Hesabu 33 Swahili & English

Listen/Download Audio
Hesabu 33 (Swahili) Numbers 33 (English)

Hizi ndizo safari za wana wa Israeli, hapo walipotoka nchi ya Misri kwa jeshi zao chini ya mkono wa Musa na Haruni. Hesabu 33:1

These are the journeys of the children of Israel, when they went forth out of the land of Egypt by their hosts under the hand of Moses and Aaron.

Musa akaandika jinsi walivyotoka katika safari zao, kwa amri ya Bwana; na hizi ndizo safari zao kama kutoka kwao kulivyokuwa. Hesabu 33:2

Moses wrote their goings out according to their journeys by the commandment of Yahweh: and these are their journeys according to their goings out.

Wakasafiri kutoka Ramesesi mwezi wa kwanza, siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza; siku ya pili baada ya Pasaka, wana wa Israeli wakatoka kwa mkono wa nguvu mbele ya macho ya Wamisri wote, Hesabu 33:3

They traveled from Rameses in the first month, on the fifteenth day of the first month; on the next day after the Passover the children of Israel went out with a high hand in the sight of all the Egyptians,

hapo Wamisri walipokuwa wanazika wazaliwa wa kwanza wao wote, Bwana aliokuwa amewapiga kati yao; Bwana akafanya hukumu juu ya miungu yao nayo. Hesabu 33:4

while the Egyptians were burying all their firstborn, whom Yahweh had struck among them: on their gods also Yahweh executed judgments.

Wana wa Israeli wakasafiri kutoka Ramesesi, wakapanga katika Sukothi. Hesabu 33:5

The children of Israel traveled from Rameses, and encamped in Succoth.

Kisha wakasafiri kutoka Sukothi, wakapanga Ethamu, palipo katika mwisho wa nyika. Hesabu 33:6

They traveled from Succoth, and encamped in Etham, which is in the edge of the wilderness.

Wakasafiri kutoka Ethamu, na kurudi nyuma hata Pi-hahirothi palipokabili Baal-sefoni; wakapanga mbele ya Migdoli. Hesabu 33:7

They traveled from Etham, and turned back to Pihahiroth, which is before Baal Zephon: and they encamped before Migdol.

Wakasafiri kutoka hapo mbele ya Hahirothi, wakapita katikati ya bahari na kuingia jangwani; kisha wakaenda safari ya siku tatu katika nyika ya Ethamu, wakapanga Mara. Hesabu 33:8

They traveled from before Hahiroth, and passed through the midst of the sea into the wilderness: and they went three days' journey in the wilderness of Etham, and encamped in Marah.

Wakasafiri kutoka Mara, wakafikilia Elimu; huko Elimu palikuwa na chemchemi za maji kumi na mbili, na mitende sabini; nao wakapanga hapo. Hesabu 33:9

They traveled from Marah, and came to Elim: and in Elim were twelve springs of water, and seventy palm trees; and they encamped there.

Wakasafiri kutoka Elimu wakapanga karibu na Bahari ya Shamu. Hesabu 33:10

They traveled from Elim, and encamped by the Red Sea.

Wakasafiri kutoka Bahari ya Shamu, wakapanga katika nyika ya Sini. Hesabu 33:11

They traveled from the Red Sea, and encamped in the wilderness of Sin.

Wakasafiri kutoka nyika ya Sini, wakapanga Dofka. Hesabu 33:12

They traveled from the wilderness of Sin, and encamped in Dophkah.

Wakasafiri kutoka Dofka, wakapanga Alushi. Hesabu 33:13

They traveled from Dophkah, and encamped in Alush.

Wakasafiri kutoka Alushi, wakapanga Refidimu, ambapo hapakuwa na maji ya watu kunywa. Hesabu 33:14

They traveled from Alush, and encamped in Rephidim, where was no water for the people to drink.

Wakasafiri kutoka Refidimu, wakapanga katika nyika ya Sinai. Hesabu 33:15

They traveled from Rephidim, and encamped in the wilderness of Sinai.

Wakasafiri kutoka nyika ya Sinai, wakapanga Kibroth-hataava. Hesabu 33:16

They traveled from the wilderness of Sinai, and encamped in Kibroth-hattaavah.

Wakasafiri kutoka Kibroth-hataava, wakapanga Haserothi. Hesabu 33:17

They traveled from Kibroth-hattaavah, and encamped in Hazeroth.

