Ayabu 17 Swahili & English

Listen/Download Audio
Ayabu 17 (Swahili) Job 17 (English)

Roho yangu imezimika, siku zangu zimekoma, Kaburi i tayari kunipokea. Ayabu 17:1

"My spirit is consumed, my days are extinct, And the grave is ready for me.

Ni kweli wako kwangu wenye kufanya dhihaka, Jicho langu hukaa katika kunifanyia uchungu kwao. Ayabu 17:2

Surely there are mockers with me, My eye dwells on their provocation.

Nipe rehani basi, uwe dhamana kwa ajili yangu kwako wewe mwenyewe; Kuna nani atakayeniwekea dhamana? Ayabu 17:3

"Now give a pledge, be collateral for me with yourself. Who is there who will strike hands with me?

Kwani mioyo yao imeificha ufahamu; Kwa hiyo hutawakuza. Ayabu 17:4

For you have hidden their heart from understanding, Therefore shall you not exalt them.

Awafitiniye rafiki zake wawe mawindo, Hata macho ya watoto wake yataingia kiwi. Ayabu 17:5

He who denounces his friends for a prey, Even the eyes of his children shall fail.

Amenifanya niwe simo kwa watu; Nimekuwa mwenye kuchukiwa kwa wazi. Ayabu 17:6

"But he has made me a byword of the people. They spit in my face.

Jicho langu nalo limekuwa giza kwa sababu ya majonzi, Na via vyangu vyote vimekuwa kama kivuli. Ayabu 17:7

My eye also is dim by reason of sorrow. All my members are as a shadow.

Walekevu watayastaajabia hayo, Na asiye na hatia atajiamsha juu ya mpotovu. Ayabu 17:8

Upright men shall be astonished at this. The innocent shall stir up himself against the godless.

Lakini mwenye haki ataishika njia yake, Naye mwenye mikono safi atazidi kupata nguvu. Ayabu 17:9

Yet shall the righteous hold on his way. He who has clean hands shall grow stronger and stronger.

Lakini rudini; ninyi nyote, njoni sasa; Wala sitampata mtu mwenye hekima kati yenu. Ayabu 17:10

But as for you all, come on now again; I shall not find a wise man among you.

Siku zangu zimepita, makusudi yangu yamevunjika, Hata hayo niliyo nayo moyoni mwangu. Ayabu 17:11

My days are past, my plans are broken off, As are the thoughts of my heart.

Wabadili usiku kuwa mchana; Wasema, Mwanga u karibu kwa sababu ya giza. Ayabu 17:12

They change the night into day, Saying 'The light is near' in the presence of darkness.

Nikitazamia kuzimu kuwa nyumba yangu; Nikitandika malazi yangu gizani; Ayabu 17:13

If I look for Sheol as my house, If I have spread my couch in the darkness,

Ikiwa nimeuita uharibifu, Wewe u baba yangu; Na kuliambia buu, Wewe u mama yangu, na umbu langu; Ayabu 17:14

If I have said to corruption, 'You are my father;' To the worm, 'My mother,' and 'my sister;'

Basi, tumaini langu li wapi? Na tumaini langu, ni nani atakayeliona? Ayabu 17:15

Where then is my hope? As for my hope, who shall see it?

Litashuka kwenye makomeo ya kuzimu, Itakapokuwapo raha mavumbini. Ayabu 17:16

Shall it go down with me to the gates of Sheol, Or descend together into the dust?"