Kutoka 29 Swahili & English

Listen/Download Audio
Kutoka 29 (Swahili) Exodus 29 (English)

Nawe uwafanyie jambo hili, ili kuwatakasa, wapate kunitumikia mimi katika kazi ya ukuhani; twaa ng'ombe mmoja mume kijana, na kondoo waume wawili walio wakamilifu, Kutoka 29:1

"This is the thing that you shall do to them to make them holy, to minister to me in the priest's office: take one young bull and two rams without blemish,

na mkate usiotiwa chachu, na maandazi yasiyotiwa chachu yaliyokandwa kwa mafuta, na kaki zisizotiwa chachu zilizotiwa mafuta; utazifanya za unga mzuri mwembamba wa ngano. Kutoka 29:2

unleavened bread, unleavened cakes mixed with oil, and unleavened wafers anointed with oil: you shall make them of fine wheat flour.

Nawe vitie vyote katika kikapu, uvilete ndani ya kikapu, pamoja na huyo ng'ombe, na hao kondoo waume wawili. Kutoka 29:3

You shall put them into one basket, and bring them in the basket, with the bull and the two rams.

Kisha mlete Haruni na wanawe hata mlangoni pa hema ya kukutania, ukawaoshe kwa maji. Kutoka 29:4

You shall bring Aaron and his sons to the door of the tent of meeting, and shall wash them with water.

Kisha twaa hayo mavazi na kumvika Haruni; itie kanzu, na joho ya naivera, na naivera, na kifuko cha kifuani, na kumkaza kwa huo mshipi wa naivera uliosukwa kwa ustadi; Kutoka 29:5

You shall take the garments, and put on Aaron the coat, the robe of the ephod, the ephod, and the breastplate, and dress him with the skillfully woven band of the ephod;

nawe mvike kile kilemba kichwani, na ile taji takatifu utaitia katika kile kilemba. Kutoka 29:6

and you shall set the turban on his head, and put the holy crown on the turban.

Ndipo utakapotwaa hayo mafuta ya kutiwa, na kummiminia kichwani mwake, na kumtia mafuta. Kutoka 29:7

Then you shall take the anointing oil, and pour it on his head, and anoint him.

Kisha walete hao wanawe na kuwavika kanzu. Kutoka 29:8

You shall bring his sons, and put coats on them.

Nawe uwakaze mishipi, Haruni na wanawe, na kuwavika kofia; nao watakuwa na huo ukuhani kwa amri ya milele; nawe utawaweka Haruni na wanawe kwa kazi takatifu. Kutoka 29:9

You shall dress them with belts, Aaron and his sons, and bind headbands on them: and they shall have the priesthood by a perpetual statute: and you shall consecrate Aaron and his sons.

Kisha utamleta huyo ng'ombe mbele ya hema ya kukutania; na Haruni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo ng'ombe. Kutoka 29:10

"You shall bring the bull before the tent of meeting: and Aaron and his sons shall lay their hands on the head of the bull.

Kisha utamchinja huyo ng'ombe mbele ya Bwana, mlangoni pa hema ya kukutania. Kutoka 29:11

You shall kill the bull before Yahweh, at the door of the tent of meeting.

Kisha twaa baadhi ya damu ya ng'ombe, uitie katika pembe za madhabahu kwa kidole chako; na kuimimina damu yote chini ya madhabahu. Kutoka 29:12

You shall take of the blood of the bull, and put it on the horns of the altar with your finger; and you shall pour out all the blood at the base of the altar.

Kisha twaa mafuta yote yafunikayo matumbo, na kitambi kilicho katika ini, na figo mbili, na mafuta yaliyo juu yake, uyateketeze yote juu ya madhabahu. Kutoka 29:13

You shall take all the fat that covers the innards, the cover of the liver, the two kidneys, and the fat that is on them, and burn them on the altar.

Lakini nyama yake huyo ng'ombe, na ngozi yake, na mavi yake, utayachoma kwa moto nje ya marago; ni sadaka kwa ajili ya dhambi. Kutoka 29:14

But the flesh of the bull, and its skin, and its dung, you shall burn with fire outside of the camp: it is a sin-offering.

