Ayabu 23 Swahili & English
Listen/Download AudioAyabu 23 (Swahili) | Job 23 (English) |
---|---|
Ndipo Ayubu akajibu, na kusema, Ayabu 23:1 |
Then Job answered, |
Hata leo mashitaka yangu yana uchungu; Pigo langu ni zito zaidi ya kuugua kwangu. Ayabu 23:2 |
"Even today is my complaint rebellious. His hand is heavy in spite of my groaning. |
Laiti ningejua mahali niwezapo kumwona, Nifike hata hapo anapokaa! Ayabu 23:3 |
Oh that I knew where I might find him! That I might come even to his seat! |
Ningeiweka daawa yangu mbele yake, Na kukijaza kinywa changu hoja. Ayabu 23:4 |
I would set my cause in order before him, And fill my mouth with arguments. |
Ningeyajua maneno atakayonijibu, Na kuelewa na hayo atakayoniambia. Ayabu 23:5 |
I would know the words which he would answer me, And understand what he would tell me. |
Je! Angeshindana nami kwa ukuu wa uwezo wake? La, lakini angenisikiliza. Ayabu 23:6 |
Would he contend with me in the greatness of his power? No, but he would listen to me. |
Hapo walekevu wangepata kuhojiana naye; Basi hivyo ningeachiliwa na mwamuzi wangu milele. Ayabu 23:7 |
There the upright might reason with him, So I should be delivered forever from my judge. |
Tazama, naenda mbele, wala hayuko; Narudi nyuma, lakini siwezi kumwona; Ayabu 23:8 |
"If I go east, he is not there; If west, I can't find him; |
Na mkono wa kushoto, afanyapo kazi, lakini siwezi kumwona; Hujificha upande wa kuume, hata nisimwone. Ayabu 23:9 |
He works to the north, but I can't see him; He turns south, but I can't catch a glimpse of him. |
Lakini yeye aijua njia niendeayo; Akisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu. Ayabu 23:10 |
But he knows the way that I take. When he has tried me, I shall come forth like gold. |
Mguu wangu umeshikamana sana na hatua zake; Njia yake nimeishika, wala sikukengeuka. Ayabu 23:11 |
My foot has held fast to his steps. His way have I kept, and not turned aside. |
Sikurudi nyuma kuiacha amri ya midomo yake; Nimeyatunza maneno ya kinywa chake zaidi ya riziki yangu, Ayabu 23:12 |
I haven't gone back from the commandment of his lips. I have treasured up the words of his mouth more than my necessary food. |
Lakini yeye ni mmoja, ni nani awezaye kumgeuza? Tena nafsi yake ilitakalo, ndilo afanyalo. Ayabu 23:13 |
But he stands alone, and who can oppose him? What his soul desires, even that he does. |
Kwani yeye hulitimiliza hilo nililoamuriwa; Tena mambo mengi kama hayo ya pamoja naye. Ayabu 23:14 |
For he performs that which is appointed for me. Many such things are with him. |
Kwa hiyo naona taabu mbele ya uso wake; Nitakapofikiri, namwogopa. Ayabu 23:15 |
Therefore I am terrified at his presence. When I consider, I am afraid of him. |
Kwani Mungu ameufanya moyo wangu kuzimia, Naye Mwenyezi amenitaabisha; Ayabu 23:16 |
For God has made my heart faint. The Almighty has terrified me. |
Maana sikufadhaishwa kwa sababu ya giza, Wala kwa sababu giza kuu limenifunika uso. Ayabu 23:17 |
Because I was not cut off before the darkness, Neither did he cover the thick darkness from my face. |