Roho yangu imezimika, siku zangu zimekoma, Kaburi i tayari kunipokea.
"My spirit is consumed, my days are extinct, And the grave is ready for me.
Ni kweli wako kwangu wenye kufanya dhihaka, Jicho langu hukaa katika kunifanyia uchungu kwao.
Surely there are mockers with me, My eye dwells on their provocation.
Nipe rehani basi, uwe dhamana kwa ajili yangu kwako wewe mwenyewe; Kuna nani atakayeniwekea dhamana?
"Now give a pledge, be collateral for me with yourself. Who is there who will strike hands with me?
Kwani mioyo yao imeificha ufahamu; Kwa hiyo hutawakuza.
For you have hidden their heart from understanding, Therefore shall you not exalt them.
Awafitiniye rafiki zake wawe mawindo, Hata macho ya watoto wake yataingia kiwi.
He who denounces his friends for a prey, Even the eyes of his children shall fail.
Amenifanya niwe simo kwa watu; Nimekuwa mwenye kuchukiwa kwa wazi.
"But he has made me a byword of the people. They spit in my face.
Jicho langu nalo limekuwa giza kwa sababu ya majonzi, Na via vyangu vyote vimekuwa kama kivuli.
My eye also is dim by reason of sorrow. All my members are as a shadow.
Walekevu watayastaajabia hayo, Na asiye na hatia atajiamsha juu ya mpotovu.
Upright men shall be astonished at this. The innocent shall stir up himself against the godless.
Lakini mwenye haki ataishika njia yake, Naye mwenye mikono safi atazidi kupata nguvu.
Yet shall the righteous hold on his way. He who has clean hands shall grow stronger and stronger.
Lakini rudini; ninyi nyote, njoni sasa; Wala sitampata mtu mwenye hekima kati yenu.
But as for you all, come on now again; I shall not find a wise man among you.
Siku zangu zimepita, makusudi yangu yamevunjika, Hata hayo niliyo nayo moyoni mwangu.
My days are past, my plans are broken off, As are the thoughts of my heart.
Wabadili usiku kuwa mchana; Wasema, Mwanga u karibu kwa sababu ya giza.
They change the night into day, Saying 'The light is near' in the presence of darkness.
Nikitazamia kuzimu kuwa nyumba yangu; Nikitandika malazi yangu gizani;
If I look for Sheol as my house, If I have spread my couch in the darkness,
Ikiwa nimeuita uharibifu, Wewe u baba yangu; Na kuliambia buu, Wewe u mama yangu, na umbu langu;
If I have said to corruption, 'You are my father;' To the worm, 'My mother,' and 'my sister;'
Basi, tumaini langu li wapi? Na tumaini langu, ni nani atakayeliona?
Where then is my hope? As for my hope, who shall see it?
Litashuka kwenye makomeo ya kuzimu, Itakapokuwapo raha mavumbini.
Shall it go down with me to the gates of Sheol, Or descend together into the dust?"