Pia mtwae kondoo mume mmoja; na Haruni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake huyo kondoo mume. Kutoka 29:15

"You shall also take the one ram; and Aaron and his sons shall lay their hands on the head of the ram.

Kisha utamchinja huyo kondoo mume, na kuitwaa damu yake, na kuinyunyiza katika madhabahu kuizunguka kando-kando. Kutoka 29:16

You shall kill the ram, and you shall take its blood, and sprinkle it around on the altar.

Kisha utamkata-kata kondoo vipande vyake, na kuyaosha matumbo yake na miguu yake, na kuiweka pamoja na vipande vyake na kichwa chake. Kutoka 29:17

You shall cut the ram into its pieces, and wash its innards, and its legs, and put them with its pieces, and with its head.

Nawe mteketeze kondoo mzima juu ya madhabahu; ni sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya Bwana; ni harufu nzuri, sadaka iliyosongezwa kwa Bwana kwa njia ya moto. Kutoka 29:18

You shall burn the whole ram on the altar: it is a burnt offering to Yahweh; it is a sweet savor, an offering made by fire to Yahweh.

Kisha mtwae huyo kondoo wa pili; na Haruni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake huyo kondoo. Kutoka 29:19

"You shall take the other ram; and Aaron and his sons shall lay their hands on the head of the ram.

Kisha utamchinja kondoo, na kuitwaa damu yake, na kuitia katika ncha ya sikio la Haruni la upande wa kuume, na katika ncha za masikio ya kuume ya wanawe, na katika vyanda vya gumba vya mikono yao ya kuume, na katika vidole vikuu vya miguu yao ya kuume, na kuinyunyiza hiyo damu katika madhabahu kuizunguka kando-kando. Kutoka 29:20

Then you shall kill the ram, and take some of its blood, and put it on the tip of the right ear of Aaron, and on the tip of the right ear of his sons, and on the thumb of their right hand, and on the big toe of their right foot, and sprinkle the blood on the altar round about.

Kisha twaa katika hiyo damu iliyo juu ya madhabahu, na katika hayo mafuta ya kutiwa, na kumnyunyizia Haruni, juu ya mavazi yake, na wanawe, na mavazi yao pia, pamoja naye; naye atatakaswa, na mavazi yake, na wanawe, na mavazi ya wanawe, pamoja naye. Kutoka 29:21

You shall take of the blood that is on the altar, and of the anointing oil, and sprinkle it on Aaron, and on his garments, and on his sons, and on the garments of his sons with him: and he shall be made holy, and his garments, and his sons, and his sons' garments with him.

Tena yatwae mafuta ya huyo kondoo mume, na mkia wake wa mafuta, na mafuta yafunikayo matumbo, na kitambi kilicho katika ini, na figo mbili, na mafuta yaliyo katika hizo figo, na paja la kuume; kwani ni kondoo ambaye ni wa kuwekwa kwa kazi takatifu; Kutoka 29:22

Also you shall take some of the ram's fat, the fat tail, the fat that covers the innards, the cover of the liver, the two kidneys, the fat that is on them, and the right thigh (for it is a ram of consecration),

utwae na mkate mmoja wa unga, na mkate mmoja ulioandaliwa kwa mafuta, na kaki moja katika kile kikapu cha mikate isiyotiwa chachu, kilichowekwa mbele ya Bwana; Kutoka 29:23

and one loaf of bread, one cake of oiled bread, and one wafer out of the basket of unleavened bread that is before Yahweh.

nawe utavitia hivi vyote katika mikono ya Haruni, na katika mikono ya wanawe; nawe utavitikisa-tikisa viwe sadaka ya kutikiswa mbele za Bwana. Kutoka 29:24

You shall put all of this in Aaron's hands, and in his sons' hands, and shall wave them for a wave-offering before Yahweh.

