Ayabu 23 Swahili & English

Listen/Download Audio
Ayabu 23 (Swahili) Job 23 (English)

Ndipo Ayubu akajibu, na kusema, Ayabu 23:1

Then Job answered,

Hata leo mashitaka yangu yana uchungu; Pigo langu ni zito zaidi ya kuugua kwangu. Ayabu 23:2

"Even today is my complaint rebellious. His hand is heavy in spite of my groaning.

Laiti ningejua mahali niwezapo kumwona, Nifike hata hapo anapokaa! Ayabu 23:3

Oh that I knew where I might find him! That I might come even to his seat!

Ningeiweka daawa yangu mbele yake, Na kukijaza kinywa changu hoja. Ayabu 23:4

I would set my cause in order before him, And fill my mouth with arguments.

Ningeyajua maneno atakayonijibu, Na kuelewa na hayo atakayoniambia. Ayabu 23:5

I would know the words which he would answer me, And understand what he would tell me.

Je! Angeshindana nami kwa ukuu wa uwezo wake? La, lakini angenisikiliza. Ayabu 23:6

Would he contend with me in the greatness of his power? No, but he would listen to me.

Hapo walekevu wangepata kuhojiana naye; Basi hivyo ningeachiliwa na mwamuzi wangu milele. Ayabu 23:7

There the upright might reason with him, So I should be delivered forever from my judge.

Tazama, naenda mbele, wala hayuko; Narudi nyuma, lakini siwezi kumwona; Ayabu 23:8

"If I go east, he is not there; If west, I can't find him;

Na mkono wa kushoto, afanyapo kazi, lakini siwezi kumwona; Hujificha upande wa kuume, hata nisimwone. Ayabu 23:9

He works to the north, but I can't see him; He turns south, but I can't catch a glimpse of him.

Lakini yeye aijua njia niendeayo; Akisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu. Ayabu 23:10

But he knows the way that I take. When he has tried me, I shall come forth like gold.

Mguu wangu umeshikamana sana na hatua zake; Njia yake nimeishika, wala sikukengeuka. Ayabu 23:11

My foot has held fast to his steps. His way have I kept, and not turned aside.

Sikurudi nyuma kuiacha amri ya midomo yake; Nimeyatunza maneno ya kinywa chake zaidi ya riziki yangu, Ayabu 23:12

I haven't gone back from the commandment of his lips. I have treasured up the words of his mouth more than my necessary food.

Lakini yeye ni mmoja, ni nani awezaye kumgeuza? Tena nafsi yake ilitakalo, ndilo afanyalo. Ayabu 23:13

But he stands alone, and who can oppose him? What his soul desires, even that he does.

Kwani yeye hulitimiliza hilo nililoamuriwa; Tena mambo mengi kama hayo ya pamoja naye. Ayabu 23:14

For he performs that which is appointed for me. Many such things are with him.

Kwa hiyo naona taabu mbele ya uso wake; Nitakapofikiri, namwogopa. Ayabu 23:15

Therefore I am terrified at his presence. When I consider, I am afraid of him.

Kwani Mungu ameufanya moyo wangu kuzimia, Naye Mwenyezi amenitaabisha; Ayabu 23:16

For God has made my heart faint. The Almighty has terrified me.

Maana sikufadhaishwa kwa sababu ya giza, Wala kwa sababu giza kuu limenifunika uso. Ayabu 23:17

Because I was not cut off before the darkness, Neither did he cover the thick darkness from my face.