Kutoka 24 Swahili & English

Listen/Download Audio
Kutoka 24 (Swahili) Exodus 24 (English)

Kisha Bwana akamwambia Musa, Kweeni wewe, na Haruni, na Nadabu, na Abihu, na watu sabini wa wazee wa Israeli, mkamfikilie Bwana; mkasujudie kwa mbali; Kutoka 24:1

He said to Moses, "Come up to Yahweh, you, and Aaron, Nadab, and Abihu, and seventy of the elders of Israel; and worship from a distance.

na Musa peke yake ndiye atakayekaribia karibu na Bwana; lakini hao hawatakaribia karibu; wala hao watu hawatakwea pamoja naye. Kutoka 24:2

Moses alone shall come near to Yahweh, but they shall not come near, neither shall the people go up with him."

Musa akaenda akawaambia watu maneno yote ya Bwana, na hukumu zake zote; watu wote wakajibu kwa sauti moja, wakasema, Maneno yote aliyoyanena Bwana tutayatenda. Kutoka 24:3

Moses came and told the people all the words of Yahweh, and all the ordinances; and all the people answered with one voice, and said, "All the words which Yahweh has spoken will we do."

Basi Musa akayaandika maneno yote ya Bwana, akaondoka asubuhi na mapema, akajenga madhabahu chini ya mlima, na nguzo kumi na mbili, kwa hesabu ya kabila kumi na mbili za Israeli, Kutoka 24:4

Moses wrote all the words of Yahweh, and rose up early in the morning, and built an altar under the mountain, and twelve pillars for the twelve tribes of Israel.

akapeleka vijana wa wana wa Israeli, waliotoa sadaka za kuteketezwa, wakamchinjia Bwana sadaka za amani za ng'ombe. Kutoka 24:5

He sent young men of the children of Israel, who offered burnt offerings and sacrificed peace-offerings of oxen to Yahweh.

Musa akatwaa nusu ya ile damu, akaitia katika mabakuli; na nusu ya ile damu akainyunyiza juu ya madhabahu. Kutoka 24:6

Moses took half of the blood and put it in basins, and half of the blood he sprinkled on the altar.

Kisha akakitwaa kitabu cha agano akakisoma masikioni mwa watu; wakasema, Hayo yote aliyoyanena Bwana tutayatenda, nasi tutatii. Kutoka 24:7

He took the book of the covenant and read it in the hearing of the people, and they said, "All that Yahweh has spoken will we do, and be obedient."

Musa akaitwaa ile damu, akawanyunyizia watu, akasema, Hii ndiyo damu ya agano alilolifanya Bwana pamoja nanyi katika maneno haya yote. Kutoka 24:8

Moses took the blood, and sprinkled it on the people, and said, "Look, this is the blood of the covenant, which Yahweh has made with you concerning all these words."

Ndipo akakwea juu, Musa, na haruni, na Nadabu, na Abihu, na watu sabini miongoni mwa wazee wa Israeli; Kutoka 24:9

Then Moses, Aaron, Nadab, Abihu, and seventy of the elders of Israel went up.

wakamwona Mungu wa Israeli; chini ya miguu yake palikuwa na kama sakafu iliyofanyizwa kwa yakuti samawi, kama zile mbingu zenyewe kwa usafi wake. Kutoka 24:10

They saw the God of Israel. Under his feet was like a paved work of sapphire{or, lapis lazuli} stone, like the skies for clearness.

Naye hakuweka mkono wake juu ya hao wakuu wa wana wa Israeli; nao wakamwona Mungu, wakala na kunywa. Kutoka 24:11

He didn't lay his hand on the nobles of the children of Israel. They saw God, and ate and drank.

Bwana akamwambia Musa, Njoo huku juu kwangu mlimani, uwe huku; nami nitakupa mbao za mawe na ile sheria na hiyo amri niliyoiandika ili uwafundishe. Kutoka 24:12

Yahweh said to Moses, "Come up to me on the mountain, and stay here, and I will give you the tables of stone with the law and the commands that I have written, that you may teach them."

Musa akaondoka na Yoshua, mtumishi wake, Musa akapanda mlimani kwa Mungu. Kutoka 24:13

Moses rose up with Joshua, his servant, and Moses went up onto God's Mountain.

Akawaambia hao wazee, Tungojeeni hapa, mpaka tutakaporudi kwenu; na tazameni, Haruni na Huri wapo pamoja nanyi; kila mtu aliye na neno na awaendee. Kutoka 24:14

He said to the elders, "Wait here for us, until we come again to you. Behold, Aaron and Hur are with you. Whoever is involved in a dispute can go to them."

Musa akapanda mlimani, lile wingu likaufunikiza mlima. Kutoka 24:15

Moses went up on the mountain, and the cloud covered the mountain.

Na huo utukufu wa Bwana ukakaa juu ya mlima wa Sinai; lile wingu likaufunikiza siku sita; na siku ya saba akamwita Musa toka kati ya lile wingu. Kutoka 24:16

The glory of Yahweh settled on Mount Sinai, and the cloud covered it six days. The seventh day he called to Moses out of the midst of the cloud.

Na kuonekana kwake ule utukufu wa Bwana kulikuwa kama moto uteketezao, juu ya mlima machoni pa wana wa Israeli. Kutoka 24:17

The appearance of the glory of Yahweh was like devouring fire on the top of the mountain in the eyes of the children of Israel.

Musa akaingia ndani ya lile wingu, akapanda mlimani; Musa akawa humo katika ule mlima siku arobaini, mchana na usiku. Kutoka 24:18

Moses entered into the midst of the cloud, and went up on the mountain; and Moses was on the mountain forty days and forty nights.