Kutoka 31 Swahili & English
Listen/Download AudioKutoka 31 (Swahili) | Exodus 31 (English) |
---|---|
Bwana akanena na Musa, na kumwambia, Kutoka 31:1 |
Yahweh spoke to Moses, saying, |
Angalia, nimemwita kwa jina lake Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila ya Yuda; Kutoka 31:2 |
"Behold, I have called by name Bezalel the son of Uri, the son of Hur, of the tribe of Judah: |
nami nimemjaza roho ya Mungu, katika hekima, na maarifa, na ujuzi, na mambo ya kazi ya kila aina, Kutoka 31:3 |
and I have filled him with the Spirit of God, in wisdom, and in understanding, and in knowledge, and in all manner of workmanship, |
ili abuni kazi za ustadi, kuwa fundi wa dhahabu, na wa fedha, na wa shaba, Kutoka 31:4 |
to devise skillful works, to work in gold, and in silver, and in brass, |
na kukata vito kwa kutiwa mahali, na kuchora miti, na kufanya kazi ya ustadi iwayo yote. Kutoka 31:5 |
and in cutting of stones for setting, and in carving of wood, to work in all manner of workmanship. |
Tena, tazama, nimemchagua, awe pamoja naye, huyo Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila ya Dani; nami nimetia hekima katika mioyo ya wote wenye moyo wa hekima, ili wapate kufanya vyote nilivyokuagiza; Kutoka 31:6 |
I, behold, I have appointed with him Oholiab, the son of Ahisamach, of the tribe of Dan; and in the heart of all who are wise-hearted I have put wisdom, that they may make all that I have commanded you: |
yaani, hema ya kukutania na sanduku la ushuhuda, na kiti cha rehema kilicho juu yake, na vyombo vyote vya Hema; Kutoka 31:7 |
the tent of meeting, the ark of the testimony, the mercy seat that is on it, all the furniture of the Tent, |
na meza, na vyombo vyake, na kinara cha taa safi pamoja na vyombo vyake vyote, na madhabahu ya kufukizia uvumba; Kutoka 31:8 |
the table and its vessels, the pure lampstand with all its vessels, the altar of incense, |
na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na vyombo vyake vyote, na birika na tako lake; Kutoka 31:9 |
the altar of burnt offering with all its vessels, the basin and its base, |
na mavazi yenye kufumwa kwa uzuri, na mavazi matakatifu ya Haruni kuhani, na mavazi ya wanawe, ili kutumika katika kazi ya ukuhani; Kutoka 31:10 |
the finely worked garments--the holy garments for Aaron the priest--the garments of his sons to minister in the priest's office, |
na mafuta ya kutiwa, na uvumba wa manukato mazuri, kwa ajili ya mahali patakatifu; sawasawa na yote niliyokuagiza ndivyo watakavyofanya wao. Kutoka 31:11 |
the anointing oil, and the incense of sweet spices for the holy place: according to all that I have commanded you they shall do." |
Bwana akasema na Musa, na kumwambia, Kutoka 31:12 |
Yahweh spoke to Moses, saying, |
Kisha, nena wewe na wana wa Israeli, na kuwaambia, Hakika mtazishika Sabato zangu, kwa kuwa ni ishara kati ya mimi na ninyi katika vizazi vyenu vyote; ili mpate kujua ya kuwa mimi ndimi Bwana niwatakasaye ninyi. Kutoka 31:13 |
"Speak also to the children of Israel, saying, 'Most assuredly you shall keep my Sabbaths: for it is a sign between me and you throughout your generations; that you may know that I am Yahweh who sanctifies you. |
Basi mtaishika hiyo Sabato; kwa kuwa ni takatifu kwenu; kila mtu atakayeitia unajisi hakika yake atauawa; kwa kuwa kila mtu afanyaye kazi katika siku hiyo, nafsi hiyo itakatiliwa mbali na watu wake. Kutoka 31:14 |
You shall keep the Sabbath therefore; for it is holy to you. Everyone who profanes it shall surely be put to death; for whoever does any work therein, that soul shall be cut off from among his people. |
Kazi itafanywa siku sita; lakini siku ya saba ni Sabato ya kustarehe kabisa, takatifu kwa Bwana; kila mtu atakayefanya kazi yo yote katika siku ya Sabato, hakika yake atauawa. Kutoka 31:15 |
Six days shall work be done, but on the seventh day is a Sabbath of solemn rest, holy to Yahweh. Whoever does any work on the Sabbath day shall surely be put to death. |
Kwa ajili ya hayo wana wa Israeli wataishika Sabato, kuiangalia sana hiyo Sabato katika vizazi vyao vyote, ni agano la milele. Kutoka 31:16 |
Therefore the children of Israel shall keep the Sabbath, to observe the Sabbath throughout their generations, for a perpetual covenant. |
Ni ishara kati ya mimi na wana wa Israeli milele; kwani kwa siku sita Bwana alifanya mbingu na nchi, akastarehe kwa siku ya saba na kupumzika. Kutoka 31:17 |
It is a sign between me and the children of Israel forever; for in six days Yahweh made heaven and earth, and on the seventh day he rested, and was refreshed.'" |
Hapo Bwana alipokuwa amekwisha zungumza na Musa katika mlima wa Sinai, akampa hizo mbao mbili za ushuhuda, mbao mbili za mawe, zilizoandikwa kwa chanda cha Mungu. Kutoka 31:18 |
He gave to Moses, when he finished speaking with him on Mount Sinai, the two tablets of the testimony, stone tablets, written with God's finger. |