Basi hao watu watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa sababu alikuwa mwenye haki machoni pake mwenyewe.
So these three men ceased to answer Job, because he was righteous in his own eyes.
Ndipo zikawaka hasira za huyo Elihu mwana wa Barakeli, Mbuzi, katika jamaa ya Ramu, juu ya Ayubu, kwa sababu alikuwa amejipa haki mwenyewe zaidi ya Mungu.
Then the wrath of Elihu the son of Barachel, the Buzite, of the family of Ram, was kindled against Job. His wrath was kindled because he justified himself rather than God.
Tena hasira zake ziliwaka juu ya hao rafiki zake watatu kwa sababu hawakupata jawabu, lakini wamemhukumia Ayubu makosa.
Also his wrath was kindled against his three friends, because they had found no answer, and yet had condemned Job.
Basi huyo Elihu alikuwa anangoja ili anene na Ayubu, kwa sababu hao wengine walikuwa wazee kuliko yeye.
Now Elihu had waited to speak to Job, because they were elder than he.
Hata Elihu alipoona kuwa hapana jawabu katika vinywa vya watu hao watatu, hasira zake ziliwaka.
When Elihu saw that there was no answer in the mouth of these three men, his wrath was kindled.
Basi Elihu mwana wa Barakeli, Mbuzi, akajibu, na kusema, Mimi ni kijana, na ninyi ni wazee sana; Kwa hiyo nilijizuia, nisithubutu kuwaonyesha nionavyo.
Elihu the son of Barachel the Buzite answered, "I am young, and you are very old; Therefore I held back, and didn't dare show you my opinion.
Nilisema, Yafaa siku ziseme, Na wingi wa miaka ufundishe hekima.
I said, 'Days should speak, And multitude of years should teach wisdom.'
Lakini imo roho ndani ya mwanadamu, Na pumzi za Mwenyezi huwapa akili.
But there is a spirit in man, And the breath of the Almighty gives them understanding.
Sio wakuu walio wenye akili, Wala sio wazee watambuao hukumu.
It is not the great who are wise, Nor the aged who understand justice.
Basi nilisema, Nisikilizeni mimi; Mimi nami nitawaonyesha nionavyo.
Therefore I said, 'Listen to me; I also will show my opinion.'
Tazama, niliyangojea maneno yenu, Nilizisikiliza nisikie hoja zenu, Hapo mlipokitafuta mtakalonena.
"Behold, I waited for your words, And I listened for your reasoning, While you searched out what to say.
Naam, niliwasikiza ninyi, Na tazama, hapana mmoja aliyemshinda Ayubu, Wala kumjibu maneno yake, kati yenu.
Yes, I gave you my full attention, But there was no one who convinced Job, Or who answered his words, among you.
Jitunzeni msiseme, Sisi tumepata hekima; Mungu yumkini akamshinda, si mtu;
Beware lest you say, 'We have found wisdom, God may refute him, not man:'
Kwa kuwa yeye hajayaelekeza maneno yake kwangu; Wala sitamjibu mimi kwa maneno yenu.
For he has not directed his words against me; Neither will I answer him with your speeches.
Wameshangaa, hawajibu tena; Hawana neno la kusema.
"They are amazed. They answer no more. They don't have a word to say.
Na mimi, je! Ningoje, kwa sababu hawaneni, Kwa sababu wasimama kimya, wala wasijibu tena;
Shall I wait, because they don't speak, Because they stand still, and answer no more?
Mimi nami nitajibu sehemu yangu, Mimi nami nitaonyesha nionavyo.
I also will answer my part, And I also will show my opinion.
Kwa kuwa nimejaa maneno; Roho iliyo ndani yangu hunihimiza.
For I am full of words. The spirit within me constrains me.
Tazama, tumbo langu ni kama divai iliyozibwa; Kama viriba vipya li karibu na kupasuka.
Behold, my breast is as wine which has no vent; Like new wineskins it is ready to burst.
Nitanena, ili nipate kutulia; Nitafunua midomo yangu na kujibu.
I will speak, that I may be refreshed. I will open my lips and answer.
Tafadhali, nisiupendelee uso wa mtu; Wala sitajipendekeza kwa mtu ye yote.
Please don't let me respect any man's person, Neither will I give flattering titles to any man.
Kwani mimi sijui kujipendekeza; Au Muumba wangu angeniondoa kwa upesi.
For I don't know how to give flattering titles; Or else my Maker would soon take me away.