Hesabu 29 Swahili & English

Listen/Download Audio
Hesabu 29 (Swahili) Numbers 29 (English)

Tena mwezi wa saba, siku ya kwanza ya mwezi, mtakuwa na kusanyiko takatifu; hamtafanya kazi yo yote ya utumishi; ni siku ya kupiga tarumbeta kwenu. Hesabu 29:1

In the seventh month, on the first day of the month, you shall have a holy convocation; you shall do no servile work: it is a day of blowing of trumpets to you.

Nanyi mtasongeza sadaka ya kuteketezwa kuwa harufu ya kupendeza kwa Bwana; ng'ombe mume mdogo mmoja, na kondoo mume mmoja, na wana-kondoo waume wa mwaka wa kwanza wakamilifu saba; Hesabu 29:2

You shall offer a burnt offering for a sweet savor to Yahweh: one young bull, one ram, seven he-lambs a year old without blemish;

pamoja na sadaka yake ya unga, unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, sehemu ya kumi tatu kwa ng'ombe, sehemu ya kumi mbili kwa kondoo mume, Hesabu 29:3

and their meal-offering, fine flour mixed with oil, three tenth parts for the bull, two tenth parts for the ram,

na sehemu ya kumi moja kwa kila mwana-kondoo katika wale wana-kondoo saba; Hesabu 29:4

and one tenth part for every lamb of the seven lambs;

na mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi, ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu; Hesabu 29:5

and one male goat for a sin-offering, to make atonement for you;

zaidi ya hiyo sadaka ya kuteketezwa ya kuandama mwezi, na sadaka yake ya unga, na hiyo sadaka ya kuteketezwa ya sikuzote, na sadaka yake ya unga, na sadaka zake za vinywaji, kama ilivyo amri yake, kuwa harufu ya kupendeza, ni sadaka iliyosongezwa kwa Bwana kwa moto. Hesabu 29:6

besides the burnt offering of the new moon, and the meal-offering of it, and the continual burnt offering and the meal-offering of it, and their drink-offerings, according to their ordinance, for a sweet savor, an offering made by fire to Yahweh.

Tena siku ya kumi ya huo mwezi wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu; nanyi mtazitesa nafsi zenu, msifanye kazi yo yote ya utumishi Hesabu 29:7

On the tenth day of this seventh month you shall have a holy convocation; and you shall afflict your souls: you shall do no manner of work;

lakini mtamsongezea Bwana sadaka ya kuteketezwa, kuwa harufu ya kupendeza; ng'ombe mume mdogo mmoja, na kondoo mume mmoja, na wana-kondoo waume wa mwaka wa kwanza saba; watakuwa wakamilifu kwenu; Hesabu 29:8

but you shall offer a burnt offering to Yahweh for a sweet savor: one young bull, one ram, seven he-lambs a year old; they shall be to you without blemish;

pamoja na sadaka zake za unga, unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, sehemu ya kumi tatu kwa huyo ng'ombe, na sehemu ya kumi mbili kwa huyo kondoo, Hesabu 29:9

and their meal-offering, fine flour mixed with oil, three tenth parts for the bull, two tenth parts for the one ram,

na sehemu ya kumi moja kwa kila mwana-kondoo katika wale wana-kondoo saba; Hesabu 29:10

a tenth part for every lamb of the seven lambs:

na mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi; zaidi ya hiyo sadaka ya dhambi ya upatanisho, na hiyo sadaka ya kuteketezwa ya sikuzote, na sadaka yake ya unga, na sadaka zake za vinywaji. Hesabu 29:11

one male goat for a sin-offering; besides the sin-offering of atonement, and the continual burnt offering, and the meal-offering of it, and their drink-offerings.

Tena siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu; hamtafanya kazi yo yote ya utumishi, nanyi mtamfanyia Bwana sikukuu muda wa siku saba; Hesabu 29:12

