:12 |
Is my strength the strength of stones? Or is my flesh of brass? |
Je! Si kwamba sina msaada ndani yangu. Tena kwamba kufanikiwa kumeondolewa mbali nami? Ayabu 6:13 |
Isn't it that I have no help in me, That wisdom is driven quite from me? |
Kwake huyo atakaye kuzima roho inapasa atendewe mema na rafiki; Hata kwake huyo aachaye kumcha Mwenyezi. Ayabu 6:14 |
"To him who is ready to faint, kindness should be shown from his friend; Even to him who forsakes the fear of the Almighty. |
Ndugu zangu wametenda udanganyifu kama kijito cha maji. Mfano wa fumbi la vijito vipitavyo. Ayabu 6:15 |
My brothers have dealt deceitfully as a brook, As the channel of brooks that pass away; |
Vilivyokuwa vyeusi kwa sababu ya barafu, Ambamo theluji hujificha. Ayabu 6:16 |
Which are black by reason of the ice, in which the snow hides itself: |
Wakati vipatapo moto hutoweka; Kukiwako hari, hukoma mahali pao. Ayabu 6:17 |
In the dry season, they vanish. When it is hot, they are consumed out of their place. |
Misafara isafiriyo kwa njia yao hugeuka; Hukwea kwenda barani, na kupotea. Ayabu 6:18 |
The caravans that travel beside them turn aside; They go up into the waste, and perish. |
Misafara ya Tema huvitazama, Majeshi ya Sheba huvingojea. Ayabu 6:19 |
The caravans of Tema looked, The companies of Sheba waited for them. |
Wametahayari kwa sababu walitumaini; Wakaja huku, nao walifadhaika. Ayabu 6:20 |
They were distressed because they were confident; They came there, and were confounded. |
Kwani sasa ninyi mmekuwa vivyo; Mwaona jambo la kutisha, mkaogopa. Ayabu 6:21 |
For now you are nothing. You see a terror, and are afraid. |
Je! Nilisema, Nipeni? Au, Nitoleeni toleo katika mali yenu? Ayabu 6:22 |
Did I say, 'Give to me?' Or, 'Offer a present for me from your substance?' |
Au, Niokoeni na mkono wa adui? Au, Nikomboeni na mikono ya hao waoneao? Ayabu 6:23 |
Or, 'Deliver me from the adversary's hand?' Or, 'Redeem me from the hand of the oppressors?' |
Nifunzeni, nami nitanyamaa kimya; Mkanijulishe ni jambo gani nililokosa. Ayabu 6:24 |
"Teach me, and I will hold my peace; Cause me to understand wherein I have erred. |
Jinsi yafaavyo maneno ya uelekevu! Lakini kuhoji kwenu, je! Kumeonya nini? Ayabu 6:25 |
How forcible are words of uprightness! But your reproof, what does it reprove? |
Je! Mwafikiri kuyakemea maneno? Maana maneno ya huyo aliyekata tamaa ni kama upepo. Ayabu 6:26 |
Do you intend to reprove words, Seeing that the speeches of one who is desperate are as wind? |
Naam, mwapenda kuwapigia kura hao mayatima, Na kufanya biashara ya rafiki yenu. Ayabu 6:27 |
Yes, you would even cast lots for the fatherless, And make merchandise of your friend. |
Sasa basi iweni radhi kuniangalia; Kwani hakika sitanena uongo usoni penu. Ayabu 6:28 |
Now therefore be pleased to look at me, For surely I shall not lie to your face. |
Rudini, nawasihi, lisiwe neno la udhalimu; Naam, rudini tena, neno langu ni la haki. Ayabu 6:29 |
Please return. Let there be no injustice; Yes, return again, my cause is righteous. |
Je! Mna udhalimu ulimini mwangu? Je! Makaakaa yangu hayatambui mambo ya madhara? Ayabu 6:30 |
Is there injustice on my tongue? Can't my taste discern mischievous things? |