Kutoka 39 Swahili & English

Listen/Download Audio
Kutoka 39 (Swahili) Exodus 39 (English)

Na zile nyuzi za rangi ya samawi, na nyuzi za rangi ya zambarau, na nyekundu, wakafanya mavazi yaliyofumwa kwa ustadi sana kwa ajili ya kutumika katika mahali patakatifu, na kuyafanya hayo mavazi matakatifu ya Haruni, vile vile kama Bwana alivyomwagiza Musa. Kutoka 39:1

Of the blue, purple, and scarlet, they made finely worked garments, for ministering in the holy place, and made the holy garments for Aaron; as Yahweh commanded Moses.

Naye akaifanya hiyo naivera, ya nyuzi za dhahabu, na za rangi ya samawi, na za rangi ya zambarau, na za rangi nyekundu, na kitani nzuri ya kusokotwa. Kutoka 39:2

He made the ephod of gold, blue, purple, scarlet, and fine twined linen.

Nao wakaifua hiyo dhahabu hata ikawa mabamba membamba sana, kisha wakaikata iwe nyuzi, ili wapate kuifuma pamoja na hizo nyuzi za rangi ya samawi, na za rangi ya zambarau, na nyuzi nyekundu na za kitani nzuri, kazi ya fundi stadi sana. Kutoka 39:3

They beat the gold into thin plates, and cut it into wires, to work it in the blue, in the purple, in the scarlet, and in the fine linen, the work of the skillful workman.

Nao wakafanya na vipande vya mabegani kwa ajili yake, vilivyoungwa pamoja; viliungwa pamoja kwa ncha zake mbili. Kutoka 39:4

They made shoulder-pieces for it, joined together. At the two ends it was joined together.

Na huo mshipi wa kazi ya werevu, uliokuwa juu yake ili kuifunga mahali pake; ulikuwa wa kitu kimoja, na wa kazi moja na naivera ya dhahabu, na rangi ya samawi, na rangi ya zambarau, na nyekundu, na kitani nzuri ya kusokotwa; vile vile kama Bwana alivyomwagiza Musa. Kutoka 39:5

The skillfully woven band that was on it, with which to fasten it on, was of the same piece, like its work; of gold, of blue, purple, scarlet, and fine twined linen; as Yahweh commanded Moses.

Nao wakavitengeza vile vito vya shohamu, vilivyotiwa katika vijalizo vya dhahabu, vilivyochorwa mfano wa kuchora kwake muhuri, kwa majina ya hao wana wa Israeli. Kutoka 39:6

They worked the onyx stones, enclosed in settings of gold, engraved with the engravings of a signet, according to the names of the children of Israel.

Naye akavitia katika vile vipande vya mabegani vya hiyo naivera, viwe vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli, kama Bwana alivyomwagiza Musa. Kutoka 39:7

He put them on the shoulder-pieces of the ephod, to be stones of memorial for the children of Israel, as Yahweh commanded Moses.

Naye akafanya kile kifuko cha kifuani, kazi ya fundi stadi, kama hiyo kazi ya naivera; ya nyuzi za dhahabu, na za rangi ya samawi, na za rangi ya zambarau, na nyekundu, na kitani nzuri ya kusokotwa. Kutoka 39:8

He made the breastplate, the work of a skillful workman, like the work of the ephod; of gold, of blue, purple, scarlet, and fine twined linen.

Kilikuwa mraba; wakakifanya kile kifuko cha kifuani kwa kukikunja; urefu wake ulikuwa shibiri, na upana wake ulikuwa shibiri, tena kilikuwa ni cha kukunjwa. Kutoka 39:9

It was square. They made the breastplate double. Its length was a span, and its breadth a span, being double.

Nao wakatia safu nne za vito ndani yake, safu moja ilikuwa ni akiki, na yakuti ya rangi ya manjano, na baharamani, vilikuwa ni safu ya kwanza. Kutoka 39:10

They set in it four rows of stones. A row of ruby, topaz, and beryl was the first row;

Na safu ya pili ilikuwa zumaridi, na yakuti samawi, na almasi. Kutoka 39:11

and the second row, a turquoise, a sapphire{or, lapis lazuli}, and an emerald;

Na safu ya tatu ilikuwa ni hiakintho, na akiki nyekundu, na amethisto. Kutoka 39:12

and the third row, a jacinth, an agate, and an amethyst;

Na safu ya nne ilikuwa ni zabarajadi, na shohamu, na yaspi: vito hivyo vilikuwa vimetiwa katika vijalizo vya dhahabu, kila kimoja mahali pake. Kutoka 39:13

and the fourth row, a chrysolite, an onyx, and a jasper. They were enclosed in gold settings.

