Kutoka 33 Swahili & English

Listen/Download Audio
Kutoka 33 (Swahili) Exodus 33 (English)

Bwana akanena na Musa, Haya, ondokeni, katokeni hapo, wewe na hao watu uliowaleta wakwee kutoka nchi ya Misri, waende nchi hiyo niliyomwapia Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, niliposema, Nitakipa kizazi chako nchi hii; Kutoka 33:1

Yahweh spoke to Moses, "Depart, go up from here, you and the people that you have brought up out of the land of Egypt, to the land of which I swore to Abraham, to Isaac, and to Jacob, saying, 'I will give it to your seed.'

nami nitamtuma malaika aende mbele yako; nami nitawafukuza Mkanaani, na Mwamori, na Mhiti, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi; Kutoka 33:2

I will send an angel before you; and I will drive out the Canaanite, the Amorite, and the Hittite, and the Perizzite, the Hivite, and the Jebusite:

waifikilie nchi imiminikayo maziwa na asali; kwa maana mimi sitakwenda kati yenu; kwa sababu ninyi ni watu wenye shingo ngumu; nisiwaangamize ninyi katika njia. Kutoka 33:3

to a land flowing with milk and honey: for I will not go up in the midst of you, for you are a stiff-necked people, lest I consume you in the way."

Watu waliposikia habari hizo mbaya wakaomboleza wala hapana mtu aliyevaa vyombo vyake vya uzuri. Kutoka 33:4

When the people heard this evil news, they mourned: and no one put on his jewelry.

Bwana akamwambia Musa, Waambie wana wa Israeli, Ninyi ni watu wenye shingo ngumu; kama mimi nikiingia kati yenu dakika moja, nitawaangamiza; basi sasa vueni vyombo vyenu vya uzuri ili nipate kujua nitakalowatenda. Kutoka 33:5

Yahweh said to Moses, "Tell the children of Israel, 'You are a stiff-necked people. If I were to go up into your midst for one moment, I would consume you. Therefore now take off your jewelry from you, that I may know what to do to you."

Basi wana wa Israeli wakavua vyombo vyao vyote vya uzuri, tangu mlima wa Horebu na mbele. Kutoka 33:6

The children of Israel stripped themselves of their jewelry from Mount Horeb onward.

Basi desturi ya Musa, ilikuwa kuitwaa ile hema, na kuikita nje ya marago mbali na hayo marago; akaiita, hema ya kukutania. Hata kila mtu aliyekuwa akitaka neno kwa Bwana, akatoka, akaenda hata hema ya kukutania, iliyokuwa nje ya marago. Kutoka 33:7

Now Moses used to take the tent and to pitch it outside the camp, far away from the camp, and he called it "The tent of meeting." It happened that everyone who sought Yahweh went out to the tent of meeting, which was outside the camp.

Hata Musa alipotoka kuiendea ile hema, watu wote waliondoka wakasimama, kila mtu mlangoni pa hema yake, akamtazama Musa, hata alipokwisha kuingia hemani. Kutoka 33:8

It happened that when Moses went out to the Tent, that all the people rose up, and stood, everyone at their tent door, and watched Moses, until he had gone into the Tent.

Ikawa Musa alipoingia humo hemani, ile nguzo ya wingu ikashuka, ikasimama mlangoni pa ile hema; naye Bwana akasema na Musa. Kutoka 33:9

It happened, when Moses entered into the Tent, that the pillar of cloud descended, stood at the door of the Tent, and spoke with Moses.

Watu wote wakaiona nguzo ya wingu ikisimama penye mlango wa hema; watu wote wakaondoka wakasujudu, kila mtu mlangoni pa hema yake. Kutoka 33:10

All the people saw the pillar of cloud stand at the door of the Tent, and all the people rose up and worshiped, everyone at their tent door.

Naye Bwana akasema na Musa uso kwa uso, kama vile mtu asemavyo na rafiki yake. Kisha akageuka akarejea hata maragoni; bali mtumishi wake Yoshua, mwana wa Nuni, naye ni kijana, hakutoka mle hemani. Kutoka 33:11

Yahweh spoke to Moses face to face, as a man speaks to his friend. He turned again into the camp, but his servant Joshua, the son of Nun, a young man, didn't depart out of the Tent.

Musa akamwambia Bwana, Angalia, wewe waniambia, Wachukue watu hawa; nawe hukunijulisha ni nani utakayemtuma pamoja nami. Walakini umesema, Nakujua jina lako, nawe umepata neema mbele zangu. Kutoka 33:12

Moses said to Yahweh, "Behold, you tell me, 'Bring up this people:' and you haven't let me know whom you will send with me. Yet you have said, 'I know you by name, and you have also found favor in my sight.'

Basi, sasa nakuomba, ikiwa nimepata neema mbele zako, unionyeshe njia zako, nipate kukujua, ili nipate neema mbele zako; ukakumbuke ya kuwa taifa hilo ndilo watu wako. Kutoka 33:13

Now therefore, if I have found favor in your sight, please show me now your ways, that I may know you, so that I may find favor in your sight: and consider that this nation is your people."

Akasema, Uso wangu utakwenda pamoja nawe, nami nitakupa raha. Kutoka 33:14

He said, "My presence will go with you, and I will give you rest."

Naye akamwambia, Uso wako usipokwenda pamoja nami, usituchukue kutoka hapa. Kutoka 33:15

He said to him, "If your presence doesn't go with me, don't carry us up from here.

Kwa maana itajulikanaje kuwa nimepata neema mbele zako, mimi na watu wako? Siyo kwa sababu unakwenda pamoja nasi, hata mimi na watu wako tutengwe na watu wote walio juu ya uso wa nchi? Kutoka 33:16

For how would people know that I have found favor in your sight, I and your people? Isn't it in that you go with us, so that we are separated, I and your people, from all the people who are on the surface of the earth?"

Bwana akamwambia Musa, Nitafanya na neno hili ulilolinena, kwa maana umepata neema mbele zangu, nami nakujua jina lako. Kutoka 33:17

Yahweh said to Moses, "I will do this thing also that you have spoken; for you have found favor in my sight, and I know you by name."

Akasema, Nakusihi unionyeshe utukufu wako. Kutoka 33:18

He said, "Please show me your glory."

Akasema, Nitapitisha wema wangu wote mbele yako, nami nitalitangaza jina la Bwana mbele yako; nami nitamfadhili yeye nitakayemfadhili; nitamrehemu yeye nitakayemrehemu. Kutoka 33:19

He said, "I will make all my goodness pass before you, and will proclaim the name of Yahweh before you. I will be gracious to whom I will be gracious, and will show mercy on whom I will show mercy."

Kisha akasema, Huwezi kuniona uso wangu, maana mwanadamu hataniona akaishi. Kutoka 33:20

He said, "You cannot see my face, for man may not see me and live."

Bwana akasema, Tazama, hapa pana mahali karibu nami, nawe utasimama juu ya mwamba; Kutoka 33:21

Yahweh also said, "Behold, there is a place by me, and you shall stand on the rock.

kisha itakuwa wakati unapopita utukufu wangu, nitakutia katika ufa wa ule mwamba, na kukufunika kwa mkono wangu hata nitakapokuwa nimekwisha kupita; Kutoka 33:22

It will happen, while my glory passes by, that I will put you in a cleft of the rock, and will cover you with my hand until I have passed by;

nami nitaondoa mkono wangu, nawe utaniona nyuma yangu, bali uso wangu hautaonekana. Kutoka 33:23

then I will take away my hand, and you will see my back; but my face shall not be seen."