Ayabu 22 Swahili & English

Listen/Download Audio
Ayabu 22 (Swahili) Job 22 (English)

Ndipo huyo Elifazi Mtemani akajibu, na kusema, Ayabu 22:1

Then Eliphaz the Temanite answered,

Je! Yumkini mtu awaye yote kumfaa Mungu? Hakika yeye aliye na hekima hujifaa mwenyewe. Ayabu 22:2

"Can a man be profitable to God? Surely he who is wise is profitable to himself.

Je! Mwenyezi hupata furaha katika wewe kuwa mwenye haki? Au je, ni faida kwake, kwamba wafanya njia zako kuwa timilifu? Ayabu 22:3

Is it any pleasure to the Almighty, that you are righteous? Or does it benefit him, that you make your ways perfect?

Je! Ni kwa wewe kumcha yeye anakukemea? Na kuingia hukumuni nawe? Ayabu 22:4

Is it for your piety that he reproves you, That he enters with you into judgment?

Je! Uovu wako si mkuu? Wala maovu yako hayana mwisho. Ayabu 22:5

Isn't your wickedness great? Neither is there any end to your iniquities.

Kwa kuwa umetwaa dhamana kwa nduguyo bure, Na kuwavua nguo zao walio uchi. Ayabu 22:6

For you have taken pledges from your brother for nothing, And stripped the naked of their clothing.

Hukumpa maji ya kunywa huyo aliyechoka, Nawe umemnyima chakula huyo mwenye njaa. Ayabu 22:7

You haven't given water to the weary to drink, And you have withheld bread from the hungry.

Lakini huyo shujaa, nchi ilikuwa yake; Na huyo mwenye kusifiwa, yeye aliikaa. Ayabu 22:8

But as for the mighty man, he had the earth. The honorable man, he lived in it.

Umewafukuza wanawake wajane hali ya utupu, Na mikono ya mayatima imevunjwa. Ayabu 22:9

You have sent widows away empty, And the arms of the fatherless have been broken.

Kwa hiyo umezungukwa na mitego, Na hofu ya ghafula yakutaabisha, Ayabu 22:10

Therefore snares are round about you. Sudden fear troubles you,

Au je! Huoni giza, Na maji mengi yanayokufunika? Ayabu 22:11

Or darkness, so that you can not see, And floods of waters cover you.

Je! Mungu hayuko mbinguni juu? Tena tazama umbali wa nyota, jinsi zilivyo juu! Ayabu 22:12

"Isn't God in the heights of heaven? See the height of the stars, how high they are!

Nawe wasema, Mungu anajua nini? Je! Aweza kuamua kati ya giza kuu? Ayabu 22:13

You say, 'What does God know? Can he judge through the thick darkness?

Mawingu mazito ni kifuniko chake, hata asione; Naye yuatembea juu ya kuba ya mbingu. Ayabu 22:14

Thick clouds are a covering to him, so that he doesn't see. He walks on the vault of the sky.'

Je! Utaiandama njia ya zamani Waliyoikanyaga watu waovu? Ayabu 22:15

Will you keep the old way Which wicked men have trodden,

Ambao walinyakuliwa kabla ya wakati wao, Msingi wao ulimwagika kama kijito cha maji; Ayabu 22:16

Who were snatched away before their time, Whose foundation was poured out as a stream,

Waliomwambia Mungu, Tuondokee; Tena, Huyo Mwenyezi aweza kutufanyia nini? Ayabu 22:17

Who said to God, 'Depart from us;' And, 'What can the Almighty do for us?'

Naye ndiye aliyezijaza nyumba zao vitu vyema; Lakini mashauri ya waovu na yawe mbali nami. Ayabu 22:18

Yet he filled their houses with good things, But the counsel of the wicked is far from me.

Wenye haki huyaona hayo wakafurahi; Nao wasio na hatia huwacheka; Ayabu 22:19

The righteous see it, and are glad; The innocent ridicule them,

Wasema, Hakika hao waliotuinukia wamekatiliwa mbali, Na mabaki yao moto umeyateketeza. Ayabu 22:20

Saying, 'Surely those who rose up against us are cut off, The fire has consumed the remnant of them.'

Mjue sana Mungu, ili uwe na amani; Ndivyo mema yatakavyokujia. Ayabu 22:21

"Acquaint yourself with him, now, and be at peace. Thereby good shall come to you.

Uyapokee, tafadhali, mafunzo yatokayo kinywani mwake, Na maneno yake yaweke moyoni mwako. Ayabu 22:22

Please receive instruction from his mouth, And lay up his words in your heart.

Ukimrudia Mwenyezi, utajengwa; Ukiuondoa udhalimu mbali na hema yako. Ayabu 22:23

If you return to the Almighty, you shall be built up, If you put away unrighteousness far from your tents.

Nawe hazina zako ziweke mchangani, Na dhahabu ya Ofiri iweke kati ya mawe ya vijito; Ayabu 22:24

Lay your treasure in the dust, The gold of Ophir among the stones of the brooks.

Naye Mwenyezi atakuwa hazina yako, Atakuwa ni fedha ya thamani kwako. Ayabu 22:25

The Almighty will be your treasure, Precious silver to you.

Kwani ndipo utakapojifurahisha katika Mwenyezi, Na kuinua uso wako kumwelekea Mungu. Ayabu 22:26

For then shall you delight yourself in the Almighty, And shall lift up your face to God.

Utamwomba yeye naye atakusikia; Nawe utazitimiliza nadhiri zako. Ayabu 22:27

You shall make your prayer to him, and he will hear you. You shall pay your vows.

Nawe utakusudia neno, nalo litathibitika kwako; Na mwanga utaziangazia njia zako. Ayabu 22:28

You shall also decree a thing, and it shall be established to you. Light shall shine on your ways.

Hapo watakapokuangusha, utasema, Kuna kuinuka tena; Naye mnyenyekevu Mungu atamwokoa. Ayabu 22:29

When they cast down, you shall say, 'be lifted up.' He will save the humble person.

Atamwokoa na huyo asiye na hatia; Naam, utaokolewa kwa sababu ya usafi wa mikono yako.

Ayabu 22:30

He will even deliver him who is not innocent; Yes, he shall be delivered through the cleanness of your hands."