On the fifteenth day of the seventh month you shall have a holy convocation; you shall do no servile work, and you shall keep a feast to Yahweh seven days:

nanyi mtasongeza sadaka ya kuteketezwa, sadaka isongezwayo kwa moto, harufu ya kupendeza kwa Bwana; ng'ombe waume wadogo kumi na watatu, na kondoo waume wawili, na wana-kondoo waume wa mwaka wa kwanza kumi na wanne; wote watakuwa wakamilifu; Hesabu 29:13

and you shall offer a burnt offering, an offering made by fire, of a sweet savor to Yahweh; thirteen young bulls, two rams, fourteen he-lambs a year old; they shall be without blemish;

pamoja na sadaka zake za unga, unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, sehemu ya kumi tatu kwa kila ng'ombe katika wale kumi na watatu na sehemu ya kumi mbili kwa kila kondoo katika hao kondoo waume wawili; Hesabu 29:14

and their meal-offering, fine flour mixed with oil, three tenth parts for every bull of the thirteen bulls, two tenth parts for each ram of the two rams,

na sehemu ya kumi moja kwa kila mwana-kondoo katika wale wana-kondoo kumi na wanne; Hesabu 29:15

and a tenth part for every lamb of the fourteen lambs;

na mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi zaidi ya hiyo sadaka ya kuteketezwa ya sikuzote, na sadaka yake ya unga, na sadaka yake ya kinywaji. Hesabu 29:16

and one male goat for a sin-offering, besides the continual burnt offering, the meal-offering of it, and the drink-offering of it.

Tena siku ya pili mtasongeza ng'ombe waume wadogo kumi na wawili, na kondoo waume wawili, na wana-kondoo waume wa mwaka wa kwanza kumi na wanne wakamilifu; Hesabu 29:17

On the second day [you shall offer] twelve young bulls, two rams, fourteen he-lambs a year old without blemish;

pamoja na sadaka yake ya unga, na sadaka zake za vinywaji kwa hao ng'ombe, na kwa hao kondoo, na kwa wale wana-kondoo, kama hesabu yao ilivyo, kwa kuandama hiyo amri; Hesabu 29:18

and their meal-offering and their drink-offerings for the bulls, for the rams, and for the lambs, according to their number, after the ordinance;

na mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi; zaidi ya hiyo sadaka ya kuteketezwa ya sikuzote, na sadaka yake ya unga, na sadaka zake za vinywaji. Hesabu 29:19

and one male goat for a sin-offering; besides the continual burnt offering, and the meal-offering of it, and their drink-offerings.

Tena siku ya tatu mtasongeza ng'ombe waume kumi na mmoja, na kondoo waume wawili, na wana-kondoo waume wa mwaka wa kwanza wakamilifu kumi na wanne; Hesabu 29:20

On the third day eleven bulls, two rams, fourteen he-lambs a year old without blemish;

pamoja na sadaka yake ya unga, na sadaka zake za vinywaji, kwa hao ng'ombe, na kwa hao kondoo, na kwa wale wana-kondoo, kama hesabu yao ilivyo, kwa kuiandama amri; Hesabu 29:21

and their meal-offering and their drink-offerings for the bulls, for the rams, and for the lambs, according to their number, after the ordinance;

na mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi; zaidi ya hiyo sadaka ya kuteketezwa ya sikuzote, na sadaka yake ya unga, na sadaka yake ya kinywaji. Hesabu 29:22

and one male goat for a sin-offering; besides the continual burnt offering, and the meal-offering of it, and the drink-offering of it.

Tena siku ya nne mtasongeza ng'ombe waume kumi, na kondoo waume wawili, na wana-kondoo waume wa mwaka wa kwanza wakamilifu kumi na wanne; Hesabu 29:23

On the fourth day ten bulls, two rams, fourteen he-lambs a year old without blemish;

na sadaka yake ya unga, na sadaka zake za vinywaji kwa hao ng'ombe, na kwa hao kondoo, na kwa wale wana-kondoo, kama hesabu yao ilivyo, kwa kuiandama amri; Hesabu 29:24

their meal-offering and their drink-offerings for the bulls, for the rams, and for the lambs, according to their number, after the ordinance;

na mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi, zaidi ya hiyo sadaka ya kuteketezwa ya sikuzote, na sadaka yake ya unga, na sadaka yake ya kinywaji. Hesabu 29:25

and one male goat for a sin-offering; besides the continual burnt offering, the meal-offering of it, and the drink-offering of it.

Tena siku ya tano mtasongeza ng'ombe waume kenda, na kondoo Waume wawili, na wana-kondoo waume wa mwaka wa kwanza wakamilifu kumi na wanne; Hesabu 29:26

On the fifth day nine bulls, two rams, fourteen he-lambs a year old without blemish;

pamoja na sadaka yake ya unga, na sadaka zake za vinywaji, kwa hao ng'ombe, na kwa hao kondoo, na kwa wale wana-kondoo, kama hesabu yao ilivyo, kwa kuiandama amri; Hesabu 29:27

and their meal-offering and their drink-offerings for the bulls, for the rams, and for the lambs, according to their number, after the ordinance;

na mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi; zaidi ya hiyo sadaka ya kuteketezwa ya siku zote, na hiyo sadaka yake ya unga na sadaka yake ya kinywaji. Hesabu 29:28

and one male goat for a sin-offering, besides the continual burnt offering, and the meal-offering of it, and the drink-offering of it.

