Kutoka 35 Swahili & English

Listen/Download Audio
Kutoka 35 (Swahili) Exodus 35 (English)

Musa akakutanisha mkutano wote wa wana wa Israeli, na kuwaambia, Maneno aliyoyausia Bwana ni haya, kwamba myafanye. Kutoka 35:1

Moses assembled all the congregation of the children of Israel, and said to them, "These are the words which Yahweh has commanded, that you should do them.

Fanyeni kazi siku sita, lakini siku ya saba itakuwa siku takatifu kwenu; ni Sabato ya kustarehe kabisa kwa Bwana; mtu awaye yote atakayefanya kazi yo yote katika siku hiyo atauawa. Kutoka 35:2

'Six days shall work be done, but on the seventh day there shall be a holy day for you, a Sabbath of solemn rest to Yahweh: whoever does any work in it shall be put to death.

Hamtawasha moto katika nyumba zenu kwa siku ya Sabato. Kutoka 35:3

You shall kindle no fire throughout your habitations on the Sabbath day.'"

Kisha Musa akanena na mkutano wote wa wana wa Israeli, akawaambia, Neno hili ndilo aliloliamuru Bwana, akisema, Kutoka 35:4

Moses spoke to all the congregation of the children of Israel, saying, "This is the thing which Yahweh commanded, saying,

Katwaeni kati yenu matoleo kwa Bwana; mtu awaye yote aliye na moyo wa kupenda, ayalete matoleo; dhahabu na fedha na shaba; Kutoka 35:5

'Take from among you an offering to Yahweh. Whoever is of a willing heart, let him bring it, Yahweh's offering: gold, silver, brass,

na nyuzi za rangi ya samawi, na za rangi ya zambarau, na za rangi nyekundu, na kitani nzuri, na singa za mbuzi; Kutoka 35:6

blue, purple, scarlet, fine linen, goats' hair,

na ngozi za kondoo waume zilizotiwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo, na mbao za mshita; Kutoka 35:7

rams' skins dyed red, sea cow hides, acacia wood,

na mafuta kwa hiyo taa, na viungo vya manukato kwa hayo mafuta ya kutiwa, na kwa huo uvumba mzuri; Kutoka 35:8

oil for the light, spices for the anointing oil and for the sweet incense,

na vito vya shohamu, na vito vya kutiwa kwa hiyo naivera, na kwa hicho kifuko cha kifuani. Kutoka 35:9

onyx stones, and stones to be set for the ephod and for the breastplate.

Na kila mtu kati yenu aliye na moyo wa hekima na aje, na kuyafanya hayo yote ambayo Bwana ameyaagiza; Kutoka 35:10

"Let every wise-hearted man among you come, and make all that Yahweh has commanded:

yaani, hiyo maskani na hema yake, na kifuniko chake, na vifungo vyake, na mbao zake, na mataruma yake, na viguzo vyake, na matako yake; Kutoka 35:11

the tent, its outer covering, its roof, its clasps, its boards, its bars, its pillars, and its sockets;

hilo sanduku, na miti yake, na hicho kiti cha rehema, na lile pazia la sitara; Kutoka 35:12

the ark, and its poles, the mercy seat, the veil of the screen;

na hiyo meza, na miti yake, na vyombo vyake vyote, na hiyo mikate ya wonyesho; Kutoka 35:13

the table with its poles and all its vessels, and the show bread;

na hicho kinara cha taa kwa mwanga, na vyombo vyake, na taa zake, na hayo mafuta kwa nuru; Kutoka 35:14

the lampstand also for the light, with its vessels, its lamps, and the oil for the light;

na hiyo madhabahu ya kufukizia uvumba, na miti yake, na hayo mafuta ya kupaka, na huo uvumba mzuri, na hicho kisitiri cha mlango, mlangoni mwa hiyo maskani; Kutoka 35:15

and the altar of incense with its poles, the anointing oil, the sweet incense, the screen for the door, at the door of the tent;

na hiyo madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa, pamoja na wavu wake wa shaba, na miti yake, na vyombo vyake vyote, na hilo birika na tako lake; Kutoka 35:16

the altar of burnt offering, with its grating of brass, it poles, and all its vessels, the basin and its base;

na hizo kuta za nguo za ua, na viguzo vyake, na matako yake, na pazia la lango la ua; Kutoka 35:17

the hangings of the court, its pillars, their sockets, and the screen for the gate of the court;

na vile vigingi vya maskani, na vigingi vya ua, na kamba zake Kutoka 35:18

the pins of the tent, the pins of the court, and their cords;

na mavazi yenye kufumwa kwa uzuri, kwa ajili ya kutumika ndani ya mahali patakatifu, hayo mavazi matakatifu ya Haruni kuhani, na mavazi ya wanawe, ili kutumika katika kazi ya ukuhani. Kutoka 35:19

the finely worked garments, for ministering in the holy place, the holy garments for Aaron the priest, and the garments of his sons, to minister in the priest's office.'"

Basi mkutano wote wa wana wa Israeli wakaondoka hapo mbele ya Musa. Kutoka 35:20

All the congregation of the children of Israel departed from the presence of Moses.

