Kutoka 36 Swahili & English

Listen/Download Audio
Kutoka 36 (Swahili) Exodus 36 (English)

Basi Bezaleli na Oholiabu watatenda kazi, na kila mtu mwenye moyo wa hekima, ambaye Bwana amemtia akili na hekima ili ajue kufanya kazi hiyo yote kwa huo utumishi wa mahali patakatifu, kama hayo yote Bwana aliyoyaagiza. Kutoka 36:1

"Bezalel and Oholiab shall work with every wise-hearted man, in whom Yahweh has put wisdom and understanding to know how to work all the work for the service of the sanctuary, according to all that Yahweh has commanded."

Basi Musa akawaita Bezaleli na Oholiabu, na kila mtu aliyekuwa na moyo wa akili, ambaye Bwana alimtia moyoni mwake hekima, kila mtu ambaye moyo wake ulimhimiza ili aende kuifanya kazi hiyo; Kutoka 36:2

Moses called Bezalel and Oholiab, and every wise-hearted man, in whose heart Yahweh had put wisdom, even everyone whose heart stirred him up to come to the work to do it:

nao wakapokea mkononi mwa Musa matoleo yote, ambayo hao wana wa Israeli walikuwa wameyaleta kwa ajili ya huo utumishi wa mahali patakatifu, ili wapafanye. Kisha wakamletea matoleo kila siku asubuhi kwa moyo wa kupenda. Kutoka 36:3

and they received from Moses all the offering which the children of Israel had brought for the work of the service of the sanctuary, with which to make it. They brought yet to him freewill-offerings every morning.

Na hao watu wote wenye hekima, waliotumika katika kazi yote ya mahali patakatifu, wakaenda kila mtu kutoka katika kazi yake aliyokuwa akiifanya; Kutoka 36:4

All the wise men, who performed all the work of the sanctuary, each came from his work which they did.

nao wakasema na Musa, na kumwambia, Watu waleta vitu vingi sana zaidi ya hivyo vitoshavyo kwa ajili ya utumishi wa hiyo kazi, ambayo Bwana aliagiza ifanywe. Kutoka 36:5

They spoke to Moses, saying, "The people bring much more than enough for the service of the work which Yahweh commanded to make."

Basi Musa akatoa amri, nao wakatangaza mbiu katika marago yote, wakisema, Wasifanye kazi tena, mtu mume wala mwanamke, kwa ajili ya matoleo kwa mahali patakatifu. Basi watu wakazuiwa wasilete tena. Kutoka 36:6

Moses gave commandment, and they caused it to be proclaimed throughout the camp, saying, "Let neither man nor woman make anything else for the offering for the sanctuary." So the people were restrained from bringing.

Kwani vile vitu walivyokuwa navyo vilikuwa vyatosha kwa kuifanya kazi hiyo yote, kisha vilizidi. Kutoka 36:7

For the stuff they had was sufficient for all the work to make it, and too much.

Basi kila mtu mwenye moyo wa hekima miongoni mwa hao waliofanya kazi, akaifanya hiyo maskani ya mapazia kumi; ya nguo ya kitani nzuri ya kusokotwa, na nyuzi za rangi ya samawi, na za rangi ya zambarau, na nyekundu; pamoja na makerubi, kazi ya fundi stadi; ndivyo alivyoyafanya. Kutoka 36:8

All the wise-hearted men among those who did the work made the tent with ten curtains; of fine twined linen, blue, purple, and scarlet, with cherubim, the work of the skillful workman, they made them.

Urefu wa kila pazia ulikuwa ni dhiraa ishirini na nane, na upana wa kila pazia ulikuwa ni dhiraa nne; mapazia yote yalikuwa ya kipimo kimoja. Kutoka 36:9

The length of each curtain was twenty-eight cubits, and the breadth of each curtain four cubits. All the curtains had one measure.

Naye akaunganisha mapazia matano hili na hili; na mapazia matano mengine akayaunganisha hili na hili. Kutoka 36:10

He coupled five curtains to one another, and the other five curtains he coupled one to another.