Kisha uvitwae vile vitu mikononi mwao, na kuviteketeza juu ya madhabahu, juu ya ile sadaka ya kuteketezwa, viwe harufu nzuri mbele ya Bwana; ni sadaka iliyosongezwa kwa Bwana kwa njia ya moto. Kutoka 29:25

You shall take them from their hands, and burn them on the altar on the burnt offering, for a sweet savor before Yahweh: it is an offering made by fire to Yahweh.

Kisha twaa kidari cha huyo kondoo wa kuwekwa kwake Haruni kwa kazi takatifu, na kukitikisa-tikisa kiwe sadaka ya kutikiswa mbele za Bwana; nacho kitakuwa ni sehemu yako. Kutoka 29:26

"You shall take the breast of Aaron's ram of consecration, and wave it for a wave-offering before Yahweh: and it shall be your portion.

Nawe kitakase kile kidari cha ile sadaka ya kutikiswa, na lile paja la sadaka ya kuinuliwa, lililotikiswa, na lililoinuliwa juu, vya yule kondoo wa kuwekwa kwa kazi takatifu, huyo aliyekuwa kwa ajili ya Haruni, na huyo aliyekuwa kwa ajili ya wanawe; Kutoka 29:27

You shall sanctify the breast of the wave-offering, and the thigh of the heave-offering, which is waved, and which is heaved up, of the ram of consecration, even of that which is for Aaron, and of that which is for his sons:

navyo vitakuwa vya Haruni na wanawe posho ya lazima sikuzote itokayo kwa hao wana wa Israeli; kwa kuwa ni sadaka ya kuinuliwa; nayo itakuwa ni sadaka ya kuinuliwa itokayo kwa hao wana wa Israeli katika dhabihu zao za sadaka za amani, ni sadaka yao ya kuinuliwa kwa ajili ya Bwana. Kutoka 29:28

and it shall be for Aaron and his sons as their portion forever from the children of Israel; for it is a heave-offering: and it shall be a heave-offering from the children of Israel of the sacrifices of their peace-offerings, even their heave-offering to Yahweh.

Na hayo mavazi matakatifu ya Haruni yatakuwa ya wanawe baada yake, wayavae watakapotiwa mafuta, na watakapowekwa kwa kazi takatifu. Kutoka 29:29

"The holy garments of Aaron shall be for his sons after him, to be anointed in them, and to be consecrated in them.

Huyo mwanawe atakayekuwa kuhani badala yake atayavaa muda wa siku saba, hapo atakapoingia ndani ya hiyo hema ya kukutania, ili atumike ndani ya mahali patakatifu. Kutoka 29:30

Seven days shall the son who is priest in his place put them on, when he comes into the tent of meeting to minister in the holy place.

Nawe twaa huyo kondoo mume aliyekuwa wa kuwekwa kwa kazi takatifu, na kuitokosa nyama yake katika mahali patakatifu. Kutoka 29:31

"You shall take the ram of consecration, and boil its flesh in a holy place.

Na Haruni na wanawe wataila ile nyama ya kondoo, na mikate iliyo katika kile kikapu, hapo mbele ya mlango wa hema ya kukutania. Kutoka 29:32

Aaron and his sons shall eat the flesh of the ram, and the bread that is in the basket, at the door of the tent of meeting.

Nao watakula vile vitu ambavyo upatanisho ulifanywa kwa hivyo, ili kuwaweka kwa kazi takatifu na kuwatakasa; lakini mgeni asivile, maana, ni vitu vitakatifu. Kutoka 29:33

They shall eat those things with which atonement was made, to consecrate and sanctify them: but a stranger shall not eat of it, because they are holy.

Na kwamba kitu cho chote cha ile nyama, iliyo kwa ajili ya kuweka kwa kazi takatifu, au cho chote cha hiyo mikate, kikisalia hata asubuhi, ndipo utavichoma kwa moto hivyo vilivyosalia; havitaliwa, maana, ni vitu vitakatifu. Kutoka 29:34

If anything of the flesh of the consecration, or of the bread, remains to the morning, then you shall burn the remainder with fire: it shall not be eaten, because it is holy.

