1
Ndipo Bwana akamjibu Ayubu katika upepo wa kisulisuli, na kusema,
Then the LORD answered Job out of the whirlwind and said:
2
Ni nani huyu atiaye mashauri giza Kwa maneno yasiyo na maarifa?
“Who is this who obscures My counsel by words without knowledge?
3
Basi jifunge viuno kama mwanamume, Maana nitakuuliza neno, nawe niambie.
Now brace yourself like a man; I will question you, and you shall inform Me.
4
Ulikuwa wapi nilipoiweka misingi ya nchi? Haya! Sema, kama ukiwa na ufahamu.
Where were you when I laid the foundations of the earth? Tell Me, if you have understanding.
5
Ni nani aliyeamrisha vipimo vyake, kama ukijua? Au ni nani aliyenyosha kamba juu yake?
Who fixed its measurements? Surely you know! Or who stretched a measuring line across it?
6
Misingi yake ilikazwa juu ya kitu gani? Au ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni,
On what were its foundations set, or who laid its cornerstone,
7
Hapo nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, Na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
while the morning stars sang together and all the sons of God shouted for joy?
8
Au ni nani aliyeifunga bahari kwa milango, Hapo ilipofurika kana kwamba imetoka tumboni.
Who enclosed the sea behind doors when it burst forth from the womb,
9
Nilipolifanya wingu kuwa vazi lake, Na giza zito kuwa nguo ya kuifungia,
when I made the clouds its garment and thick darkness its blanket,
10
Nikaiagiza amri yangu; Nikaiwekea makomeo na milango,
when I fixed its boundaries and set in place its bars and doors,
11
Nikasema, Utafika mpaka hapa, lakini hutapita, Na hapa mawimbi yako yanyetayo yatazuiliwa?
and I declared: ‘You may come this far, but no farther; here your proud waves must stop’?
12
Je! Umeiamuru asubuhi tangu siku zako zilipoanza? Umeyajulisha mapambazuko mahali pake?
In your days, have you commanded the morning or assigned the dawn its place,
13
Yapate kuishika miisho ya nchi, Waovu wakung'utwe wakawe mbali nayo?
that it might spread to the ends of the earth and shake the wicked out of it?
14
Hubadilika mfano wa udongo chini ya muhuri, Vitu vyote vinatokea kama mavazi.
The earth takes shape like clay under a seal; its hills stand out like the folds of a garment.
15
Na waovu nuru yao huzuiliwa isiwafikie, Na mkono ulioinuka huvunjika.
Light is withheld from the wicked, and their upraised arm is broken.
16
Je! Umeziingia chemchemi za bahari, Au umetembea mahali pa siri pa vilindi?
Have you journeyed to the vents of the sea or walked in the trenches of the deep?
17
Je! Umefunuliwa malango ya mauti, Au umeyaona malango ya kuzimu?
Have the gates of death been revealed to you? Have you seen the gates of the shadow of death?
18
Umeyafahamu mapana ya dunia? Haya! Sema, ikiwa unayajua hayo yote.
Have you surveyed the extent of the earth? Tell Me, if you know all this.
19
Iko wapi njia ya kuyafikia makao ya nuru? Na giza pia, mahali pake ni wapi?
Where is the way to the home of light? Do you know where darkness resides,
20
Upate kuipeleka hata mpaka wake, Upate kuelewa na mapito ya kuiendea nyumba yake?
so you can lead it back to its border? Do you know the paths to its home?
21
Hukosi unajua, maana ulizaliwa wakati huo, Na hesabu ya siku zako ni kubwa!
Surely you know, for you were already born! And the number of your days is great!
22
Je! Umeziingia ghala za theluji, Au umeziona ghala za mvua ya mawe,
Have you entered the storehouses of snow or observed the storehouses of hail,
23
Nilizoziweka akiba kwa wakati wa misiba, Kwa siku ya mapigano na vita?
which I hold in reserve for times of trouble, for the day of war and battle?
24
Je! Nuru hutengwa kwa njia gani, Au upepo wa mashariki hutawanywaje juu ya nchi?
In which direction is the lightning dispersed, or the east wind scattered over the earth?
25
Ni nani aliyepasua mfereji kwa maji ya gharika, Au njia kwa umeme wa radi;
Who cuts a channel for the flood or clears a path for the thunderbolt,
26
Kunyesha mvua juu ya nchi isiyo na watu; Juu ya jangwa asiyokaa mwanadamu;
to bring rain on a barren land, on a desert where no man lives,
27
Kuishibisha nchi iliyo kame na ukiwa, Na kuyameza majani yaliyo mororo?
to satisfy the parched wasteland and make it sprout with tender grass?
28
Je! Mvua ina baba? Au ni nani aliyeyazaa matone ya umande?
Does the rain have a father? Who has begotten the drops of dew?
29
Barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na sakitu ya mbinguni ni nani aliyeizaa?
From whose womb does the ice emerge? Who gives birth to the frost from heaven,
30
Maji hugandamana kama jiwe, Na uso wa vilindi huganda kwa baridi.
when the waters become hard as stone and the surface of the deep is frozen?
31
Je! Waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia, Au kuvilegeza vifungo vya Orioni?
Can you bind the chains of the Pleiades or loosen the belt of Orion?
32
Je! Waweza kuziongoza Sayari kwa wakati wake? Au waweza kuongoza Dubu na watoto wake?
Can you bring forth the constellations in their seasons or lead out the Bear and her cubs?
33
Je! Unazijua amri zilizoamuriwa mbingu? Waweza kuyathibitisha mamlaka yake juu ya dunia?
Do you know the laws of the heavens? Can you set their dominion over the earth?
34
Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, ili wingi wa maji ukufunikize?
Can you command the clouds so that a flood of water covers you?
35
Waweza kuutuma umeme, nao ukaenda, Ukakuambia, Sisi tupo hapa?
Can you send the lightning bolts on their way? Do they report to you, ‘Here we are’?
36
Je! Ni nani aliyetia hekima moyoni? Au ni nani aliyetia ufahamu rohoni?
Who has put wisdom in the heart or given understanding to the mind?
37
Ni nani awezaye kuyahesabu mawingu kwa hekima? Au ni nani awezaye kuzimimina chupa za mbinguni?
Who has the wisdom to count the clouds? Or who can tilt the water jars of the heavens
38
Wakati mavumbi yagandamanapo, Na madongoa kushikamana pamoja?
when the dust hardens into a mass and the clods of earth stick together?
39
Je! Utamwindia simba mke mawindo? Au utashibisha njaa ya simba wachanga,
Can you hunt the prey for a lioness or satisfy the hunger of young lions
40
Waoteapo mapangoni mwao, Wakaapo mafichoni wapate kuvizia?
when they crouch in their dens and lie in wait in the thicket?
41
Ni nani anayempatia kunguru chakula, Makinda yake wanapomlilia Mungu, Na kutanga-tanga kwa kutindikiwa na chakula?
Who provides food for the raven when its young cry out to God as they wander about for lack of food?