Kisha akafanya matanzi ya rangi ya samawi katika ncha za pazia moja, katika upindo wa kiungo chake; akafanya vivyo katika ncha ya pazia lililokuwa upande wa nje katika kiungo cha pili. Kutoka 36:11

He made loops of blue on the edge of the one curtain from the edge in the coupling. Likewise he made in the edge of the curtain that was outmost in the second coupling.

Akafanya matanzi hamsini katika pazia moja, na matanzi hamsini katika upindo wa pazia lililokuwa katika kiungo cha pili; hayo matanzi yalikuwa yakabiliana hili na hili. Kutoka 36:12

He made fifty loops in the one curtain, and he made fifty loops in the edge of the curtain that was in the second coupling. The loops were opposite one to another.

Kisha akafanya vifungo hamsini vya dhahabu, na kuyaunganya hayo mapazia hili na hili kwa vile vifungo; hivi ile maskani ilikuwa ni moja. Kutoka 36:13

He made fifty clasps of gold, and coupled the curtains one to another with the clasps: so the tent was a unit.

Kisha akafanya vifuniko vya singa za mbuzi kuwa hema ya kuifunika hiyo maskani; akafanya mapazia kumi na moja. Kutoka 36:14

He made curtains of goats' hair for a covering over the tent. He made them eleven curtains.

Urefu wa kila pazia ulikuwa ni dhiraa thelathini, na upana wa kila pazia ulikuwa ni dhiraa nne; hayo mapazia yote kumi na moja yalikuwa ya kipimo kimoja. Kutoka 36:15

The length of each curtain was thirty cubits, and four cubits the breadth of each curtain. The eleven curtains had one measure.

Naye akaunganya mapazia matano mbali, na mapazia sita mbali. Kutoka 36:16

He coupled five curtains by themselves, and six curtains by themselves.

Kisha akafanya matanzi hamsini katika upindo wa pazia lililo upande wa nje katika kile kiungo, naye akafanya matanzi hamsini katika ncha ya pazia lililokuwa upande wa nje katika kiungo cha pili. Kutoka 36:17

He made fifty loops on the edge of the curtain that was outmost in the coupling, and he made fifty loops on the edge of the curtain which was outmost in the second coupling.

Kisha akafanya vifungo hamsini vya shaba aiunganye ile hema pamoja, ili iwe hema moja. Kutoka 36:18

He made fifty clasps of brass to couple the tent together, that it might be a unit.

Kisha akafanya kifuniko kwa ajili ya hiyo hema cha ngozi za kondoo waume zilizotiwa rangi nyekundu; tena juu yake akafanya kifuniko cha ngozi za pomboo. Kutoka 36:19

He made a covering for the tent of rams' skins dyed red, and a covering of sea cow hides above.

Kisha akafanya mbao za mti wa mshita kwa hiyo maskani, zilizosimama. Kutoka 36:20

He made the boards for the tent of acacia wood, standing up.

Urefu wa kila ubao ulikuwa ni dhiraa kumi, na upana wa kila ubao ulikuwa ni dhiraa moja na nusu. Kutoka 36:21

Ten cubits was the length of a board, and a cubit and a half the breadth of each board.

Kila ubao ulikuwa na ndimi mbili, zilizounganywa pamoja; ndivyo alivyozifanya hizo mbao zote za maskani. Kutoka 36:22

Each board had two tenons, joined one to another. He made all the boards of the tent this way.

Naye akazifanya hizo mbao kwa ajili ya hiyo maskani; mbao ishirini kwa upande wa kusini kuelekea kusini; Kutoka 36:23

He made the boards for the tent: twenty boards for the south side southward.

naye akafanya matako ya fedha arobaini yawe chini ya hizo mbao ishirini; matako mawili chini ya ubao mmoja kwa hizo ndimi zake mbili, na matako mawili chini ya ubao mwingine kwa ndimi zake mbili. Kutoka 36:24

He made forty sockets of silver under the twenty boards; two sockets under one board for its two tenons, and two sockets under another board for its two tenons.

