Ayabu 17 Swahili & English
Listen/Download AudioAyabu 17 (Swahili) | Job 17 (English) |
---|---|
Roho yangu imezimika, siku zangu zimekoma, Kaburi i tayari kunipokea. Ayabu 17:1 |
"My spirit is consumed, my days are extinct, And the grave is ready for me. |
Ni kweli wako kwangu wenye kufanya dhihaka, Jicho langu hukaa katika kunifanyia uchungu kwao. Ayabu 17:2 |
Surely there are mockers with me, My eye dwells on their provocation. |
Nipe rehani basi, uwe dhamana kwa ajili yangu kwako wewe mwenyewe; Kuna nani atakayeniwekea dhamana? Ayabu 17:3 |
"Now give a pledge, be collateral for me with yourself. Who is there who will strike hands with me? |
Kwani mioyo yao imeificha ufahamu; Kwa hiyo hutawakuza. Ayabu 17:4 |
For you have hidden their heart from understanding, Therefore shall you not exalt them. |
Awafitiniye rafiki zake wawe mawindo, Hata macho ya watoto wake yataingia kiwi. Ayabu 17:5 |
He who denounces his friends for a prey, Even the eyes of his children shall fail. |
Amenifanya niwe simo kwa watu; Nimekuwa mwenye kuchukiwa kwa wazi. Ayabu 17:6 |
"But he has made me a byword of the people. They spit in my face. |
Jicho langu nalo limekuwa giza kwa sababu ya majonzi, Na via vyangu vyote vimekuwa kama kivuli. Ayabu 17:7 |
My eye also is dim by reason of sorrow. All my members are as a shadow. |
Walekevu watayastaajabia hayo, Na asiye na hatia atajiamsha juu ya mpotovu. Ayabu 17:8 |
Upright men shall be astonished at this. The innocent shall stir up himself against the godless. |
Lakini mwenye haki ataishika njia yake, Naye mwenye mikono safi atazidi kupata nguvu. Ayabu 17:9 |
Yet shall the righteous hold on his way. He who has clean hands shall grow stronger and stronger. |
Lakini rudini; ninyi nyote, njoni sasa; Wala sitampata mtu mwenye hekima kati yenu. Ayabu 17:10 |
But as for you all, come on now again; I shall not find a wise man among you. |
Siku zangu zimepita, makusudi yangu yamevunjika, Hata hayo niliyo nayo moyoni mwangu. Ayabu 17:11 |
My days are past, my plans are broken off, As are the thoughts of my heart. |
Wabadili usiku kuwa mchana; Wasema, Mwanga u karibu kwa sababu ya giza. Ayabu 17:12 |
They change the night into day, Saying 'The light is near' in the presence of darkness. |
Nikitazamia kuzimu kuwa nyumba yangu; Nikitandika malazi yangu gizani; Ayabu 17:13 |
If I look for Sheol as my house, If I have spread my couch in the darkness, |
Ikiwa nimeuita uharibifu, Wewe u baba yangu; Na kuliambia buu, Wewe u mama yangu, na umbu langu; Ayabu 17:14 |
If I have said to corruption, 'You are my father;' To the worm, 'My mother,' and 'my sister;' |
Basi, tumaini langu li wapi? Na tumaini langu, ni nani atakayeliona? Ayabu 17:15 |
Where then is my hope? As for my hope, who shall see it? |
Litashuka kwenye makomeo ya kuzimu, Itakapokuwapo raha mavumbini. Ayabu 17:16 |
Shall it go down with me to the gates of Sheol, Or descend together into the dust?" |