Wakaja kila mtu ambaye moyo wake ulimhimiza, na kila mtu ambaye roho yake ilimfanya kuwa apenda, nao wakaleta sadaka za kumpa Bwana, kwa kazi ya hema ya kukutania, na kwa utumishi wake, na kwa hayo mavazi matakatifu. Kutoka 35:21

They came, everyone whose heart stirred him up, and everyone whom his spirit made willing, and brought Yahweh's offering, for the work of the tent of meeting, and for all of its service, and for the holy garments.

Nao wakaja, waume kwa wake, wote waliokuwa na moyo wa kupenda, wakaleta vipini, na hazama, na pete za muhuri, na vikuku, na vyombo vyote vya dhahabu; kila mtu aliyetoa toleo la dhahabu la kumpa Bwana. Kutoka 35:22

They came, both men and women, as many as were willing-hearted, and brought brooches, ear-rings, signet-rings, and armlets, all jewels of gold; even every man who offered an offering of gold to Yahweh.

Tena kila mtu aliyeona kwake nyuzi za rangi ya samawi, na nyuzi za rangi ya zambarau, na nyekundu, na kitani nzuri, na singa za mbuzi, na ngozi za kondoo waume zilizotiwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo, akavileta. Kutoka 35:23

Everyone, with whom was found blue, purple, scarlet, fine linen, goats' hair, rams' skins dyed red, and sea cow hides, brought them.

Kila mtu aliyetoa toleo la fedha, na la shaba, akaileta sadaka ya Bwana; na kila mtu, aliyeona kwake mti wa mshita kwa kazi yo yote ya huo utumishi, akauleta. Kutoka 35:24

Everyone who did offer an offering of silver and brass brought Yahweh's offering; and everyone, with whom was found acacia wood for any work of the service, brought it.

Na wanawake wote waliokuwa na mioyo ya hekima, walisokota kwa mikono yao, nao wakaleta hizo walizokuwa wamezisokota, nguo za rangi ya samawi, na za rangi ya zambarau, na hizo nyuzi nyekundu, na hiyo nguo ya kitani nzuri. Kutoka 35:25

All the women who were wise-hearted spun with their hands, and brought that which they had spun, the blue, the purple, the scarlet, and the fine linen.

Na wanawake wote ambao mioyo yao iliwahimiza katika hekima wakasokota hizo singa za mbuzi. Kutoka 35:26

All the women whose heart stirred them up in wisdom spun the goats' hair.

Na hao wakuu wakavileta vile vito vya shohamu, na vito vya kutiwa, kwa hiyo naivera, na kwa hicho kifuko cha kifuani, Kutoka 35:27

The rulers brought the onyx stones, and the stones to be set, for the ephod and for the breastplate;

na viungo vya manukato, na mafuta; kwa hiyo taa, na kwa hayo mafuta ya kutiwa, na kwa huo uvumba mzuri. Kutoka 35:28

and the spice, and the oil for the light, for the anointing oil, and for the sweet incense.

Wana wa Israeli wakaleta sadaka za kumpa Bwana kwa moyo wa kupenda; wote, waume kwa wake, ambao mioyo yao iliwafanya kuwa wapenda kuleta kwa hiyo kazi, ambayo Bwana aliamuru ifanywe kwa mkono wa Musa. Kutoka 35:29

The children of Israel brought a freewill offering to Yahweh; every man and woman, whose heart made them willing to bring for all the work, which Yahweh had commanded to be made by Moses.

Kisha Musa akawaambia wana wa Israeli, Angalieni, Bwana amemwita kwa jina lake Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila ya Yuda; Kutoka 35:30

Moses said to the children of Israel, "Behold, Yahweh has called by name Bezalel the son of Uri, the son of Hur, of the tribe of Judah.

naye amemjaza roho ya Mungu, katika hekima, na akili, na ujuzi, na kazi ya ustadi kila aina; Kutoka 35:31

He has filled him with the Spirit of God, in wisdom, in understanding, in knowledge, and in all manner of workmanship;

na kuvumbua kazi za werevu, na kufanya kazi ya dhahabu, na fedha, na shaba, Kutoka 35:32

and to make skillful works, to work in gold, in silver, in brass,

na kukata vito vya kutilia, na kuchora miti, atumike katika kazi za werevu kila aina. Kutoka 35:33

in cutting of stones for setting, and in carving of wood, to work in all kinds of skillful workmanship.

Naye amemtilia moyoni mwake ili apate kufundisha, yeye, na Oholiabu mwana wa Ahisamaki, wa kabila ya Dani. Kutoka 35:34

He has put in his heart that he may teach, both he, and Oholiab, the son of Ahisamach, of the tribe of Dan.

Amewajaza watu hao akili za moyoni, ili watumike katika kazi kila aina, ya mwenye kuchora mawe, na kazi ya werevu, na ya mwenye kutia taraza, katika nyuzi za rangi ya samawi, na za rangi ya zambarau, na nyekundu, na kitani nzuri, na ya mwenye kufuma nguo; ya hao wafanyao kazi yo yote, na ya wenye kuvumbua kazi za werevu.

Kutoka 35:35

He has filled them with wisdom of heart, to work all manner of workmanship, of the engraver, of the skillful workman, and of the embroiderer, in blue, in purple, in scarlet, and in fine linen, and of the weaver, even of those who do any workmanship, and of those who make skillful works.