Hesabu 1 Swahili & English

Listen/Download Audio
Hesabu 1 (Swahili) Numbers 1 (English)

Bwana akanena na Musa katika bara ya Sinai, hemani mwa kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya kutoka kwao nchi ya Misri, akamwambia, Hesabu 1:1

Yahweh spoke to Moses in the wilderness of Sinai, in the Tent of Meeting, on the first day of the second month, in the second year after they had come out of the land of Egypt, saying,

Fanyeni hesabu ya mkutano wote wa wana wa Israeli, kwa kuandama jamaa zao, na nyumba za baba zao, kama hesabu ya majina ilivyo, kila mtu mume kichwa kwa kichwa; Hesabu 1:2

"Take a census of all the congregation of the children of Israel, by their families, by their fathers' houses, according to the number of the names, every male, one by one;

tangu mwenye miaka ishirini umri wake, na zaidi, wote wawezao kutoka kwenenda vitani katika Israeli; wewe na Haruni mtawahesabu kwa kuandama majeshi yao. Hesabu 1:3

from twenty years old and upward, all who are able to go out to war in Israel. You and Aaron shall number them by their divisions.

Tena mtu mume mmoja wa kila kabila atakuwa pamoja nanyi; kila mmoja aliye kichwa cha nyumba ya baba zake. Hesabu 1:4

With you there shall be a man of every tribe; everyone head of his fathers' house.

Na majina ya hao waume watakaosimama pamoja nanyi ni haya; Wa Reubeni; Elisuri mwana wa Shedeuri. Hesabu 1:5

These are the names of the men who shall stand with you: Of Reuben: Elizur the son of Shedeur.

Wa Simeoni; Shelumieli mwana wa Suri-shadai. Hesabu 1:6

Of Simeon: Shelumiel the son of Zurishaddai.

Wa Yuda; Nashoni mwana wa Aminadabu. Hesabu 1:7

Of Judah: Nahshon the son of Amminadab.

Wa Isakari; Nethaneli mwana wa Suari. Hesabu 1:8

Of Issachar: Nethanel the son of Zuar.

Wa Zabuloni; Eliabu mwana wa Heloni. Hesabu 1:9

Of Zebulun: Eliab the son of Helon.

Katika wana wa Yusufu; wa Efraimu, Elishama mwana wa Amihudi; na wa Manase; Gamalieli mwana wa Pedasuri. Hesabu 1:10

Of the children of Joseph: Of Ephraim: Elishama the son of Ammihud. Of Manasseh: Gamaliel the son of Pedahzur.

Wa Benyamini Abidani mwana wa Gideoni. Hesabu 1:11

Of Benjamin: Abidan the son of Gideoni.

Wa Dani; Ahiezeri mwana wa Amishadai. Hesabu 1:12

Of Dan: Ahiezer the son of Ammishaddai.

Wa Asheri; Pagieli mwana wa Okirani. Hesabu 1:13

Of Asher: Pagiel the son of Ochran.

Wa Gadi; Eliasafu mwana wa Deueli. Hesabu 1:14

Of Gad: Eliasaph the son of Deuel.

Wa Naftali; Ahira mwana wa Enani. Hesabu 1:15

Of Naphtali: Ahira the son of Enan."

Hao ndio walioitwa wa mkutano, wakuu wa kabila za baba zao; nao ndio vichwa vya wale maelfu ya Israeli. Hesabu 1:16

These are those who were called of the congregation, the princes of the tribes of their fathers; they were the heads of the thousands of Israel.

Basi Musa na Haruni wakawatwaa hao watu waume waliotajwa majina yao; Hesabu 1:17

Moses and Aaron took these men who are mentioned by name.

nao waliukutanisha mkutano mzima, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, nao wakaonyesha ukoo wa vizazi vyao kwa kuandama jamaa zao, kwa nyumba za baba zao, kama hesabu ya majina, tangu umri wa miaka ishirini na zaidi, kichwa kwa kichwa. Hesabu 1:18

They assembled all the congregation together on the first day of the second month; and they declared their ancestry by their families, by their fathers' houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, one by one.

Kama Bwana alivyomwagiza Musa, ndivyo alivyowahesabu huko katika bara ya Sinai. Hesabu 1:19

As Yahweh commanded Moses, so he numbered them in the wilderness of Sinai.

Na wana wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa Israeli, vizazi vyao, kwa kuandama jamaa zao, na nyumba za baba zao, kama hesabu ya majina, kichwa kwa kichwa, kila mtu mume tangu umri wa miaka ishirini na zaidi wote walioweza kwenda vitani; Hesabu 1:20

The children of Reuben, Israel's firstborn, their generations, by their families, by their fathers' houses, according to the number of the names, one by one, every male from twenty years old and upward, all who were able to go out to war;

wale waliohesabiwa katika kabila ya Reubeni, walikuwa watu arobaini na sita elfu na mia tano (46,500). Hesabu 1:21

those who were numbered of them, of the tribe of Reuben, were forty-six thousand five hundred.