Na hivyo vito vilikuwa vyaandama majina ya wana wa Israeli, kumi na mawili, sawasawa na majina yao; mfano wa kuchora muhuri, kila moja kwa jina lake, kwa zile kabila kumi na mbili. Kutoka 39:14

The stones were according to the names of the children of Israel, twelve, according to their names; like the engravings of a signet, everyone according to his name, for the twelve tribes.

Nao wakafanya katika kile kifuko cha kifuani mikufu mfano wa kamba, ya kazi ya kusokotwa ya dhahabu safi. Kutoka 39:15

They made on the breastplate chains like cords, of braided work of pure gold.

Nao wakafanya vijalizo viwili vya dhahabu, na pete mbili za dhahabu; nao wakazitia hizo pete mbili katika ncha mbili za hicho kifuko. Kutoka 39:16

They made two settings of gold, and two gold rings, and put the two rings on the two ends of the breastplate.

Nao wakaitia hiyo mikufu miwili iliyosokotwa katika hizo pete mbili zilizokuwa katika ncha mbili za hicho kifuko. Kutoka 39:17

They put the two braided chains of gold in the two rings at the ends of the breastplate.

Na ncha hizo mbili nyingine, za hiyo mikufu miwili ya kusokotwa, wakazitia katika vile vijalizo viwili, na kuvitia katika vile vipande vya mabegani vya naivera, upande wa mbele. Kutoka 39:18

The other two ends of the two braided chains they put on the two settings, and put them on the shoulder-pieces of the ephod, in the front of it.

Nao wakafanya pete mbili za dhahabu, na kuzitia katika ncha mbili za kifuko cha kifuani, katika ukingo wake, ulio upande wa naivera ulio ndani. Kutoka 39:19

They made two rings of gold, and put them on the two ends of the breastplate, on the edge of it, which was toward the side of the ephod inward.

Nao wakafanya pete mbili za dhahabu, na kuzitia katika vile vipande viwili vya ile naivera chini yake, upande wa mbele, karibu na kifungo chake, juu ya huo mshipi wa naivera uliosukwa kwa ustadi. Kutoka 39:20

They made two rings of gold, and put them on the two shoulder-pieces of the ephod underneath, in the front of it, close by its coupling, above the skillfully woven band of the ephod.

Nao wakakikaza kile kifuko kwa pete zake kwenye naivera kwa ukanda wa rangi ya samawi, ili kikae pale juu ya mshipi wa naivera uliosukwa kwa ustadi, na ya kwamba kifuko cha kifuani kisiachane na naivera; vile vile kama Bwana alivyomwagiza Musa. Kutoka 39:21

They bound the breastplate by its rings to the rings of the ephod with a lace of blue, that it might be on the skillfully woven band of the ephod, and that the breastplate might not come loose from the ephod, as Yahweh commanded Moses.

Naye akafanya hiyo joho ya naivera ya kazi ya kusuka, rangi ya samawi yote; Kutoka 39:22

He made the robe of the ephod of woven work, all of blue.

na hilo tundu lililokuwa katikati yake, mfano wa tundu lililo katika kanzu ya chuma, na utepe wake kulizunguka hilo tundu, ili lisipasuke. Kutoka 39:23

The opening of the robe in the midst of it was like the opening of a coat of mail, with a binding around its opening, that it should not be torn.

Nao wakatia katika upindo wa joho makomamanga ya nyuzi za rangi ya samawi, na rangi ya zambarau, na rangi nyekundu, na kitani iliyosokotwa. Kutoka 39:24

They made on the skirts of the robe pomegranates of blue, purple, scarlet, and twined linen.

Nao wakafanya njuga za dhahabu safi, na kuzitia hizo njuga kati ya hayo makomamanga pande zote, kati ya hayo makomamanga; Kutoka 39:25

They made bells of pure gold, and put the bells between the pomegranates around the skirts of the robe, between the pomegranates;

njuga na komamanga, njuga na komamanga katika pindo za joho kuizunguka pande zote, ili kutumika kwa hiyo; vile vile kama Bwana alivyomwagiza Musa. Kutoka 39:26

a bell and a pomegranate, a bell and a pomegranate, around the skirts of the robe, to minister in, as Yahweh commanded Moses.

