Ayabu 40 Swahili & English
Listen/Download AudioAyabu 40 (Swahili) | Job 40 (English) |
---|---|
Bwana akafuliza kumjibu Ayubu, na kusema, Ayabu 40:1 |
Moreover Yahweh answered Job, |
Je! Mwenye hoja atashindana na Mwenyezi? Mwenye kujadiliana na Mungu, na ajibu yeye. Ayabu 40:2 |
"Shall he who argues contend with the Almighty? He who argues with God, let him answer it." |
Ndipo Ayubu akamjibu Mungu, na kusema, Ayabu 40:3 |
Then Job answered Yahweh, |
Tazama, mimi si kitu kabisa, nikujibu nini? Naweka mkono wangu kinywani pangu. Ayabu 40:4 |
"Behold, I am of small account. What shall I answer you? I lay my hand on my mouth. |
Nimenena mara moja, nami sitajibu; Naam, nimenena mara mbili, lakini sitaendelea zaidi. Ayabu 40:5 |
I have spoken once, and I will not answer; Yes, twice, but I will proceed no further." |
Ndipo Bwana akamjibu Ayubu katika upepo wa kisulisuli, na kusema, Ayabu 40:6 |
Then Yahweh answered Job out of the whirlwind, |
Jifunge viuno kama mwanamume, Mimi nitakuuliza neno, nawe niambie. Ayabu 40:7 |
"Now brace yourself like a man. I will question you, and you will answer me. |
Je! Hata hukumu yangu utaibatilisha? Utanitia mimi hatiani, upate kuhesabiwa haki? Ayabu 40:8 |
Will you even annul my judgment? Will you condemn me, that you may be justified? |
Au je! Wewe una mkono kama Mungu? Waweza kutoa ngurumo kwa sauti kama yeye? Ayabu 40:9 |
Or have you an arm like God? Can you thunder with a voice like him? |
Haya! Jivike sasa fahari na ukuu; Jipambe heshima na enzi. Ayabu 40:10 |
"Now deck yourself with excellency and dignity. Array yourself with honor and majesty. |
Mwaga mafuriko ya hasira zako, Ukamtazame kila mtu mwenye kiburi, ukamdhili. Ayabu 40:11 |
Pour forth the fury of your anger. Look on everyone who is proud, and bring him low. |
Mtazame kila mtu mwenye kiburi ukamshushe, Ukawakanyage waovu hapo wasimamapo. Ayabu 40:12 |
Look on everyone who is proud, and humble him. Crush the wicked in their place. |
Wafiche mavumbini pamoja, Wafunge nyuso zao mahali palipositirika. Ayabu 40:13 |
Hide them in the dust together. Bind their faces in the hidden place. |
Ndipo mimi nami nitazikiri habari zako, Ya kuwa mkono wako wa kuume waweza kukuokoa. Ayabu 40:14 |
Then I will also admit to you That your own right hand can save you. |
Mwangalie huyo kiboko, niliyemwumba pamoja nawe; Yeye hula nyasi kama vile ng'ombe, Ayabu 40:15 |
"See now, behemoth, which I made as well as you. He eats grass as an ox. |
Tazama basi, nguvu zake ni katika viuno vyake, Na uwezo wake u katika mishipa ya tumbo lake. Ayabu 40:16 |
Look now, his strength is in his loins, His force is in the muscles of his belly. |
Yeye hutikisa mkia wake mfano wa mwerezi; Mishipa ya mapaja yake yanaungamana pamoja. Ayabu 40:17 |
He moves his tail like a cedar: The sinews of his thighs are knit together. |
Mifupa yake ni kama mirija ya shaba; Mbavu zake ni kama vipande vya chuma. Ayabu 40:18 |
His bones are like tubes of brass. His limbs are like bars of iron. |
Yeye ni mkuu wa njia za Mungu; Yeye aliyemfanya alimpa upanga wake. Ayabu 40:19 |
He is the chief of the ways of God. He who made him gives him his sword. |
Hakika milima humtolea chakula; Hapo wachezapo wanyama wote wa barani. Ayabu 40:20 |
Surely the mountains bring him forth food, Where all the animals of the field do play. |
Hulala chini ya miti yenye vivuli, Mafichoni penye mianzi, na matopeni. Ayabu 40:21 |
He lies under the lotus trees, In the covert of the reed, and the marsh. |
Hiyo miti yenye vivuli humfunika kwa vivuli vyao; Mierebi ya vijito humzunguka. Ayabu 40:22 |
The lotuses cover him with their shade. The willows of the brook surround him. |
Tazama, mto ukifurika, yeye hatetemeki; Hujiona yu salama, ijapokuwa Yordani hufurika hata kinywani pake. Ayabu 40:23 |
Behold, if a river overflows, he doesn't tremble. He is confident, though the Jordan swells even to his mouth. |
Je! Mtu ye yote atamnasa akiwa yu macho, Au, kumtoboa pua yake kwa mtego? Ayabu 40:24 |
Shall any take him when he is on the watch, Or pierce through his nose with a snare? |