Katika wana wa Simeoni, vizazi vyao, kwa kuandama jamaa zao, na nyumba za baba zao, wale waliohesabiwa kama hesabu ya majina, kichwa kwa kichwa, kila mume tangu umri wa miaka ishirini na zaidi, wote walioweza kwenda vitani; Hesabu 1:22

Of the children of Simeon, their generations, by their families, by their fathers' houses, those who were numbered of it, according to the number of the names, one by one, every male from twenty years old and upward, all who were able to go out to war;

wale waliohesabiwa katika kabila ya Simeoni, walikuwa watu hamsini na kenda elfu na mia tatu (59,300). Hesabu 1:23

those who were numbered of them, of the tribe of Simeon, were fifty-nine thousand three hundred.

Katika wana wa Gadi, kwa kuandama vizazi vyao, jamaa zao, na nyumba za baba zao, kama hesabu ya majina, tangu umri wa miaka ishirini na zaidi, wote walioweza kwenda vitani; Hesabu 1:24

Of the children of Gad, their generations, by their families, by their fathers' houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war;

wale waliohesabiwa katika kabila ya Gadi, walikuwa watu arobaini na tano elfu na mia sita na hamsini (45,650). Hesabu 1:25

those who were numbered of them, of the tribe of Gad, were forty-five thousand six hundred fifty.

Katika wana wa Yuda, vizazi vyao, kwa kuandama jamaa zao, na nyumba za baba zao, kama hesabu ya majina, tangu umri wa miaka ishirini na zaidi, wote walioweza kwenda vitani; Hesabu 1:26

Of the children of Judah, their generations, by their families, by their fathers' houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war;

wale waliohesabiwa katika kabila ya Yuda, walikuwa watu sabini na nne elfu na mia sita (74,600). Hesabu 1:27

those who were numbered of them, of the tribe of Judah, were sixty-four thousand six hundred.

Katika wana wa Isakari, vizazi vyao, kwa kuandama jamaa zao, na nyumba za baba zao, kwa hesabu ya majina, tangu umri wa miaka ishirini na zaidi, wote walioweza kwenda vitani; Hesabu 1:28

Of the children of Issachar, their generations, by their families, by their fathers' houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war;

wale waliohesabiwa katika kabila ya Isakari, walikuwa watu hamsini na nne elfu na mia nne (54,400). Hesabu 1:29

those who were numbered of them, of the tribe of Issachar, were fifty-four thousand four hundred.

Katika wana wa Zabuloni, vizazi vyao, kwa kuandama jamaa zao, na nyumba za baba zao, kama hesabu ya majina, tangu umri wa miaka ishirini na zaidi, wote walioweza kwenda vitani; Hesabu 1:30

Of the children of Zebulun, their generations, by their families, by their fathers' houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war;

wale waliohesabiwa katika kabila ya Zabuloni, walikuwa watu hamsini na saba elfu na mia nne (57,400). Hesabu 1:31

those who were numbered of them, of the tribe of Zebulun, were fifty-seven thousand four hundred.

Katika wana wa Yusufu, maana katika wana wa Efraimu, vizazi vyao kwa kuandama jamaa zao, na nyumba za baba zao, kama hesabu ya majina, tangu umri wa miaka ishirini na zaidi, wote walioweza kwenda vitani, Hesabu 1:32

Of the children of Joseph, of the children of Ephraim, their generations, by thir families, by their fathers' houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war;

wale waliohesabiwa katika kabila ya Efraimu, walikuwa watu arobaini elfu na mia tano (40,500). Hesabu 1:33

those who were numbered of them, of the tribe of Ephraim, were forty thousand five hundred.

Katika wana wa Manase, vizazi vyao, kwa kuandama jamaa zao, na nyumba za baba zao, kama hesabu ya majina, tangu umri wa miaka ishirini na zaidi, wote walioweza kwenda vitani; Hesabu 1:34

Of the children of Manasseh, their generations, by their families, by their fathers' houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war;

wale waliohesabiwa katika kabila ya Manase, walikuwa watu thelathini na mbili elfu na mia mbili (32,200). Hesabu 1:35

those who were numbered of them, of the tribe of Manasseh, were thirty-two thousand two hundred.

Katika wana wa Benyamini, vizazi vyao, kwa kuandama jamaa zao, na nyumba za baba zao, kama hesabu ya majina, tangu umri wa miaka ishirini na zaidi, wote walioweza kwenda vitani; Hesabu 1:36

Of the children of Benjamin, their generations, by their families, by their fathers' houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war;

wale waliohesabiwa katika kabila ya Benyamini, walikuwa watu thelathini na tano elfu na mia nne (35,400). Hesabu 1:37

those who were numbered of them, of the tribe of Benjamin, were thirty-five thousand four hundred.