Nao wakafanya hizo kanzu za nguo ya kitani nzuri ya kufumwa, kwa Haruni, na kwa wanawe Kutoka 39:27

They made the coats of fine linen of woven work for Aaron, and for his sons,

na hicho kilemba cha nguo ya kitani nzuri, na zile kofia nzuri za kitani, na hizo suruali za nguo ya kitani nzuri iliyosokotwa, Kutoka 39:28

and the turban of fine linen, and the linen headbands of fine linen, and the linen breeches of fine twined linen,

na huo mshipi wa nguo nzuri ya kitani iliyosokotwa, na rangi ya samawi, na rangi ya zambarau, na nyekundu, kazi ya fundi mwenye kutia taraza; vile vile kama Bwana alivyomwagiza Musa. Kutoka 39:29

and the sash of fine twined linen, and blue, and purple, and scarlet, the work of the embroiderer, as Yahweh commanded Moses.

Nao wakafanya hilo bamba la hiyo taji takatifu la dhahabu safi, na kuandika juu yake andiko, mfano wa kuchorwa kwa muhuri, MTAKATIFU KWA Bwana. Kutoka 39:30

They made the plate of the holy crown of pure gold, and wrote on it a writing, like the engravings of a signet: "HOLY TO YAHWEH."

Nao wakatia ukanda wa rangi ya samawi ili kulifunga katika hicho kilemba upande wa juu; vile vile kama Bwana alivyomwagiza Musa. Kutoka 39:31

They tied to it a lace of blue, to fasten it on the turban above, as Yahweh commanded Moses.

Basi ndivyo ilivyomalizwa kazi yote ya maskani ya hema ya kukutania; na wana wa Israeli walifanya kama yote Bwana aliyomwagiza Musa, ndivyo walivyofanya. Kutoka 39:32

Thus all the work of the tent of the tent of meeting was finished. The children of Israel did according to all that Yahweh commanded Moses; so they did.

Nao wakamletea Musa hiyo maskani; yaani Hema, na vyombo vyake vyote, vifungo vyake, na mbao zake, na mataruma yake, na nguzo zake, na matako yake; Kutoka 39:33

They brought the tent to Moses, the tent, with all its furniture, its clasps, its boards, it bars, its pillars, its sockets,

na kifuniko chake cha ngozi za kondoo waume zilizotiwa rangi nyekundu, na kifuniko cha ngozi za pomboo, na pazia la sitara; Kutoka 39:34

the covering of rams' skins dyed red, the covering of sea cow hides, the veil of the screen,

na sanduku la ushuhuda, na miti yake, na kiti cha rehema; Kutoka 39:35

the ark of the testimony with its poles, the mercy seat,

na meza, na vyombo vyake vyote, na mikate ya wonyesho; Kutoka 39:36

the table, all its vessels, the show bread,

na kinara cha taa safi, na taa zake, hizo taa za kuwekwa mahali pake, na vyombo vyake vyote, na mafuta ya taa, Kutoka 39:37

the pure lampstand, its lamps, even the lamps to be set in order, all its vessels, the oil for the light,

na madhabahu ya dhahabu, na mafuta ya kutiwa, na uvumba mzuri, na pazia kwa mlango wa hema; Kutoka 39:38

the golden altar, the anointing oil, the sweet incense, the screen for the door of the Tent,

na madhabahu ya shaba, na wavu wake wa shaba, na miti yake, na vyombo vyake vyote, na birika na tako lake; Kutoka 39:39

the brazen altar, its grating of brass, its poles, all of its vessels, the basin and its base,

na ukuta wa nguo wa ua, na nguzo zake na matako yake, na pazia la lango la ua, na kamba zake, na vigingi vyake, na vyombo vyote vya kutumiwa katika utumishi wa maskani, kwa hiyo hema ya kukutania, Kutoka 39:40

the hangings of the court, its pillars, its sockets, the screen for the gate of the court, its cords, its pins, all the instruments of the service of the tent, for the tent of meeting,

na mavazi ya kazi nzuri kwa utumishi katika mahali patakatifu, na mavazi matakatifu ya Haruni kuhani, na mavazi ya wanawe, ili kutumika katika kazi ya ukuhani. Kutoka 39:41

the finely worked garments for ministering in the holy place, the holy garments for Aaron the priest, and the garments of his sons, to minister in the priest's office.

Sawasawa na yote Bwana aliyomwagiza Musa, ndivyo walivyoifanya hiyo kazi yote wana wa Israeli. Kutoka 39:42

According to all that Yahweh commanded Moses, so the children of Israel did all the work.

Musa akaiona hiyo kazi yote, na tazama, walikuwa wameimaliza; vile vile kama Bwana alivyoagiza, walikuwa wameifanya vivyo; basi Musa akawaombea heri. Kutoka 39:43

Moses saw all the work, and, behold, they had done it as Yahweh had commanded, even so had they done it: and Moses blessed them.