Ni hivyo utakavyowatendea Haruni na wanawe, sawasawa na hayo yote niliyokuagiza; utawaweka kwa kazi takatifu siku saba. Kutoka 29:35

"Thus shall you do to Aaron, and to his sons, according to all that I have commanded you. Seven days shall you consecrate them.

Kila siku utamtoa ng'ombe wa sadaka ya dhambi kwa ajili ya upatanisho; nawe utaisafisha hiyo madhabahu, hapo utakapofanya upatanisho kwa ajili ya hiyo madhabahu; nawe utaitia mafuta, ili kuitakasa. Kutoka 29:36

Every day shall you offer the bull of sin-offering for atonement: and you shall cleanse the altar, when you make atonement for it; and you shall anoint it, to sanctify it.

Utafanya upatanisho kwa ajili ya hiyo madhabahu muda wa siku saba, na kuitakasa; ndipo madhabahu itakapokuwa takatifu sana; kila kitu kiigusacho madhabahu kitakuwa kitakatifu. Kutoka 29:37

Seven days you shall make atonement for the altar, and sanctify it: and the altar shall be most holy; whatever touches the altar shall be holy.

Basi sadaka utakazozitoa juu ya madhabahu ni hizi; wana-kondoo wa mwaka mmoja wawili siku baada ya siku daima. Kutoka 29:38

"Now this is that which you shall offer on the altar: two lambs a year old day by day continually.

Mwana-kondoo mmoja utamchinja asubuhi; na mwana-kondoo wa pili utamchinja jioni; Kutoka 29:39

The one lamb you shall offer in the morning; and the other lamb you shall offer at evening:

tena, pamoja na mwana-kondoo mmoja utatoa vibaba vitatu vya unga mzuri uliochanganyika na mafuta yenye kupondwa, kiasi cha kibaba na robo kibaba; na divai kiasi cha kibaba na robo kibaba, iwe sadaka ya kinywaji. Kutoka 29:40

and with the one lamb a tenth part of an ephah of fine flour mixed with the fourth part of a hin of beaten oil, and the fourth part of a hin of wine for a drink-offering.

Na huyo mwana-kondoo wa pili utamchinja wakati wa jioni, nawe utamfanyia vivyo kama ile sadaka ya unga ya asubuhi, na kama ile sadaka yake ya kinywaji, iwe harufu nzuri, ni dhabihu ya kusongezwa kwa Bwana kwa njia ya moto. Kutoka 29:41

The other lamb you shall offer at evening, and shall do to it according to the meal-offering of the morning, and according to its drink-offering, for a sweet savor, an offering made by fire to Yahweh.

Itakuwa ni sadaka ya kuteketezwa milele katika vizazi vyenu vyote mlangoni pa ile hema ya kukutania mbele ya Bwana; hapo nitakapokutana nanyi, ili ninene na wewe hapo. Kutoka 29:42

It shall be a continual burnt offering throughout your generations at the door of the tent of meeting before Yahweh, where I will meet with you, to speak there to you.

Nami nitakutana na wana wa Israeli hapo, na hiyo Hema itafanywa takatifu na utukufu wangu. Kutoka 29:43

There I will meet with the children of Israel; and the place shall be sanctified by my glory.

Nami nitaitakasa hiyo hema ya kukutania, na hiyo madhabahu; pia Haruni na wanawe nitawatakasa, ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani. Kutoka 29:44

I will sanctify the tent of meeting and the altar: Aaron also and his sons I will sanctify, to minister to me in the priest's office.

Na mimi nitakaa kati ya wana wa Israeli, nami nitakuwa Mungu wao. Kutoka 29:45

I will dwell among the children of Israel, and will be their God.

Nao watanijua kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wao, niliyewaleta watoke katika nchi ya Misri, nipate kukaa kati yao; ni mimi Bwana Mungu wao.

Kutoka 29:46

They shall know that I am Yahweh their God, who brought them forth out of the land of Egypt, that I might dwell among them: I am Yahweh their God.