Wakasafiri kutoka Haserothi, wakapanga Rithma. Hesabu 33:18

They traveled from Hazeroth, and encamped in Rithmah.

Wakasafiri kutoka Rithma, wakapanga Rimon-peresi. Hesabu 33:19

They traveled from Rithmah, and encamped in Rimmon Perez.

Wakasafiri kutoka Rimon-peresi, wakapanga Libna. Hesabu 33:20

They traveled from Rimmon Perez, and encamped in Libnah.

Wakasafiri kutoka Libna, wakapanga Risa. Hesabu 33:21

They traveled from Libnah, and encamped in Rissah.

Wakasafiri kutoka Risa, wakapanga Keheletha. Hesabu 33:22

They traveled from Rissah, and encamped in Kehelathah.

Wakasafiri kutoka Keheletha, wakapanga katika mlima wa Sheferi Hesabu 33:23

They traveled from Kehelathah, and encamped in Mount Shepher.

Wakasafiri kutoka huo mlima wa Sheferi, wakapanga Harada. Hesabu 33:24

They traveled from Mount Shepher, and encamped in Haradah.

Wakasafiri kutoka Harada, wakapanga Makelothi. Hesabu 33:25

They traveled from Haradah, and encamped in Makheloth.

Wakasafiri kutoka Makelothi, wakapanga Tahathi. Hesabu 33:26

They traveled from Makheloth, and encamped in Tahath.

Wakasafiri kutoka Tahathi wakapanga Tera. Hesabu 33:27

They traveled from Tahath, and encamped in Terah.

Wakasafiri kutoka Tera, wakapanga Mithka. Hesabu 33:28

They traveled from Terah, and encamped in Mithkah.

Wakasafiri kutoka Mithka, wakapanga Hashmona. Hesabu 33:29

They traveled from Mithkah, and encamped in Hashmonah.

Wakasafiri kutoka Hashmona, wakapanga Moserothi. Hesabu 33:30

They traveled from Hashmonah, and encamped in Moseroth.

Wakasafiri kutoka Moserothi, wakapanga Bene-yakani. Hesabu 33:31

They traveled from Moseroth, and encamped in Bene Jaakan.

Wakasafiri kutoka Bene-yakani, wakapanga Hor-hagidgadi. Hesabu 33:32

They traveled from Bene Jaakan, and encamped in Hor Haggidgad.

Wakasafiri kutoka Hor-hagidgadi, wakapanga Yotbatha. Hesabu 33:33

They traveled from Hor Haggidgad, and encamped in Jotbathah.

Wakasafiri kutoka Yotbatha, wakapanga Abrona. Hesabu 33:34

They traveled from Jotbathah, and encamped in Abronah.

Wakasafiri kutoka Abrona, wakapanga Esion-geberi. Hesabu 33:35

They traveled from Abronah, and encamped in Ezion Geber.

Wakasafiri kutoka Esion-geberi, wakapanga katika nyika ya Sini (ni Kadeshi). Hesabu 33:36

They traveled from Ezion Geber, and encamped in the wilderness of Zin (the same is Kadesh).

Wakasafiri kutoka Kadeshi wakapanga katika mlima wa Hori, katika mpaka wa nchi ya Edomu, Hesabu 33:37

They traveled from Kadesh, and encamped in Mount Hor, in the edge of the land of Edom.

Haruni akakwea mlima wa Hori, kwa amri ya Bwana, akafa hapo, katika mwaka wa arobaini baada ya wana wa Israeli kutoka katika nchi ya Misri, mwezi wa tano, siku ya kwanza ya mwezi. Hesabu 33:38

Aaron the priest went up into Mount Hor at the commandment of Yahweh, and died there, in the fortieth year after the children of Israel were come out of the land of Egypt, in the fifth month, on the first day of the month.

Naye Haruni alikuwa mtu wa umri wa miaka mia na ishirini na mitatu hapo alipokufa katika mlima wa Hori. Hesabu 33:39

Aaron was one hundred twenty-three years old when he died in Mount Hor.

Ndipo Mkanaani, mfalme wa Aradi, aliyekaa pande za Negebu katika nchi ya Kanaani akasikia habari za kuja kwao wana wa Israeli. Hesabu 33:40

The Canaanite, the king of Arad, who lived in the South in the land of Canaan, heard of the coming of the children of Israel.