Tena siku ya sita mtasongeza ng'ombe waume wanane, na kondoo waume wawili, na wana-kondoo waume wa mwaka wa kwanza wakamilifu kumi na wanne; Hesabu 29:29

On the sixth day eight bulls, two rams, fourteen he-lambs a year old without blemish;

pamoja na sadaka yake ya unga, na sadaka zake za vinywaji, kwa hao ng'ombe, na kwa hao kondoo, na kwa wale wana-kondoo, kama hesabu yao ilivyo, kwa kuiandama amri; Hesabu 29:30

and their meal-offering and their drink-offerings for the bulls, for the rams, and for the lambs, according to their number, after the ordinance;

na mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi; zaidi ya hiyo sadaka ya kuteketezwa ya siku zote, na hiyo sadaka yake ya unga na sadaka yake ya kinywaji. Hesabu 29:31

and one male goat for a sin-offering; besides the continual burnt offering, the meal-offering of it, and the drink-offerings of it.

Tena siku ya saba mtasongeza ng'ombe waume saba, na kondoo waume wawili, na wana-kondoo waume wa mwaka wa kwanza wakamilifu kumi na wanne; Hesabu 29:32

On the seventh day seven bulls, two rams, fourteen he-lambs a year old without blemish;

pamoja na sadaka yake ya unga, na sadaka zake za vinywaji, kwa hao ng'ombe, na kwa hao kondoo, na kwa wale wana-kondoo, kama hesabu yao ilivyo, kwa kuiandama amri; Hesabu 29:33

and their meal-offering and their drink-offerings for the bulls, for the rams, and for the lambs, according to their number, after the ordinance;

na mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi; zaidi ya hiyo sadaka ya kuteketezwa ya siku zote, na hiyo sadaka yake ya unga na sadaka yake ya kinywaji. Hesabu 29:34

and one male goat for a sin-offering; besides the continual burnt offering, the meal-offering of it, and the drink-offering of it.

Tena siku ya nane mtakuwa na kusanyiko la makini sana; hamtafanya kazi yo yote ya utumishi; Hesabu 29:35

On the eighth day you shall have a solemn assembly: you shall do no servile work;

lakini mtasongeza sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya kusongezwa kwa moto, harufu ya kupendeza kwa Bwana; ng'ombe mume mmoja, na kondoo mume mmoja, na wana-kondoo waume wa mwaka wa kwanza wakamilifu saba; Hesabu 29:36

but you shall offer a burnt offering, an offering made by fire, of a sweet savor to Yahweh: one bull, one ram, seven he-lambs a year old without blemish;

pamoja na sadaka yake ya unga, na sadaka zake za vinywaji, kwa huyo ng'ombe, na kwa huyo kondoo mume, na kwa wale wana-kondoo, kama hesabu yao ilivyo, kwa kuiandama amri; Hesabu 29:37

their meal-offering and their drink-offerings for the bull, for the ram, and for the lambs, shall be according to their number, after the ordinance:

na mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi; zaidi ya hiyo sadaka ya kuteketezwa ya siku zote, na hiyo sadaka yake ya unga na sadaka yake ya kinywaji. Hesabu 29:38

and one male goat for a sin-offering, besides the continual burnt offering, and the meal-offering of it, and the drink-offering of it.

Sadaka hizo mtamsongezea Bwana katika sikukuu zenu zilizoamriwa, zaidi ya nadhiri zenu, na sadaka zenu za hiari, kuwa sadaka zenu za kuteketezwa, na sadaka zenu za unga, na sadaka zenu za vinywaji, na sadaka zenu za amani. Hesabu 29:39

These you shall offer to Yahweh in your set feasts, besides your vows, and your freewill-offerings, for your burnt offerings, and for your meal-offerings, and for your drink-offerings, and for your peace-offerings.

Naye Musa akawaambia wana wa Israeli vile vile kama hayo yote Bwana alivyomwagiza Musa. Hesabu 29:40

Moses told the children of Israel according to all that Yahweh commanded Moses.