Na kwa upande wa pili wa maskani upande wa kaskazini, akafanya mbao ishirini, Kutoka 36:25

For the second side of the tent, on the north side, he made twenty boards,

na matako yake ya fedha arobaini; matako mawili chini ya ubao mmoja, na matako mawili chini ya ubao mwingine. Kutoka 36:26

and their forty sockets of silver; two sockets under one board, and two sockets under another board.

Na kwa upande wa nyuma wa hiyo maskani kuelekea magharibi akafanya mbao sita. Kutoka 36:27

For the far part of the tent westward he made six boards.

Naye akafanya mbao mbili kwa pembe za maskani upande wa nyuma. Kutoka 36:28

He made two boards for the corners of the tent in the far part.

Nazo zilikuwa mbao pacha upande wa chini, vivyo zilishikamana pamoja hata ncha ya juu kufikilia pete ya kwanza; ndivyo alivyofanya zote mbili katika hizo pembe mbili. Kutoka 36:29

They were double beneath, and in like manner they were all the way to the top of it to one ring. He did thus to both of them in the two corners.

Hivyo zilikuwa mbao nane, na matako yake ya fedha, matako kumi na sita, matako mawili chini ya kila ubao. Kutoka 36:30

There were eight boards, and their sockets of silver, sixteen sockets; under every board two sockets.

Kisha akafanya mataruma ya miti ya mshita; matano kwa mbao za upande mmoja wa maskani; Kutoka 36:31

He made bars of acacia wood; five for the boards of the one side of the tent,

na mataruma matano kwa mbao za upande wa pili wa maskani, na mataruma matano kwa hizo mbao za maskani zilizokuwa upande wa nyuma kuelekea magharibi. Kutoka 36:32

and five bars for the boards of the other side of the tent, and five bars for the boards of the tent for the hinder part westward.

Naye akalifanya hilo taruma la katikati lipenye kati ya hizo mbao kutoka upande huu hata upande huu. Kutoka 36:33

He made the middle bar to pass through in the midst of the boards from the one end to the other.

Naye akazifunika hizo mbao dhahabu, akazifanya zile pete zake za dhahabu ziwe mahali pa hayo mataruma, akayafunika dhahabu hayo mataruma. Kutoka 36:34

He overlaid the boards with gold, and made their rings of gold for places for the bars, and overlaid the bars with gold.

Kisha akafanya hilo pazia la nyuzi za rangi ya samawi, na za rangi ya zambarau, na nyekundu, na kitani nzuri zilizosokotwa; akatia na makerubi kazi ya fundi stadi, ndivyo alivyofanya. Kutoka 36:35

He made the veil of blue, purple, scarlet, and fine twined linen: with cherubim. He made it the work of a skillful workman.

Naye akafanya kwa ajili yake nguzo nne za mti wa mshita, akazifunika dhahabu; na kulabu zake zilikuwa za dhahabu; naye akasubu kwa ajili yake matako manne ya fedha. Kutoka 36:36

He made four pillars of acacia for it, and overlaid them with gold. Their hooks were of gold. He cast four sockets of silver for them.

Kisha akafanya pazia la sitara kwa ajili ya mlango wa Hema, la nguo ya rangi ya samawi, na ya rangi ya zambarau, na nyekundu, na nguo ya kitani nzuri ya kusokotwa, kazi ya mwenye kutia taraza, Kutoka 36:37

He made a screen for the door of the tent, of blue, purple, scarlet, and fine twined linen, the work of an embroiderer;

na nguzo zake tano pamoja na kulabu zake; naye akavifunika dhahabu vichwa vyake na vifungo vyake; na matako yake matano yalikuwa ya shaba. Kutoka 36:38

and the five pillars of it with their hooks. He overlaid their capitals and their fillets with gold, and their five sockets were of brass.