Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,
Then Job answered,
Hata leo mashitaka yangu yana uchungu; Pigo langu ni zito zaidi ya kuugua kwangu.
"Even today is my complaint rebellious. His hand is heavy in spite of my groaning.
Laiti ningejua mahali niwezapo kumwona, Nifike hata hapo anapokaa!
Oh that I knew where I might find him! That I might come even to his seat!
Ningeiweka daawa yangu mbele yake, Na kukijaza kinywa changu hoja.
I would set my cause in order before him, And fill my mouth with arguments.
Ningeyajua maneno atakayonijibu, Na kuelewa na hayo atakayoniambia.
I would know the words which he would answer me, And understand what he would tell me.
Je! Angeshindana nami kwa ukuu wa uwezo wake? La, lakini angenisikiliza.
Would he contend with me in the greatness of his power? No, but he would listen to me.
Hapo walekevu wangepata kuhojiana naye; Basi hivyo ningeachiliwa na mwamuzi wangu milele.
There the upright might reason with him, So I should be delivered forever from my judge.
Tazama, naenda mbele, wala hayuko; Narudi nyuma, lakini siwezi kumwona;
"If I go east, he is not there; If west, I can't find him;
Na mkono wa kushoto, afanyapo kazi, lakini siwezi kumwona; Hujificha upande wa kuume, hata nisimwone.
He works to the north, but I can't see him; He turns south, but I can't catch a glimpse of him.
Lakini yeye aijua njia niendeayo; Akisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu.
But he knows the way that I take. When he has tried me, I shall come forth like gold.
Mguu wangu umeshikamana sana na hatua zake; Njia yake nimeishika, wala sikukengeuka.
My foot has held fast to his steps. His way have I kept, and not turned aside.
Sikurudi nyuma kuiacha amri ya midomo yake; Nimeyatunza maneno ya kinywa chake zaidi ya riziki yangu,
I haven't gone back from the commandment of his lips. I have treasured up the words of his mouth more than my necessary food.
Lakini yeye ni mmoja, ni nani awezaye kumgeuza? Tena nafsi yake ilitakalo, ndilo afanyalo.
But he stands alone, and who can oppose him? What his soul desires, even that he does.
Kwani yeye hulitimiliza hilo nililoamuriwa; Tena mambo mengi kama hayo ya pamoja naye.
For he performs that which is appointed for me. Many such things are with him.
Kwa hiyo naona taabu mbele ya uso wake; Nitakapofikiri, namwogopa.
Therefore I am terrified at his presence. When I consider, I am afraid of him.
Kwani Mungu ameufanya moyo wangu kuzimia, Naye Mwenyezi amenitaabisha;
For God has made my heart faint. The Almighty has terrified me.
Maana sikufadhaishwa kwa sababu ya giza, Wala kwa sababu giza kuu limenifunika uso.
Because I was not cut off before the darkness, Neither did he cover the thick darkness from my face.