Kutoka 1 Swahili & English

Listen/Download Audio
Kutoka 1 (Swahili) Exodus 1 (English)

Basi majina ya wana wa Israeli walioingia Misri ni haya; kila mtu pamoja na jamaa zake walikuja pamoja na Yakobo. Kutoka 1:1

Now these are the names of the sons of Israel, who came into Egypt (every man and his household came with Jacob):

Reubeni, na Simeoni na Lawi, na Yuda; Kutoka 1:2

Reuben, Simeon, Levi, and Judah,

na Isakari, na Zabuloni, na Benyamini; Kutoka 1:3

Issachar, Zebulun, and Benjamin,

na Dani, na Naftali, na Gadi, na Asheri. Kutoka 1:4

Dan and Naphtali, Gad and Asher.

Na nafsi zile zote zilizotoka viunoni mwa Yakobo zilikuwa ni nafsi sabini; na huyo Yusufu alikuwa huko ndani ya Misri tangu hapo. Kutoka 1:5

All the souls who came out of the Jacob's body were seventy souls, and Joseph was in Egypt already.

Yusufu akafa, na ndugu zake wote, na watu wote wa kizazi kile. Kutoka 1:6

Joseph died, as did all his brothers, and all that generation.

Na wana wa Israeli walikuwa na uzazi sana, na kuongezeka mno, na kuzidi kuwa wengi, nao wakaendelea na kuongezeka nguvu; na ile nchi ilikuwa imejawa na wao. Kutoka 1:7

The children of Israel were fruitful, and increased abundantly, and multiplied, and grew exceedingly mighty; and the land was filled with them.

Basi akainuka mfalme mpya kutawala Misri, asiyemjua Yusufu. Kutoka 1:8

Now there arose a new king over Egypt, who didn't know Joseph.

Akawaambia watu wake, Angalieni, watu wa wana wa Israeli ni wengi tena wana nguvu kuliko sisi. Kutoka 1:9

He said to his people, "Behold, the people of the children of Israel are more and mightier than we.

Haya! Na tuwatendee kwa akili, wasije wakaongezeka; tena, ikitokea vita, wao nao wasije wakashikamana na adui zetu na kupigana nasi, na kutoka katika nchi hii. Kutoka 1:10

Come, let us deal wisely with them, lest they multiply, and it happen that when any war breaks out, they also join themselves to our enemies, and fight against us, and escape out of the land."

Basi wakaweka wasimamizi juu yao wawatese kwa mizigo yao. Nao wakamjengea Farao miji ya kuwekea akiba, Pithomu na Ramesesi. Kutoka 1:11

Therefore they set taskmasters over them to afflict them with their burdens. They built storage cities for Pharaoh: Pithom and Raamses.

Lakini kwa kadiri ya walivyowatesa ndivyo walivyoongezeka na kuzidi kuenea. Nao walichukiwa kwa sababu ya wana wa Israeli. Kutoka 1:12

But the more they afflicted them, the more they multiplied and the more they spread out. They were grieved because of the children of Israel.

Wamisri wakawatumikisha wana wa Israeli kwa ukali; Kutoka 1:13

The Egyptians ruthlessly made the children of Israel serve,

wakafanya maisha yao kuwa uchungu kwa kazi ngumu; kazi ya chokaa na ya matofali, na kila namna ya kazi ya mashamba; kwa kazi zao zote walizowatumikisha kwa ukali. Kutoka 1:14

and they made their lives bitter with hard service, in mortar and in brick, and in all manner of service in the field, all their service, in which they ruthlessly made them serve.

Kisha mfalme wa Misri akasema na wazalisha wa Waebrania, mmoja jina lake aliitwa Shifra, na wa pili jina lake aliitwa Pua; Kutoka 1:15

The king of Egypt spoke to the Hebrew midwives, of whom the name of the one was Shiphrah, and the name of the other Puah,

akasema, Wakati mwazalishapo wanawake wa Kiebrania na kuwaona wa katika kuzaa, ikiwa ni mtoto mwanamume, basi mwueni, bali ikiwa ni mtoto mwanamke, na aishi. Kutoka 1:16

and he said, "When you perform the duty of a midwife to the Hebrew women, and see them on the birth stool; if it is a son, then you shall kill him; but if it is a daughter, then she shall live."

Lakini wale wazalisha walikuwa wakimcha Mungu, wasifanye kama walivyoamriwa na huyo mfalme wa Misri, lakini wakawahifadhi hai wale wanaume. Kutoka 1:17

But the midwives feared God, and didn't do what the king of Egypt commanded them, but saved the baby boys alive.

Basi mfalme wa Misri akawaita wale wazalisha na kuwauliza, Kwa nini kufanya jambo hili, na kuwahifadhi watoto waume wawe hai? Kutoka 1:18

The king of Egypt called for the midwives, and said to them, "Why have you done this thing, and have saved the men-children alive?"

Wazalisha wakamwambia Farao, Ni kwa sababu hao wanawake wa Kiebrania si kama wanawake wa Kimisri; kwa kuwa ni hodari hao, nao huzaa kabla mzalisha hajapata kuwafikilia. Kutoka 1:19

The midwives said to Pharaoh, "Because the Hebrew women aren't like the Egyptian women; for they are vigorous, and give birth before the midwife comes to them."

Basi Mungu akawatendea mema wale wazalisha; na hao watu wakaongezeka sana, wakaendelea na kuzidi kuwa na nguvu nyingi. Kutoka 1:20

God dealt well with the midwives, and the people multiplied, and grew very mighty.

Ilikuwa kwa sababu wale wazalisha walikuwa wakimcha Mungu, akawasimamishia nyumba. Kutoka 1:21

It happened, because the midwives feared God, that he gave them families.

Kisha huyo Farao akawaagiza watu wake, akisema, Kila mtoto mwanamume atakayezaliwa mtamtupa mtoni, na kila mtoto mwanamke mtamhifadhi hai. Kutoka 1:22

Pharaoh charged all his people, saying, "You shall cast every son who is born into the river, and every daughter you shall save alive."