Nao wakasafiri kutoka mlima wa Hori, wakapanga Salmona. Hesabu 33:41

They traveled from Mount Hor, and encamped in Zalmonah.

Wakasafiri kutoka Salmona, wakapanga Punoni. Hesabu 33:42

They traveled from Zalmonah, and encamped in Punon.

Wakasafiri kutoka Punoni, wakapanga Obothi. Hesabu 33:43

They traveled from Punon, and encamped in Oboth.

Wakasafiri kutoka Obothi, wakapanga Iye-abarimu, katika mpaka wa Moabu. Hesabu 33:44

They traveled from Oboth, and encamped in Iye-abarim, in the border of Moab.

Wakasafiri kutoka Iye-abarimu, wakapanga Dibon-gadi. Hesabu 33:45

They traveled from Iyim, and encamped in Dibon-gad.

Wakasafiri kutoka Dibon-gadi, wakapanga Almon-diblathaimu. Hesabu 33:46

They traveled from Dibon-gad, and encamped in Almon Diblathaim.

Wakasafiri kutoka Almon-diblathaimu, wakapanga katika milima ya Abarimu, kukabili Nebo. Hesabu 33:47

They traveled from Almon Diblathaim, and encamped in the mountains of Abarim, before Nebo.

Wakasafiri kutoka hiyo milima ya Abarimu, wakapanga katika nchi tambarare za Moabu, karibu na mto wa Yordani, hapo Yeriko. Hesabu 33:48

They traveled from the mountains of Abarim, and encamped in the plains of Moab by the Jordan at Jericho.

Wakapanga karibu na Yordani, tangu Beth-yeshimothi hata kufikilia Abel-shitimu katika nchi tambarare za Moabu. Hesabu 33:49

They encamped by the Jordan, from Beth-jeshimoth even to Abel Shittim in the plains of Moab.

Kisha Bwana akanena na Musa hapo katika nchi tambarare za Moabu, karibu na Yordani, hapo Yeriko, na kumwambia, Hesabu 33:50

Yahweh spoke to Moses in the plains of Moab by the Jordan at Jericho, saying,

Nena na wana wa Israeli, uwaambie, Mtakapovuka mto wa Yordani na kuingia nchi ya Kanaani, Hesabu 33:51

Speak to the children of Israel, and tell them, When you pass over the Jordan into the land of Canaan,

ndipo mtakapowafukuza wenyeji wote wa hiyo nchi mbele yenu, nanyi mtayaharibu mawe yao yote yenye kuchorwa sanamu, na kuziharibu sanamu zao zote za kusubu, kuvunja-vunja mahali pao pote palipoinuka; Hesabu 33:52

then you shall drive out all the inhabitants of the land from before you, and destroy all their figured [stones], and destroy all their molten images, and demolish all their high places:

nanyi mtaishika hiyo nchi kuimiliki na kuketi humo; kwa kuwa mimi nimewapa ninyi hiyo nchi ili mwimiliki. Hesabu 33:53

and you shall take possession of the land, and dwell therein; for to you have I given the land to possess it.

Nanyi mtairithi nchi kwa kufanya kura, kama jamaa zenu zilivyo; hao walio wengi mtawapa urithi zaidi, na hao waliopunguka utawapa kama kupunguka kwao; mahali po pote kura itakapomwangukia mtu ye yote, mahali hapo ni pake; mtarithi kama kabila za baba zenu zilivyo. Hesabu 33:54

You shall inherit the land by lot according to your families; to the more you shall give the more inheritance, and to the fewer you shall give the less inheritance: wherever the lot falls to any man, that shall be his; according to the tribes of your fathers shall you inherit.

Lakini kama hamtaki kuwafukuza wenyeji wa nchi watoke mbele yenu; ndipo hao ambao mtakaowasaza watakuwa kama sindano machoni mwenu, na kama miiba ubavuni mwenu, nao watawasumbua katika hiyo nchi ambayo mwakaa. Hesabu 33:55

But if you will not drive out the inhabitants of the land from before you, then shall those who you let remain of them be as pricks in your eyes, and as thorns in your sides, and they shall vex you in the land in which you dwell.

Kisha itakuwa, kama nilivyoazimia kuwatenda wao, ndivyo nitakavyowatenda ninyi. Hesabu 33:56

It shall happen that as I thought to do to them, so will I do to you.