Katika wana wa Dani, vizazi vyao, kwa kuandama jamaa zao, na nyumba za baba zao, kama hesabu ya majina, tangu umri wa miaka ishirini na zaidi, wote walioweza kwenda vitani; Hesabu 1:38

Of the children of Dan, their generations, by their families, by their fathers' houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go forth to war;

wale waliohesabiwa katika kabila ya Dani, walikuwa watu sitini na mbili elfu na mia saba (62,700). Hesabu 1:39

those who were numbered of them, of the tribe of Dan, were sixty-two thousand seven hundred.

Katika wana wa Asheri, vizazi vyao, kwa kuandama jamaa zao, na nyumba za baba zao, kama hesabu ya majina, tangu umri wa miaka ishirini na zaidi, wote walioweza kwenda vitani; Hesabu 1:40

Of the children of Asher, their generations, by their families, by their fathers' houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go forth to war;

wale waliohesabiwa katika kabila ya Asheri, walikuwa watu arobaini na moja elfu na mia tano (41,500). Hesabu 1:41

those who were numbered of them, of the tribe of Asher, were forty-one thousand five hundred.

Katika wana wa Naftali, vizazi vyao, kwa kuandama jamaa zao, na nyumba za baba zao, kama hesabu ya majina, tangu umri wa miaka ishirini na zaidi, wote walioweza kwenda vitani; Hesabu 1:42

Of the children of Naphtali, their generations, by their families, by their fathers' houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go forth to war;

wale waliohesabiwa katika kabila ya Naftali, walikuwa watu hamsini na tatu elfu na mia nne (53,400). Hesabu 1:43

those who were numbered of them, of the tribe of Naphtali, were fifty-three thousand four hundred.

Hao ndio waliohesabiwa, ambao Musa na Haruni na wale wakuu wa Israeli watu kumi na wawili waliwahesabu; walikuwa kila mmoja kwa ajili ya nyumba ya baba zake. Hesabu 1:44

These are those who were numbered, whom Moses and Aaron numbered, and the princes of Israel, being twelve men: they were each one for his fathers' house.

Basi hao wote waliohesabiwa katika wana wa israeli kwa kuandama nyumba za baba zao tangu umri wa miaka ishirini na zaidi; wote walioweza kwenda vitani katika Israeli; Hesabu 1:45

So all those who were numbered of the children of Israel by their fathers' houses, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war in Israel;

hao wote waliohesabiwa walikuwa ni watu waume mia sita na tatu elfu na mia tano na hamsini (603,550). Hesabu 1:46

even all those who were numbered were six hundred three thousand five hundred fifty.

Lakini Walawi kwa kuiandama kabila ya baba zao hawakuhesabiwa katika watu hao. Hesabu 1:47

But the Levites after the tribe of their fathers were not numbered among them.

Kwa kuwa Bwana alinena na Musa, na kumwambia, Hesabu 1:48

For Yahweh spoke to Moses, saying,

Hiyo kabila ya Lawi tu usiihesabu, wala usiitie hesabu yao katika wana wa Israeli; Hesabu 1:49

"Only the tribe of Levi you shall not number, neither shall you take a census of them among the children of Israel;

lakini uwaweke Walawi wawe juu ya maskani ya ushahidi, na juu ya vyombo vyake vyote, na juu ya vitu vyake vyote; wao wataichukua hiyo maskani, na vyombo vyake vyote; nao wataitumikia, na kupanga hema zao kwa kuizunguka maskani pande zote. Hesabu 1:50

but appoint the Levites over the Tabernacle of the Testimony, and over all its furnishings, and over all that belongs to it. They shall carry the tabernacle, and all its furnishings; and they shall take care of it, and shall encamp around it.

Tena hapo maskani itakapokwenda mbele, Walawi wataishusha; tena hapo maskani itakaposimamishwa, Walawi wataisimamisha; na mgeni atakayekaribia atauawa. Hesabu 1:51

When the tabernacle is to move, the Levites shall take it down; and when the tabernacle is to be set up, the Levites shall set it up. The stranger who comes near shall be put to death.

Na wana wa Israeli watazipanga hema zao, kila mtu katika marago yake mwenyewe, kila mtu hapo ilipo beramu yake mwenyewe, kama majeshi yao yalivyo. Hesabu 1:52

The children of Israel shall pitch their tents, every man by his own camp, and every man by his own standard, according to their divisions.

Lakini Walawi watapanga hema zao kuizunguka maskani ya ushahidi pande zote, ili zisiwe hasira juu ya mkutano wa wana wa Israeli; kisha Walawi wataulinda ulinzi wa hiyo maskani ya ushahidi. Hesabu 1:53

But the Levites shall encamp around the Tabernacle of the Testimony, that there may be no wrath on the congregation of the children of Israel: and the Levites shall be responsible for the Tabernacle of the Testimony."

Ndivyo walivyofanya wana wa Israeli; kama yote Bwana aliyomwagiza Musa, ndivyo walivyofanya.

Hesabu 1:54

Thus the children of Israel did. According to all that Yahweh commanded Moses, so they did.