Ayabu 29 Swahili & English
Listen/Download AudioAyabu 29 (Swahili) | Job 29 (English) |
---|---|
Kisha Ayubu akaendelea na mithali yake, na kusema, Ayabu 29:1 |
Job again took up his parable, and said, |
Laiti ningekuwa kama nilivyokuwa katika miezi ya kale, Kama katika siku hizo Mungu aliponilinda; Ayabu 29:2 |
"Oh that I were as in the months of old, As in the days when God watched over me; |
Hapo taa yake ilipomulika juu yangu kichwani, Nami nilitembea gizani kwa njia ya mwanga wake; Ayabu 29:3 |
When his lamp shone on my head, And by his light I walked through darkness; |
Kama nilivyokuwa katika siku zangu za kukomaa, Hapo siri ya Mungu ilipokuwa hemani mwangu; Ayabu 29:4 |
As I was in the ripeness of my days, When the friendship of God was in my tent; |
Wakati Mwenyezi alipokuwa akali pamoja nami, Nao watoto wangu walipokuwa wakinizunguka; Ayabu 29:5 |
When the Almighty was yet with me, And my children were around me; |
Wakati hatua zangu zilipokuwa zikioshwa kwa siagi, Nalo jabali liliponimiminia mito ya mafuta! Ayabu 29:6 |
When my steps were washed with butter, And the rock poured out streams of oil for me! |
Wakati nilipotoka kwenda mjini, hata langoni, Nilipokitengeza kiti changu katika njia kuu, Ayabu 29:7 |
When I went forth to the city gate, When I prepared my seat in the street, |
Hao vijana waliniona wakajificha, Nao wazee wakaniondokea na kusimama; Ayabu 29:8 |
The young men saw me and hid themselves, The aged rose up and stood; |
Wakuu wakanyamaa wasinene, Na kuweka mikono yao vinywani mwao; Ayabu 29:9 |
The princes refrained from talking, And laid their hand on their mouth; |
Sauti yao masheki ilinyamaa, Na ndimi zao zilishikamana na makaakaa yao. Ayabu 29:10 |
The voice of the nobles was hushed, And their tongue stuck to the roof of their mouth. |
Maana sikio liliponisikia, ndipo likanibarikia; Na jicho liliponiona, likanishuhudia. Ayabu 29:11 |
For when the ear heard me, then it blessed me; And when the eye saw me, it commended me: |
Kwa sababu nalimwokoa maskini aliyenililia; Yatima naye, na yule asiyekuwa na mtu wa kumsaidia. Ayabu 29:12 |
Because I delivered the poor who cried, And the fatherless also, who had none to help him. |
Baraka yake yeye aliyekuwa karibu na kupotea ilinijia; Nikaufanya moyo wa mjane kuimba kwa furaha. Ayabu 29:13 |
The blessing of him who was ready to perish came on me, And I caused the widow's heart to sing for joy. |
Nalijivika haki, ikanifunika, Adili yangu ilikuwa kama joho na kilemba. Ayabu 29:14 |
I put on righteousness, and it clothed me. My justice was as a robe and a diadem. |
Nalikuwa macho kwa kipofu, Nalikuwa miguu kwa aliyechechemea. Ayabu 29:15 |
I was eyes to the blind, And feet to the lame. |
Nalikuwa baba kwa mhitaji, Na daawa ya mtu nisiyemjua naliichunguza. Ayabu 29:16 |
I was a father to the needy. The cause of him who I didn't know, I searched out. |
Nami nilizivunja taya za wasio haki, Na kumpokonya mawindo katika meno yake. Ayabu 29:17 |
I broke the jaws of the unrighteous, And plucked the prey out of his teeth. |
Ndipo niliposema, Nitakufa ndani ya kioto changu, Nami nitaziongeza siku zangu kama mchanga; Ayabu 29:18 |
Then I said, 'I shall die in my own house, I shall number my days as the sand. |
Shina langu limeenea hata kufika majini, Na umande hukaa usiku kucha katika matawi yangu; Ayabu 29:19 |
My root is spread out to the waters, The dew lies all night on my branch; |
Utukufu wangu utakuwa mpya kwangu, Na uta wangu hurejezwa upya mkononi mwangu. Ayabu 29:20 |
My glory is fresh in me, My bow is renewed in my hand.' |
Watu walitega masikio kunisikiliza, na kungoja, Wakanyamaa kimya wapate sikia mashauri yangu. Ayabu 29:21 |
"Men listened to me, waited, And kept silence for my counsel. |
Hawakunena tena baada ya kusikia maneno yangu; Matamko yangu yakadondoka juu yao. Ayabu 29:22 |
After my words they didn't speak again; My speech fell on them. |
Walikuwa wakiningojea kama kungojea mvua; Wakafunua vinywa vyao sana kama mvua ya masika. Ayabu 29:23 |
They waited for me as for the rain. Their mouths drank as with the spring rain. |
Walipokata tamaa nikacheka nao; Na mwanga wa uso wangu hawakuuangusha. Ayabu 29:24 |
I smiled on them when they had no confidence. They didn't reject the light of my face. |
Niliwachagulia njia, nikakaa kama mkuu wao. Nikakaa kama mfalme katika jeshi la askari, Mfano wa awafarijiye hao waombolezao. Ayabu 29:25 |
I chose out their way, and sat as chief. I lived as a king in the army, As one who comforts the mourners. |